Tanesco acheni uzembe mtaingiza watu hasara

Nyumisi

JF-Expert Member
Nov 10, 2010
13,405
19,069
Habari wakuu,

Kwa wiki nzima sasa Tanesco wamekuwa wakileta umeme mdogo kwenye baadhi ya maeneo hapa Dar kiasi kwamba kwa sisi ambao tunatumia fridge guard unakuta haiwezi kuruhusu umeme kuwasha friji kwa sababu umeme ni mdogo na kupelekea vitu vilivyohifadhiwa ndani ya friji kuanza kuharibika. Hivyo hivyo ukiwasha vifaa vingine kama feni unaona havina nguvu kabisa.

Pia kumekuwa na washa, kata nyingi, yaani umeme unakatika na kurudi ghafla.

Tanesco kuweni serious, kama hamuwezi kusambaza umeme unaotosha ni bora kuzima tu kuliko kusambambaza umeme mdogo ambao utapelekea kutuharibia vifaa, ukichukulia kwamba hivi vifaa ni gharama sana.​
 
Habari wakuu,

Kwa wiki nzima sasa Tanesco wamekuwa wakileta umeme mdogo kwenye baadhi ya maeneo hapa Dar kiasi kwamba kwa sisi ambao tunatumia fridge guard unakuta haiwezi kuruhusu umeme kuwasha friji kwa sababu umeme ni mdogo na kupelekea vitu vilivyohifadhiwa ndani ya friji kuanza kuharibika. Hivyo hivyo ukiwasha vifaa vingine kama feni unaona havina nguvu kabisa.

Pia kumekuwa na washa, kata nyingi, yaani umeme unakatika na kurudi ghafla.

Tanesco kuweni serious, kama hamuwezi kusambaza umeme unaotosha ni bora kuzima tu kuliko kusambambaza umeme mdogo ambao utapelekea kutuharibia vifaa, ukichukulia kwamba hivi vifaa ni gharama sana.​

Hawa jamaa yaani wanaboa mno halafu hizo simu wala hawapokei kuonyesha kwamba hakuna cha kuwafanya. Laiti kungekuwa na umeme unapatikana kwa njia kama ving'amuzi hawa wababaishaji wangeishia kuwa kama ttcl. Wanakiburi sababu wanajua wapo monopoly , hakuna mshindani nao. Ikifika usiku ndiyo muda wa kukata umeme kila siku ,hapa Arusha mji wa kitalii huwezi amini umeme ni kama kakakuona.
 
Ndugu Mteja,

Tunakuomba uwasiliane na kituo cha watoa huduma wetu kwa msaada zaidi. Ahsante.

Karibu sana.
 
Back
Top Bottom