Tamu na chungu ulizopitia wakati unaanza biashara yako

ANKO JEI

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,278
2,364
Habari wadau, naimani kila mmoja yuko poa na kama mambo hayajakaa sawa basi hayo ni mapito tu, yatapita.

Katika maisha ya sasa ujasiriamali ni jambo mtambuka, linahubiriwa kila kona mpaka kwenye nyumba za ibada, vijana kwa wazee wanaanzisha vibiashara iwe ni kuuza chakula mpaka vijuice point kama vya Sinza na Kinondoni.

Tofauti na watu wengi tunavyofikiri kabla ya kuanza ujasiriamali, kiukweli kuanzisha biashara ni ngumu na kuna changamoto nyingi, mpaka muda mwingine unatamani usingeanza hiyo biashara kutokana na magumu unayopambana nayo mpaka biashara isimame vizuri. Katika kutambua hilo ningependa kila mmoja aweze kutoa tamu na chungu alizokutana nazo wakati anaanza biashara ili na wengine wasione kama ni wao tu wanaopitia changamoto.

Nianze na mimi binafsi, baada ya kumaliza chuo nilikuwa nishakomaa kwenye maswala ya Youtube nikawa napata kiasi fulani cha pesa kinachotosha kusongesha life la kibachela. Baada ya kusave sana nikaamua kufungua studio ya picha mkoani, hapo ndipo shughuli ilipoanza kwanza nilifungua sehemu ambayo karibu kuna studio. Kiukweli ile kufungua asubuhi mpaka jioni hakuna anayekuja hata kuulizia picha ya passport size ilikuwa inanipa shida sana.

Yaani unaona wateja wanavyomiminika karibu na kwako lakin wewe hakuna kitu, hadi unatamani ofisi yako ndio ingekuwa ya jirani yako. Muda mwingine unasahau wewe ndio unaanza unataka kushindana na aliyeanza miaka miwili iliyopita. Yote hii ni kitete tu cha biashara ndogo, bado sijasimama vizuri japo naanza kupata angalau wateja wa kuokoteza lakini msoto ni wa hali ya juu.

Itapendeza endapo na wengine watashare changamoto wanazopata.
 
Changa'moto niliokutana nayo katika biashara zangu ni 'human resource' kupata mtu mwaminifu self driven and determined katika kazi zangu, limenichelewasha kua millionaire....watanzania wengi wakiwemo na ndugu sio waminifu hawapendi kazi boss wao anachukuliwa kama adui wao
 
Nafanya/napenda kufanya biashara ya kununua na kuuza..chungu ni pale unaponunua mzigo mwingi then inatokea kwenye market bidhaa zimeshuka so wapinzani wako wanapata kwa bei chee , hakika utaiona chungu ya biashara

Tamu ni pale unakuwa na stock nyingi then product inakuwa in demand kwenye soko, ahha utaona tamu ya biashara au competitors wako wapate the same product kwa bei ya juu
 
Ambao hawajaanza hawawezi elewa kitu hapa.... Anyway, mimi ndo kwanza nina siku ya tatu toka nianze biashara. Mambo si rahisi kama nilivyokua nafikiri.

Sikati tamaa, nakua mvumilivu maana naamini mafanikio yangekua rahisi kila mtu angekua amefanikiwa. Kila jambo linahitaji muda.

Wakati una wazo zuri la biashara, unaanza hadi ku-calculate faida ilhali hujaanza hata 😂😂
 
Changamoto ni nyingi hata sijui nianzie ipi ila kubwa kuliko zote nilipoingia kwenye ufugaji ugonjwa ukaingia bandani kila siku naokota kuku 15-30 wamekufa na kati ya kuku 700 niliuza 150 sitasahau

Kutofanya research ya biashara kabla ya kuanzisha kulinicost sana kwenye biashara ya mgahawa unapika chakula hakuna wateja kila siku unalaza aisee
 
Wakati niko chuo nilipata boom kiasi cha lakhi 4. Nikaamua nikizalishe. Nikaanza biashara ya mbao. Kwa vile sikuwa na muda wa kusimamia, ilibidi tu niwaamini marafiki. Weee... kosa kubwa. Biashara ilifilisika. Nikajifunza kuwa usimamizi wa biashara ni muhimu tu kama ilivyo mtaji. Kuanzia hapo kama sina muda wa kusimamia, sifanyi biashara.
Yaah kiongozi karibu na wewe share unacho fahamu
 
Wakati niko chuo nilipata boom kiasi cha lakhi 4. Nikaamua nikizalishe. Nikaanza biashara ya mbao. Kwa vile sikuwa na muda wa kusimamia, ilibidi tu niwaamini marafiki. Weee... kosa kubwa. Biashara ilifirisika. Nikajifunza kuwa usimamizi wa biashara ni muhimu tu kama ilivyo mtaji. Kuanzia hapo kama sina muda wa kusimamia, sifanyi biashara.

Usimamizi wa biashara unaenda pamoja na utunzaji wa kumbukumbuku kwa njia ya maandishi..ata awe ndugu gani anatakiwa kuweka record ya kile kilochotoka na kuingia
 
Biashara ya mkaa kutoa pori kupeleka mwanza,changamoto niliyokutana nayo ni jamaa tunayeshirikiana nae kupeleka mzigo yaani anaweza kupeleka mzigo hata mara tatu kwa mwezi ila mimi ananificha kwa kuwa niko bize na kazi nyingine.ila sasa hivi nasubiri akinimalizia mzigo wangu namtema naanza ku fight kivyangu.
 
Nilifungua duka la reja reja kwa mtaji wa million moja na nusu, nikwamweka wife anisaidie kuuza sababu yuko home free, kumbe mwenzangu hapendi biashara, baada ya miezi mitatu vitu vimeisha dukani nimemkuta na balance ya laki mbili tu, namshukuru mungu nilifunga duka nikawekeza kwenye kufuga mbuzi naishi mjini mbuzi nafungia kijijini msimamizi ni mama yangu,namshukuru mungu nilianza na mbuzi wa nane saivi mimefikisha mbuzi arobaini na tatu. daima nitaendelea kumwamini mzazi kuliko Mke.
 
Back
Top Bottom