TANESCO Mwanza, kuna mgao rasmi unaendelea?

TANESCO Mwanza, kuna mgao rasmi unaendelea?

Tanesco wana boa sana sio uko tu hata sisi uku Dodoma ikifika mida ya saa kumi jioni hasa muda wa kutazama mpira huwa wanakata,

Najiuliza kwa hii kata kata ya umeme kweli tutafika kwenye uchumi wa viwanda.
Viwanda vya kutazama Mpira??
 
Nasikia huko Mwanza, TANESCO imemsaliti Rais wa wanyonge, kwamba kila ifikapo jioni umeme hugeuka kuwa giza totoro! CCM ni kichaka Cha uhalifu
 
Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mwanza, acha mambo yako, hii ni wiki ya pili sasa kila ilifika saa moja jioni umeme unakatika.

Tatizo hili sasa limekuwa ni "sugu" kwa muda wa wiki mbili na pindi mnapokata umeme taarifa rasmi haitolewi.

Idara ya Mawasiliano na uhusiano inafanya kazi gani? Kwanini hawatoi taarifa? au kazi yao ni ipi hapo ofisini?

Najiuliza kwanini umeme unakatika muda huu wa saa moja kila siku? kama ni matengenezo yanafanyika taarifa ni muhimu kwetu sisi ambao muda huu tunategemea umeme kufanya shughuli zetu.

Lakini kuna taarifa zinaeleza kwamba meneja huyu kaja na mpango wake wakutaka kumfelisha Rais wetu (John Magufuli) katika mkoa huu.

Hivyo kutokana na hali hii, vyombo husika angalieni huyu mtu na watu wake waliomzunguka asije akafanya mambo mabaya zaidi ya hili analojaribu kulufanya.

Charles Charles

Uzi umekaa kimajungu majungu, nahisi kuna shida mahali.
Huo mpango wa meneja kumfelisha JPM umeusikia wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzi umekaa kimajungu majungu, nahisi kuna shida mahali.
Huo mpango wa meneja kumfelisha JPM umeusikia wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Siyo majungu ni wangese sana Tanesco wanafanya mambo kimazoea sana hapa Mwanza na kitengo chao cha mawasiliano hapa wamejazana wa kanda ya kilalacha ni shida wanaona ofisi za babu zao
 
Yawezekana tatizo la umeme likawa la nchi nzima nini
 
Tanesco na Idara ya Maji tangu uhuru hawajawahi kupata tuzo ya aina yoyote, Labda miaka 50 ijayo ndio hayo mashirika yatapata tuzo.

Na siku Tanesco wakipata tuzo jua tupo kwenye uchumi wa juu sana na kila kata imeonganishwa kwa lami

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mwanza, acha mambo yako, hii ni wiki ya pili sasa kila ilifika saa moja jioni umeme unakatika.

Tatizo hili sasa limekuwa ni "sugu" kwa muda wa wiki mbili na pindi mnapokata umeme taarifa rasmi haitolewi.

Idara ya Mawasiliano na uhusiano inafanya kazi gani? Kwanini hawatoi taarifa? au kazi yao ni ipi hapo ofisini?

Najiuliza kwanini umeme unakatika muda huu wa saa moja kila siku? kama ni matengenezo yanafanyika taarifa ni muhimu kwetu sisi ambao muda huu tunategemea umeme kufanya shughuli zetu.

Lakini kuna taarifa zinaeleza kwamba meneja huyu kaja na mpango wake wakutaka kumfelisha Rais wetu (John Magufuli) katika mkoa huu.

Hivyo kutokana na hali hii, vyombo husika angalieni huyu mtu na watu wake waliomzunguka asije akafanya mambo mabaya zaidi ya hili analojaribu kulufanya.

Charles Charles

Acha kulalamika, nenda kavue dagaa. Kuna nini zaidi cha kumfelisha Magufuli zaidi ya kuua demokrasia, uhuru wa kujieleza, haki za binadamu na utawala bora?
 
Ngozi nyeusi ni shida..eti kumhujum Rais..kwani umeme wa Mwanza umeletwa na awamu hii ya tano? Taarifa zinatolewa sana sema wengi mnakua kwenye bar basi taarifa zinawapita kombo
 
Na huku Mbeya wanamsaliti nani, make nako ni hivyo hivyo, kila siku kuanzia saa moja hakuna umeme, hata sasa maeneo yote ya nane nane, ilomba n.k hakuna umeme na ni wiki sasa inakuwa hivyo kila siku.
Nasikia huko Mwanza, TANESCO imemsaliti Rais wa wanyonge, kwamba kila ifikapo jioni umeme hugeuka kuwa giza totoro! CCM ni kichaka Cha uhalifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom