Bw. Said
Inaonekana kweli umekurupushwa kutoa hili tamko na huenda ikawa pia katika kulitoa ulikuwa na haraka za kuwahi shughuli zako nyingine muhimu kulikotangazo ambalo umeliweka bila hata wewe kuelewa mazingira ya tukio lenyewe maana maelezo yako yamejaa nadharia tupu.
Ndiyo Mkuu wa Mkoa wako kama kada wa CCM ni muhimu sana kwako kwa kuwa ukisema alikosea utakosa kula kwa hiyo kwako ni sahihi kuendelea kumtetea hadi hata kama watu watazidi kuuwawa hadi mbakai wewe na yeye na hatimaye na nyie mmoja amuuwe mwenzake.
Nilidhani andiko lako lingekuwa la msingi zaidi kama ungeeleza Mhe. Lema alifikaje AA nani alimjulisha kuhusu yaliyokuwa yanaendelea pale chuoni? Pili uongozi wa chuo ambao wewe ulitaka wakasalimiwe kwanza ulfanya jitihada gani kabla na baada ya Lema kufika? unajua kwa nini walikaa kimya kuacha wanafunzi wafanye maadamano? unaelewa kuwa walikuwa wanaunga mkono maandamano hayo?
Jiulize nani aliye mjulisha Mkuu wa Mkoa kuhusu yaliyokuwa yanajiri Arusha, ni kweli kuwa Serikali muda wote ilikuwa haina taarifa kuwa kuna mauaji yaliyotokea hadi Lema ampigie Mkuu wa Mkoa? nani aliyesadia maandamano yasiwepo?
Tukiendelea zaidi baada ya tukio hilo sasa ni karibu wiki mbili Je Mkuu wako Mtukufu wa Mkoa kama Mlinzi wa Usalama alifanya nini kuhusu mauaji ya wanachuo? kuna wauaji wangapi waliweza kutiwa nguvuni? aua hawajuliakani? je kabla ya kutoa tamka lako unataarifa za kutosha juu ya kilichopelekea mwanafunzi kuuwawa? Uliongea na Mulongo kabla ya kutoa tamko lako naye akaridhika kuwa uliyoandika ni sawa?
Nini tafsiri ya mwalifu, unataka umma uamini kuwa Lema kama Mbunge ambaye alifika eneo hilo na kuzuia maandamno ni adui zaidi kuliko wauaji? maana umeeleza yote yanauzito sawa, umetafakari hilo?
Lema alifika baada ya kujulishwa hali ilivyokuwa pale chuoni kufuatia kifo cha mwenzao, ni kwa nini polisi walitumia nguvu nyingi kumkamata mtu ambaye yupo siku zote anajulikana pa kumpata kuliko kutafuta wauaji wenyewe? Wapo wauaji wangapi ambao wewe na Mulongo (wazalendo) mumeweza kuwakamata au kusaidia kukamatwa kufuatia tukio hilo.
Kumbuka Tanzania inakoelekea sasa juu ya mauaji ya raia wasiokuwa na hatia hayatamuacha hata yule anayeshabikia, leo kwa mwingine, sijui utatoa kauli gani siku unapata taarifa kuwa mdogo wako ambaye yuko shule fulani amekutwa amekufa. Tafakari chukua hatua. Acha kukurupuka.