BILGERT
JF-Expert Member
- Feb 27, 2015
- 6,535
- 10,974
MJINGA WEWE huna hata huelewa maskini.Kama umeajiriwa ishike Ajira yako.
MJINGA WEWE huna hata huelewa maskini.Kama umeajiriwa ishike Ajira yako.
Hongera hamna aliyetajirika siku moja..never give upMnamo tar21 mwez wa tisa mwaka huu nlifungua wakala (mpesa, tigo, airtel, na halotel) kariakoo nakumbuka cku hyo ckufanya muamala hata mmoja. Nliwaza nkamwambia Mungu n nini hiki sasa. Daah wateja wakawa kidogo wanakuja mwanzo wa mwez wa kumi ka kamishen kakaja hakafiki hata elfu hamsini daah kweli nkavunjika moyo sana.
Leo namshukuru Mungu kidogo wateja wanakuja japo nnaamini hadi mwakani nitasmama kwa kudra za mwenyezi Mungu. Sitaki kabisa kuajiriwa kwakuwa nishaajiriwa miaka miwili skuambulia chochote zaid ya kulipa kodi na kununua vitu vya ndani bas
Kwahiyo hauna biashara/mradi wowote pembeni mbali na ajira yako kwa mantiki hiyo.
Hizo mbao gani mkuu ulikuwa unachukulia wapi
Wow! Hapo kwenye ufugaji hapo unaweza ukaliaChangamoto ni nyingi hata sijui nianzie ipi ila kubwa kuliko zote nilipoingia kwenye ufugaji ugonjwa ukaingia bandani kila siku naokota kuku 15-30 wamekufa na kati ya kuku 700 niliuza 150 sitasahau
Kutofanya research ya biashara kabla ya kuanzisha kulinicost sana kwenye biashara ya mgahawa unapika chakula hakuna wateja kila siku unalaza aisee
NGOJA WAJE KUKUPA MWONGOZO MKUU.mwanangu ww kama mm yaan huwa znaniboha knyama mpaka nauliza huyu jamaa kama hana cha kucomment si apite kimya ???yaan kila post yy anaandika "ngoja waje" huwa ananikata maini kinyama mpakq huwa naclose app dadeq yaan nakerekaga asee yaan naboreka ase e kama huna cha kucomment uwe unapita kimya kimya mzee for sure watu huwa tunaboreka
Sasa hivi je umeshajua kiasi cha wateja,na size ya chakula cha kupika?Changamoto ni nyingi hata sijui nianzie ipi ila kubwa kuliko zote nilipoingia kwenye ufugaji ugonjwa ukaingia bandani kila siku naokota kuku 15-30 wamekufa na kati ya kuku 700 niliuza 150 sitasahau
Kutofanya research ya biashara kabla ya kuanzisha kulinicost sana kwenye biashara ya mgahawa unapika chakula hakuna wateja kila siku unalaza aisee
Keep upMkuu Mimi nina wiki ya pili tangu nimefungua duka kuna siku sijauza siku mbili hata ile mia mbovu
lakini napata mawazo ya watu eti location niliyoipata si rafiki duh mawazo juu ya mawazo
nimeanza na mtaji kiasi ila najitahidi Kila nikipata hela naongeza mzigo dukani labda siku moja nitasimama
Naweza Kupata Kijisehemu Mkuu Na Mimi Niweke Bidhaa Zangu !Mnamo tar21 mwez wa tisa mwaka huu nlifungua wakala (mpesa, tigo, airtel, na halotel) kariakoo nakumbuka cku hyo ckufanya muamala hata mmoja. Nliwaza nkamwambia Mungu n nini hiki sasa. Daah wateja wakawa kidogo wanakuja mwanzo wa mwez wa kumi ka kamishen kakaja hakafiki hata elfu hamsini daah kweli nkavunjika moyo sana.
Leo namshukuru Mungu kidogo wateja wanakuja japo nnaamini hadi mwakani nitasmama kwa kudra za mwenyezi Mungu. Sitaki kabisa kuajiriwa kwakuwa nishaajiriwa miaka miwili skuambulia chochote zaid ya kulipa kodi na kununua vitu vya ndani bas
Ndugu wewe ndiyo umeeleza hali halisi ya biashara hapa Tanzania. Biashara ni za kubahatisha sana. Unamkuta mtu hajui imekuaje akawa anafanya biashara flani,upepo ndiyo umemfikisha hapo. Mpaka najiuliza inawezekana kweli kuna na watu kama akina Ford,Alibaba etc katika hii nchi. Siasa nazo siyo Rafiki,kila awamu na wafanyabiashara wake,kweli tuna safari ndefu.Biashara ni ngumu kwavile imeambatana na changamoto ambazo wakati mwingine ni vigumu kuziepuka.
Mfano:
1. Uzoefu
2. Uaminifu
3. Uvumilivu
4. Usimamizi n.k
Kwanza nilianza na ufugaji wa nguruwe mmoja jike. Nikaenda nae vizuri tu. Kushika mimba, kabla hajajifungua akaanza kuumwa. Akawa anakosa nguvu za miguu, kuna jamaa mfugaji mzoefu, nilipomuelezea akasema kuna sindano inabidi achomwe. Tulipomchoma ile sindano, baada ya siku mbili mimba ikatoka. Nguruwe akaja akapona. Akashika mimba nyingine na kujifungua vitoto 5,mmoja akafa. Tukaenda nao pia fresh, ila wanakula kupita maelezo. Vilipoacha kunyonya, tukauza 3 kimoja kikabaki. Baada ya kuona uelekeo sio, mama mtu nikachinja na kuuza nyama buchani. Hela haikurudi. Nikapiga chini huo mradi.
