Tamko la UVCCM Arusha juu ya Husein Bashe na Lema

Tamko la UVCCM Arusha juu ya Husein Bashe na Lema

UVCCM-Arusha-mjini-kuhusu-Bashe-na-kukamatwa-kwa-Godbless-Lema-April-29-2013.png

UVCCM-Arusha-mjini-kuhusu-Bashe-na-kukamatwa-kwa-Godbless-Lema-April-29-2013-2.png

.
UVCCM-Arusha-mjini-kuhusu-Bashe-na-kukamatwa-kwa-Godbless-Lema-April-29-2013-3.png

mwe. yaan imefika mahali mtu haitaji kusoma uso ili kujua kua kinachosemwa ni unafiki.
 
Hivi Arusha bado Kuna vijana Wako CCM?hawa basi vichwa vyao vitakuwa vimebunguliwa.Wanaserukambwa mini?
 
God have mercy , kichaa kaingia mtaani jamani, fungeni milango anakuja (Lema)
 
Je naye mukuu wa mkoa alienda kuonana na viongozi wa chuo na kama alionana nao alimpa taarifa gani?
 
Bashe anaendelea kewatesa.!

Kwa anaeitakia mema ccm Bashe yupo sahihi.!!
 
CCM vipande-vipande sakata la Lema Arusha.

Yani tarehe 9/05/ 2013 kipenga kinapulizwa rasmi tunaanza kampeni wa hizi kata 4 hapa Arusha.
Hawa vijana wanaomlamba miguu Mkuu wa Mkoa watazifunga hizo account za FB baada ya CHADEMA kutwaa kata zote 4 kwa kishindo na haibiwi mtu hapa.
 
muda si mrefu wataanza kutukana na mipasho km wale madj wao pale mjengoni.
 
huyu afisa habari kahitimu chuo gani? hii taaruma ya habari kila kukicha inakuwa dhariri
 
umejieeza sana kwa kujichanganya, pima kwanza walengwa ukichukulia teyari wameshafikiwa na habari picha.

Mkuu huyu tunamuonea bure. Mlengwa hasa wa hilo "tamko" ni gamba mwenzie Hussen Bashe; hivyo kimantiki na kimaudhui ya kimagamba yuko sahihi kabisa - hizo ndio lugha zao na uandishi wao. Yaani wanaelewana ile mbaya. Aliyefanya makosa ni aliyeli-post humu because it wasn't meant for JF or the public. Hizo ndio aina ya internal "circulars" za magamba.

Yaani kama ingetokea ukutane na "makabrasha" ya vikao vya magamba au mafaili yaliyojazana kwenye maofisi yao utacheka ufe. Hamna kitu mle pamoja na mikwara miingi; ni upuuzi umejaa tu mle. Bwaha ha ha ha!
 
hii ndo aina ya vijana wanaounda UVCCM arusha!? ama kweli nchi imepotea, na kama wewe ndo afisa habari basi rudi shule ukasome japo siasa kidogo na namna ya kujenga hoja kwenye ishu nyeti kama hii, shame on you na ccm yenu na mkuu wenu wa mkoa asiyejua majukumu yake.
 
Someni hili tamko vizuri, hamna vituo na matumizi sahihi ya lugha na herufi stahiki mahali stahiki. Hii ni taarifa ya Afisa Habari wa Wilaya.




KWA NDUGU YETU HUSSEN BASHE NA WAPOTOSHAJI WENGINE HASWA WA CHADEMA KUHUSU KUKAMATWA KWA LEMA MBUNGE WA ARUSHA MJINI

Tangu yalipo tokea mauaji ya kijana mwana chuo wa uhasibu
kitendo kilicho pelekea LEMA kukamatwa kwa uchochezi yamesemwa
mengi sana kuhusu hili suala na lawama kupewa MH MKUU WETU WA
MKOA WA ARUSHA MAGESA MULONGO hatuna malengo ya kumtetea
mkuu wetu wa mkoa bali kuweka ukweli wazi hapa na kuondoa upotoshaji
ambao unafanywa kwa makusudi na baadhi ya wanzetu

Suala la kukamatwa kwa Lema mbunge wa Arusha ni kama wanavyo
kamatwa wahalifu wengine Lema alifika uhasibu badala ya kupitia
kwa viongozi yeye akaenda moja kwa moja kwa wanachuo na
kuanza kuwahutubia kitendo ambacho ni utomvu mkubwa wa nidhamu
mbunge alipaswa aende ofisini na kuonana na uongozi wa chuo
ili apewe taarifa na uongozi wa chuo wampeleke kuongea na
wanachuo lakini Lema hakufanya hivyo badala yake alikwenda
bila utaratibu na adabu

