TANESCO Uyui, mnahujumiwa hapo kata ya Loya na mafundi uchwara!

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,535
17,479
Chama na serikali vikajitahidi sana kufikisha umeme vijijini Ili wananchi wapate huduma hii, na wananchi wakafanya mchakato wa gharama kubwa Ili wapate umeme na kweli wakaupata.

Baada ya kulipia LUKU na kuanzia kupata huduma hii mchezo wa kipumpavu ukaanza hasa na fundi mkuu wa TANESCO akishirikiana na mafundi uchwara ambao Wanakata umeme kama mtoto anazima kibatari na kukiwasha!
Ipo hivi

Wanaweza amua tangu asubuhi hadi jioni umeme ukawepo halafu ikifika muda wa mechi ya Simba au Yanga yaani sekunde chache kabla ya gem kuanza Wanakata umeme ikifika halftime Wana washa Tena halafu mechi ikianza Tena second half Wanakata tena,ni kama kwamba ni maksudi kabisa Ili kuwa KERA wananchi!

Wamejaribu kuwasiliana na viongozi wa chama na serikali katani hapo lakini hakuna Cha maana hata leo wamecheza kamchezo kao,

Nilipouliza kwa kina ni kwanini wanafanya hivyo, Baadhi ya wadau wakasema hao mafundi uchwara wawili wakiongozwa na fundi mkuu katani hapo wanapewa rushwa na wauza Solar na mafuta ya petrol Ili wahusika biashara zao zisidode!!

Chama na serikali vinahujumiwa kumbuka TANESCO lazima warudishe walau gharama za uendeshaji Ili huduma hii iendelee!

Nakumbuka hata ule umeme wa Solar wa aliekua mbunge wa Igalula ulikufa kwa style ya hujuma hadi leo vimebaki chuma chakavu na nguzo zinazooza bila kufanya kazi ya mwanzo na ule umeme ulikufa zipo solar tu pale ambazo ni chuma chakavu!!!

Cha kushangaza Diwani yupo huyo ndio mzembe kweli kweli anachojua ni kuuza duka la dawa, Hashughuliki na changamoto za wananchi, katibu wa chama katani hapo nae Hana sauti Wala viongozi wa chama!!

Zimenifikia nimezituma, wenye mamlaka chukueni hatua!

Mungu ibariki Tanzania, nchi yetu tuipendayo sana!
 
Naamini mkurugenzi mpya Uyui Bi Leokadia hatasita kuchukua hatua, haiwezekani chama na serikali yetu vikahujumiwa hivi!!
 
Habari zinachefua Sana Kama tumevamiwa na kundi la nzige hizi zimekuwa vichomi Sana kwa wananchi uchukuaji wa hatua kwa wananchi wanazotoa malalamiko imekuwa si wakuridhizisha kabisa
 
We jamaa ni mpumbavu sana na ni mshamba pia. Majungu ya mtaani kwenu unayaleta JF ijadiliwe kama ni ajenda ya kitaifa.

Umeme unakatika nchi nzima na hatulalamiki kama wewe, wewe maliza chuki binafsi zako na watu wenu huko huko Loya Igunga kwa utaratibu, na watu wako ukishindwana nao, hama kijiji nenda kakae Itilima au Goweko ambako umeme haukatiki. Toka hapa na meno yako ya kuungua ungua.
 
We jamaa ni mpumbavu sana na ni mshamba pia. Majungu ya mtaani kwenu unayaleta JF ijadiliwe kama ni ajenda ya kitaifa.

Umeme unakatika nchi nzima na hatulalamiki kama wewe, wewe maliza chuki binafsi zako na watu wenu huko huko Loya Igunga kwa utaratibu, na watu wako ukishindwana nao, hama kijiji nenda kakae Itilima au Goweko ambako umeme haukatiki. Toka hapa na meno yako ya kuungua ungua.
Zimenifikia nimezituma wenye mamlaka wachukue hatua!
 
Unapoandika "chama" unamaanisha nini?Chama cha nini?Au unadhani wote tumeshiba nsansa?
Chama na serikali,chama ndicho kilichopewa dhamana na wananchi na serikali ndio inayokusanya kodi na kuwaletea wananchi huduma,

Huelewi nini sasa hapo !!?

Zimenifikia nimezituma wenye mamlaka chukueni hatua
 
Back
Top Bottom