Kule nyanda za juu kusini ukipeleka mchumba kutoka Tanga ndugu wanakukatalia kabisa.
Ukikomaa wanaweza wakakufuta hata Kwenye list ya ndugu yao.
Kuna mzee alinisimulia kuwa miaka ya nyuma kuna mwanaume alienda Tanga Kwenye mkonge akaacha mkewe na watoto.
Hakuonekana Kwa muda mrefu.
Akatumwa mdogo mtu kumtafuta naye hakurudi tena
Akatumwa mtoto wa Kaka yake naye hakurudi tena.
Akatumwa binamu naye akapotea
Mjomba vile vile.
Baadaye akatumwa dada mtu.
Kufika huko kakuta ndugu Zake wameoa na Wana familia huko na hawana mipango ya kurudi.
Yeye Ndio akarudisha hiyo taarifa.
Ukawa mwanzo wa kuogopwa Kwa wake wa Tanga. Na ukipangiwa kazi Tanga ndugu wanaanza kuogopa kukupoteza