Baada ya Lema kufika na kumaliza kuongea aliyo yaona kuwa
ametosheka RC MULONGO alifika na kwasababu uhasibu wanafunzi
ni wengi na sauti tunatofautiana aliomba vipasa sauti ili aweze kuongea
na kusikika vizuri hapo kuna dhambi gani mtu kuomba vipasa sauti
na vilikuwepo na akapewa ili aongee lakini kwa vile tayari Lema
alishaa mwaga sumu tayari wale baadhi ya wanachuo walifanya kama
LEMA alivyokuwa amewaelekeza kuwa wafanye fujo

Ndugu HUSSEN BASHE kuhusisha kukamatwa kwa LEMA na suala
la uchaguzi wa kata nne za ARUSHA mjini hizi ni propaganda ambazo
chadema wanazieneza nashangaa na wewe kuwasaidia chadema
kufanya propaganda chafu MKUU WA MKOA YEYE NDIYE KIONGOZI WA
ULINZI NA USALAMA WA MKOA WETU amekosea wapi kumkamata
mwalifu au kukiwepo uchaguzi basi serikali isiwadhibiti wahalifu
Bashe post yako uliyo post jana umesukumwa na chuki na wala
siyo mapenzi mema

NDUGU HUSENI BASHE nawanachadema ambao mmekuwa mki
mlaumu mh mkuu wetu wa mkoa kuwa ametumia ubabe sisi
kama CHAMA TAWALA TUNARIDHISHWA SANA NA UCHAPAKAZI
WA MKUU WETU WA MKOA MAGESA MULONGO
kuhusu suala la wauaji kutafutwa lazima watafutwe lakini pia
wachochezi na wenyewe nilazima watafutwe pia maana wote ni
tatizo

USHINDI WA KATA ZETU NNE UPO NJE NJE BASHE ARUSHA
UNAYO ISEMA WEWE KUWA CCM INASHINDWA UMEISOMA
MTANDAONI ILA KWA SISI TUNAOISHI ARUSHA WANANCHI
WANASEMA WAMETUELEWA

nahawako tayari kurudia makosa tena kwa yaliyo tokea wamejifunza
Arusha ni mji wakitalii hauhitaji wahuni mwanzo tuliwambia wananchi hawakutuelewa ila kwasasa baada ya kuionja sumu ya CHADEMA
wameelewa

MKUU WETU WA MKOA VIJANA WA ARUSHA TUKO NA WEWE KATIKA
KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKO KW AMUJIBU WA SHERIA BILA KUMWONEA
YEYOTE KAMA UNAVYO FANYA ONGERA MAGESA S.MULONGO KWA
KUTEKELEZA VYEMA ILANI YETU YA UCHAGUZI

Afisa habari wa UVCCM wilaya ya Arusha mjini ndugu

SAIDI A. SAIDI
 
Huu waraka ni kipimo tosha sana cha uwezo mdogo wa akili wa vijana wa CCM. Taifa linategemea vijana kuwa chachu ya mabadiliko na maendeleo. Ukiwa kijana usipende sana kuendekeza kuganga njaa kwa kuwasifia watawala. Hao hawasaidii kitu zaidi ya kuangamiza taifa letu. Maelezo yako yamekosa kabisa thinking capacity. Unasema mkuu wa mkoa alizomewa kwa kuwa Lema alishamwaga sumu!!! Kumbe basi kilichomzuia mkuu wa mkoa naye kumwaga sumu zake ni nini? Jibu ni rahisi tu. Naye ni kama nyinyi vijana wa CCM: hana uwezo wa kufikiri. Jikomboeni kifikra ili tulikomboe taifa kwa manufaa hata ya wajukuu zenu mbeleni.
 
Hawa watu ni waongo dunia nzima kama baba zao CCM, wakati anawahutubia wanafunzi mbona alikuwa na uongozi wa chuo "uliokuwepo" wakati huo? Ndiyo, mkuu wa chuo hakuwepo lakini wasaidizi wake walikuwepo!!!! Uongo huu jamani............!
 
Hata wakimpaka ubani wa maiti ananuka tu!hafai!chaguo la Mangungo tu huyo hana jipya!baada 2015 atashangaa jina lake halitajwi popote!ataishia hivyo hivyo tu!ataweza kupambana na mwamba uliomuweka aliemteua yeye na anaemuabudu!?
 
Njie vijana mkuu wa mkoa na yeye alipitia kwa uongozi wa chuo? Wacheni kumnyima mbunge haki yake kuongoza kwa kua anatoka upinzani. Hii dhambi ya hila za kila namna itaitafuna ccm hadi mwisho baada ya kuwageuka wakulima na wafanyakazi toka chama cha ujamaa na kujitegemea na kua chama cha kutetea unyonyaji na mabwanyenye.
 
haya ni majibu dhaifu na ni majibu ya woga huyo mkuu wenu hachapi kazi ndo maana alizomewa. acheni kutapatapa ninyi nyinyiem
 
Back
Top Bottom