TAMKO la UVCCM Arusha 25/5/2011 SOMA UJIONEE!

Hao vijana si wanaCCM bali ni wafuasi wa CDM, P'se CDM msiivuruge CCM yetu, mungu ibariki CCM mungu mbariki Chatanda, japo aliwatukana watumishi wa mungu

ccm ilishakufa siku nyingi muda uliobaki tunapanga kwenda kuizika baharini,koma kabisa kuihusisha Chadema na ccm
 
CCM wamefikiria mbali sana, mtu kama chitanda wakisema wamuamishe Arusha inamaana wanabariki kupoteza jimbo huko anakoamia so wanaona bora abaki Arusha ambako tayari wamepoteza
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Sina uhakika kama tatizo ni Mh. Lowasa au mfumo wa CCM. Ndani ya CCM sasa hivi inaonekana kila mmoja ni kambale. Hivi ni lazima waanze kuumbua hadharani. Utamaduni huu unajegeka nna kuota mizizi. Mwenyekiti uko wapi?
Huyu Chatanda wao anaweza kuwa tatizo zaidi kuliko inavyofikiriwa. Lugha yake ni chafu. Nadhani na yeye ni mchafu pia. Yey husems pale ambapo anatakiwa akae kimya na kukaa kimya pale anapotakiwa kusema. Huyu ni mtaji mkubwa kwa wapinzani.
 
Waislam wajitoe kwenye vurugu ili iwe nini, ionekane wakristu ndio mabingwa wa vurugu! maimamu bwana ndio upeo wake juu ya vurugu za uvccm arusha ulipoishia
 
huu ndio udini wenyewe, shehe katumwa na chatanda?? waislamu wajitoe hata kama wanaona maasi yanafanyika?
 
Kwahiyo Imam Hambal anataka kutuaminisha kwamba mafisadi ya kikristo ndo yanayo watumia vijana safi wa kiislamu kuivuruga CCM A-town?
 
Uwezo mdogo wa Muislam huyu ndiyo maana hata kama wakisoma wanajiita Mlima Kilimanjaro wakati hakua kitu .Laana Tuulah
 
Mh. . . .haya mambo magumu sana! Kama vionGozi WA DINI wataanza kuonyesha waziwazi wako upande upi hii ni hatari sana......'nachoweza sema jamaa kachemka. . . . .!aluta continua. . . .
 
Hapa ndo shida sasa za imani,huyu yupo msikitini baadala ya kutoa Da'awa anaongea ujinga na kuufanya uislam uonekane kama imani ya majuha!
 
Nachukia sana matamshi ama bandiko lolote linalolenga jamii/lililokusudiwa kuifikia jamii lenye kuegemea upande wowote wa dini....na walaaniwe wote wenye maono mafupi wanaotumia influence zao vibaya kuchonganisha jamii...hua najiuliza ni nini Muisilamu atafanya bila Mkristu kadhalika Mkristu bila Muisilamu? na ni vipi mpagani atajidai ana amani ilihali ndugu zake wanaoteshwa chuki?...sina hakika ni bahati mbaya ama ni makusudi kupima mioyo ya watu lakini nitumie fursa hii kuombea wana wema wa nchi hii utulivu na udugu ili amani idumu daima!
 
Imamu azungumzia mgogoro wa UVCCM Arusha




Na John Ngunge



29th May 2011


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa



comment_bubble.png

Maoni




Imamu wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mkoa wa Arusha, ametoa tamko kuhusu mgogoro unaofukuta ndani ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), mkoani hapa na amewaasa vijana wa Kiislamu wanaojihusisha katika mgogoro huo kujitoa.
Aidha, amewaasa Watanzania kwa ujumla kutokubali kutumiwa na chama cho chote ili kuleta vurugu nchini.
Imamu huyo, Muhammad Said Hambal, alisema hayo kufuatia mgogoro uliopo ndani ya UVCCM ambao umedhihirisha kuwepo kwa makundi mawili yanayotumiwa na baadhi ya mafisadi.
Alisema kuna baadhi ya watu aliowaita kuwa ni mafisadi wanawatumia vijana kuleta vurugu kwa malengo wanayoyajua wao na akaonya kuwa hali hiyo ikielendelea inaweza kuleta machafuko makubwa katika jamii.
“Ndani ya CCM kuna vijana wanaonyesha mpasuko wa wazi…nawaasa vijana wote wa Kiislamu kuacha, wajitoe katika vurugu hizo mkoani hapa,” alisema.
Imamu Hambal alisema vijana hao wanafahamika na akaahidi kwenda kuwaona kila mmoja binafsi kuwaasa wajiondoe katika mgogoro huo.
Alisema hivi karibuni kumekuwa na madai yanayotolewa na baadhi ya vijana ndani ya umoja huo wakitishia kuchoma moto jengo la makao makuu ya CCM mkoa.
“Ofisi ya CCM ni mali umma, sasa ikichomwa moto wataleta madhara…sisi hatutaki madhara, na ndio maana tunakemea vurugu zozote,” alisema.
Alisema wamepata madhara makubwa katika maandamano yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), yaliyofanyika mapema Januari mwaka huu ambapo watu watatu waliuawa na polisi kwa risasi.
“Tumepata madhara makubwa katika maandamano yale ya Chadema, hilo ni funzo na tusingependa mambo haya yatokee tena, wengi walioathitika ni Waislamu,” alisema na kuongeza, “waathirika wa mabomu walikuwa wa hapa mjini kati ambao pia mali zao ziliharibiwa na nyingine kuibwa.”
Akizungumzia hatua ambazo watazichukua iwapo watakaidi, Imamu Hambal, alisema wataenda kuwaona wazazi wao na kama itashindikana wataacha.
Hata hivyo, alionyesha matumaini kuwa vijana hao hawatakaidi tamko lake pale aliposema, “kila muumini anatakiwa kuwatii viongozi wake na kama hawatatii sisi tutawaacha.”
Alisema CCM ni chama kikubwa na kama kuna kasoro basi wakae chini na kuzitafutia ufumbuzi badala ya kukaa kimya na kuwapa faida mafisadi kuwatumia vijana kwa lengo la kuleta vurugu.

source?
 
Back
Top Bottom