Nikasogea kwenye kilimo. Tikiti na maharage. Hudumia sana shamba. Kwenye kuvuna, tikiti ilinipiga hasara moja matata sana. Nikapiga chini. Nikahamia kwenye kusafirisha maharage toka mkoani kuleta Dar. Nilichora mchoro vizuri tu. Nikanunua mzigo wa kutosha na kuuagiza uje mjini. Huku town alikuwepo jamaa yangu mmoja, mtu wa karibu sana (alikuwa mtu wa karibu sana, maana sio wa karibu tena). Jamaa akaupokea mzigo na kuusimamia kwa wale madalali wauzaji. Daily ananipa mrejesho wa maendeleo, nikawa nafurahishwa na bidii yake. Kumbe daily anaenda kuchukua hela alaf anaweka heshima mitaani na bar (mimi sina habari). Kuja kustuka, kashakula hela 75%, huku mimi ananiongopea madalali hawajampa bado. Biashara ikafa.
Nikageukia kwenye tangawizi. Nikalima vizuri na kila kitu kikawa chini ya usimamizi wangu mwenyewe. Kwenye mavuno mambo hayakwenda vizuri, ila walau niliona mwanga fulani hivi. Ikabidi niwekeze tena kwenye ili zao. Msimu wa pili kilichotokea ni afadhali ya msimu wa kwanza. Kama sijapalaraizi shambani, basi sidhani kama ntakuja kupalaraizi maishani mwangu. Kifupi shambani kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua, zaidi ya hapo niliwafaidisha wao tu mimi sikupata kingine. Nikasema kilimo kwangu bye bye, siingii shambani tena.
Nikaamua kufungua duka la nafaka kwa reja reja. Ushindani niliokutana nao sio wa kawaida. Mara leo mtu aje kuulizia, then anakwambia ntarudi kuchukua kiasi kadhaa siku nyingine. Kumbe nae anafanya biashara hiyo hiyo so alikuja kunichunguza. Mara wamama watake mkopo. Kipindi mchele umekuwa hadimu mtaani, bei ya chini ilikuwaga 1500 kwa kilo, ila watu wanataka mchele wa 1300,tabu tupu. Baada ya miezi 4,nikaamua kupiga chini. Maana mzunguko ulikuwa mdogo saaana, nikawa namfaidisha mwenye fremu tu.
Kutokea hapo ndio nikaamua kuwekeza kwenye kitu kingine kabisa, tena nilianza na mtaji wa 1.5 milions. Nikaamua kusimamia mwenyewe mwanzo mwisho, hapo atleast ndio mwanga kidogo ukaonekana. Now nafikiria ni jinsi gani nitaitanua .
***** ****** ****** ******
Biashara zinahitaji kujitoa. Ukiweza kuweka hela yako sehemu, basi hakikisha unaweza kuweka na muda wako. Vinginevyo utaishia kufaidisha wengine.
Sasa hivi je umeshajua kiasi cha wateja,na size ya chakula cha kupika?
Wow! Hapo kwenye ufugaji hapo unaweza ukalia
Hiyo ninusu hasala kwasababu dar kuku walio kufa wanasoko lao pia
Mimi baada ya mkataba wangu kazini kuisha nlikaa wiki mbili nkitafakari biashara. Nlipata mawazo mengi sana ya biashara. Nliplan kufungua carwash tabata mawenzi pale highbury bar ile nmepanga kwenda kuonana na mmiliki nkaskia na wao wameanza kujenga as if waliniskia mawazo yng. Nkabadili na kuwaza nchukue viazi njombe na iringa nlete dar nkaenda sokoni mabibo nkapewa ABC za kaz nkauliza shamban nkaona mtaji wangu utapelea kidogo na ntatake risk maana hela inaweza isirud kutokana na hali ya mda ule viazi kibao sokoni. Nkaplan banda la chips nkaona sina kijana mwaminifu wa kufanya nae kazi ile. Mwisho nkaja na hitimisho nifungue wakala kariakoo nikiamini wakala hela nloinvest kupungua ni ngumu sana labda mimi nitumie au nitapeliwe jambo ambalo nipo nalo makini sana wakati huo nkiangalia fursa nyingine nyingine. Sasa nna plan biashara hii ikizaa matunda nidiversify kwenye nyingine nyingi kama phone and accessories shop, car wash na migahawa. Naamini kwa kudra za mwenyezi Mungu lengo litatimiaKing999 umenichekesha sana tena sana.Binafsi kwa sasa baada ya kuteleza mara kadhaa katika biashara ikabidi nitulie na niwaze kwa kina nikaibuka na hitimisho biashara/kilimo ni taaluma kama taaluma zingine za ualimu/udaktari/uanasheria n.k, hivyo ili uifanye kwa uhakika na ufanikiwe kwa unachokifanya huna budi kuisomea hiyo taaluma hata kwa mfumo usiorasmi kwa kufanya utafiti ili ukusanye taarifa za kina zenye mbivu na mbichi kabla ya kuanza.
ushaanzaNGOJA WAJE KUKUPA MWONGOZO MKUU.
Daah we jamaa mwepesi sana kupiga chini vitu
Ndugu wewe ndiyo umeeleza hali halisi ya biashara hapa Tanzania. Biashara ni za kubahatisha sana. Unamkuta mtu hajui imekuaje akawa anafanya biashara flani,upepo ndiyo umemfikisha hapo. Mpaka najiuliza inawezekana kweli kuna na watu kama akina Ford,Alibaba etc katika hii nchi. Siasa nazo siyo Rafiki,kila awamu na wafanyabiashara wake,kweli tuna safari ndefu.