NEW NOEL
JF-Expert Member
- May 21, 2011
- 863
- 407
Wadau,
Kuna hili tangazo la 'tuko wangapi' ambalo linarushwa kwenye vituo vya Radio na Tv sasa. Nataka kulizungumzia hili ambalo linarushwa kwenye Tv. Kwa kweli kwa maadili ninaona si sawa kwa namna ya jinsi lilivyo,hususani ukilitazama lile ambalo linaonesha watu wapo chumbani. Na linarushwa wakati ambao watu wengi wanakuwa na familia zao na wanatazama television. Yaani wakati ambao watoto wanajumuika na wazazi. Ukitazama hata ubora wa tangazo sijauona,kwa sababu ni tangazo ambalo dhumuni lake ni zuri lakini kwa namna ilivyotumika kufikisha ujumbe ni mbovu sana. Jaribu kutazama pale linapoonesha watu wakishikana miili(wanawake kwa wanaume),je mnaona ni sawa? Najua wengine watadai kuwa kizazi cha sasa kinajua kila kitu,lakini hata kama watoto wa sasa wanajua kila kitu tusiruhusu kila jambo kuwa wazi.
Ninatoa sifa ya wale waliotengeneza tangazo linaloruka kwenye Radio,kwani ujumbe wake upo wazi kabisa.
Kuna hili tangazo la 'tuko wangapi' ambalo linarushwa kwenye vituo vya Radio na Tv sasa. Nataka kulizungumzia hili ambalo linarushwa kwenye Tv. Kwa kweli kwa maadili ninaona si sawa kwa namna ya jinsi lilivyo,hususani ukilitazama lile ambalo linaonesha watu wapo chumbani. Na linarushwa wakati ambao watu wengi wanakuwa na familia zao na wanatazama television. Yaani wakati ambao watoto wanajumuika na wazazi. Ukitazama hata ubora wa tangazo sijauona,kwa sababu ni tangazo ambalo dhumuni lake ni zuri lakini kwa namna ilivyotumika kufikisha ujumbe ni mbovu sana. Jaribu kutazama pale linapoonesha watu wakishikana miili(wanawake kwa wanaume),je mnaona ni sawa? Najua wengine watadai kuwa kizazi cha sasa kinajua kila kitu,lakini hata kama watoto wa sasa wanajua kila kitu tusiruhusu kila jambo kuwa wazi.
Ninatoa sifa ya wale waliotengeneza tangazo linaloruka kwenye Radio,kwani ujumbe wake upo wazi kabisa.