Tamko la serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam juu ya ripoti ya makinikia

Aliyofanya rais ni ya hovyo....Gharama tutakazolipa ni kubwa kuliko mchanga wa Acacia. We will become an economic busket case kama Zimbabwe.... Tumeharibu Mahusiano ya kiuchumi na tutashitakiwa..... "
Tundu Lissu May 30, 2017
 
Naona kila mtu au kikundi na hata viongozi wa dini nao wamejiunga kumpongeza mheshimiwa rais.

Ni jambo zuri kumpongeza mtu pale anapofanya vizuri.

mheshimiwa huyu huyu kuna wakati anakosea sana tena wakati mwingine hadharani kwa kauli zake, kwa mfano hapo juzi alipomwambia spika awashughulikie ndani ya bunge na wakija nje atadeal nao mwenyewe, hiyo sio kauli nzuri kabisa kwa utawala unaojiita wa kidemokrasia.

Demokrasia inaminywa
Vyombo vya habari vinabanwa
Uonevu kwa watumishi wa umma
Kuukumbatia uovu wa mtu anayetuhumiwa kufoji vyeti

Haya na mengineyo mabaya mbona sijawahi kuwasikia hao viongozi wa dini wakimshutumu au hao wanaojiita wasomi wakitoa matamko?

Acheni Unafiki.
 
Hao wanafunzi wa chuo wanyamaze, wao wenyewe wanaongoza kwa ufisadi na kula ela za wanafunzi karibia vyuo vyote wote wezi.
 
Unaoneka wewe chizi

You are certainly right.....kama professors wanadai makinikia kusafirishwa kuanzia mwaka 1998 na wakati uzalishaji wa dhahabu umeanza april 2001 katika mgodi wa bulyanhulu na mwaka 2009 katika mgodi wa buzwagi.

Wanafunzi wao wa chuo kikuu wanaibuka kupongeza bila hata kujiuliza mara mbili.....kuna elimu itaheshimika hapa???
 
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM SERIKALI YA WANAFUNZI CHUO KIKUU DAR ES SALAAM (DARUSO) TAMKO LA SERIKALI YA WANAFUNZI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM JUU YA RIPOTI YA TUME YA PILI YA KUCHUNGUZA KIWANGO CHA MADINI KWENYE MAKONTENA YA MCHANGA (MAKINIKIA) Ndugu wanahabari sisi WANA DARUSO tunapenda kuchukua fursa hii adhimu kwa mara ya pili ya kumpongeza Mh. Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi ngumu za kizalendo anazoendelea kuzifanya kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Kwanza, ndugu Wana habari sisi wana DARUSO tumefarijika sana kwa kazi ya Mh. Rais wetu alivyolishughulikia suala hili la Mchanga wa Madini (Makinikia). Tofauti na wale wanasiasa wanaobeza juhudi zake sisi wana DARUSO tunapenda kumuhakikishia Mh. Rais wetu kuwa tuko pamoja nae kifikra, kimikakati na kimaombi kuhakikisha kuwa fedha iliyopaswa kulipwa na ACACIA kwa Tanzania tangu 1998 hadi 2017 zinalipwa mara moja. Ndugu wana habari tunasema kwa masikitiko makubwa sana kuona nchi yetu inageuzwa kuwa “SHAMBA LA BIBI” kwani ripoti ya kamati iliyoongozwa na Professor Ossoro imebainisha kuwa “Pesa zilizopotea zingeweza hudumia bajeti ya miaka mitatu ama kujenga reli ya standard (gauge) kutoka Dsm mpaka Mwanza!” Kwa pesa ya kiwango hiki ndugu wana habari kwenye huduma za jamii kila mtoto mwanafunzi wakitanzania angepaswa kupata kitabu chake binafsi cha kusomea cha kila somo na asingekosa dawati la kukalia na wale wa vyuo vya elimu ya juu hawakupaswa kwa nyakati tafouti wagome kwanza ndio wapatiwe fedha za mikopo ya kujikimu. Pili, ndugu wana habari tunapenda kumpongeza Mh. Rais kwa muelekeo mzuri wa juhudi zake za Kizalendo zilizomfanya Mwenyekti Mtendaji wa Kampuni ya (Afica) Barrick Gold Mining Professor John Thornton kuja Tanzania kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huu kama alivyonukuliwa kusema: “I have assured the president we are very interested in…..reaching resolution which is a win-win situation. A win for Tanzania, a win for Barrick and our subsidiary company
ACACIA.” (John Thornton, 14.06.2017, STATE HOUSE DAR ES SALAAM). Hivyo basi ndugu wanahabari kutokana na maelezo ya hapo juu tunawaomba watanzania wa makundi yote tuungane ili tukumuunge mkono Mh. Rais na tuache kubeza juhudi zake za kizalendo na zakihistoria katika kupigania uhuru na ukombozi wa kiuchumi wa Taifa letu. Tatu, ndugu wanahabari pamoja na hayo yote yaliyoainishwa hapo juu tunapenda kushauri: Mh. Rais asiwateue kwenye timu ya majadiliano wale wanasiasa wote wanaobeza na kupinga juhudi zake katika suala la madini ili kuleta ufanisi wa matokeo chanya ya majadiliano hayo yenye maslahi makubwa kwa Taifa letu. Nne, ndugu wana habari tunatanabahisha kuwa wanasiasa hawa ni wakuogopwa kama “UKOMA” kwa usaliti huu wa “KI-SAVIMBI” na ni watu hatari kwa UHAI na USALAMA wa Taifa letu kwa kuwatetea MABEBERU na kuweka pembeni na kutelekeza maslahi ya Taifa letu. Kitu kibaya zaidi hawa wanasiasa ni wanasheria na wachumi waliosoma UDSM. Je hayo ndio malipo yao kwa watanzania? Sisi wana DARUSO tunasema wameitia aibu taasisi yetu na hawakustahili kusoma kwa kodi za watanzania na kupata Digrii ya chuo chetu. Kwa usaliti wa kiwango hiki wanasiasa hawa hawatofauitishwi na YUDA ESCARIOT aliyemsaliti YESU KRISTO na kama wangekuwa kwenye timu ya waliopigania na kuutafuta Uhuru wa Tanzania kwenye miaka ya 1960 chini ya Mwl JK Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa (Simba wa Vita) wasingejali kuwasaliti waasisi wa Taifa kwenye harakati za kuikomboa nchi yetu kwenye Makucha ya WAKOLONI. Pia wanasiasa hawa wangekuwa sambamba na Mzee wetu Abeid Amani Abeid Karume kule Zanzibar basi Mapinduzi matukufu 1964 yasingepatikana kwa usaliti wa kiwango hiki cha kujali sana kuweka mbele maslahi binafsi. Mwisho, Wana DARUSO tunapenda kukumbusha kuwa vita hii sio ya chama chochote cha siasa bali ni vita ya watanzania wote kwa hivyo tusimame na kuungana na Mh. Rais wetu Dkt. JPM kwenye mapambano haya. Asanteni sana kwa kunisikiliza, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki DARUSO na Mungu M-bariki Rais wetu Mpendwa Dkt. JPM Imetolewa na DARUSO na kusomwa na Rais wa DARUSO Engineer John Jeremiah Jilili (+255 687 548 035) tarehe 16.06.2017
Aibu kwa CHADEMA
 
Back
Top Bottom