Tamko La Jeshi Jana TBC1

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Jana wakati jeshi la Tanzania linatoa hoja tofauti pamoja na kujibu maswali ya waandishi wa habari kutokana na milipuko ya mabomu yaliyotokea kule G/Mboto na kuadhiri maisha ya Watanzania, nilimsikia mkaguzi mkuu wa JWTZ Brigedia-Jenerali Leonard Mndeme alitoa sababu tofauti ambazo zinaweza kuchangia kulipuka kwa mabomo yale, lakini pia hakujaribu kugusia pia kama kunaweza kukawa na uwezekano wa hali ya maisha duni kwa wanajeshi wa Tanzania ambayo sio kitu cha kuficha hata sisi wananchi tunaona hali ya polisi pamoja na wanajeshi ilivyo, je haipelekei kwa jeshi hilo kwanjia fulani wakajitokeza wanajeshi ambao kwa lugha ya kijeshi mnasema kutokua na nidhamu wakahusika kwa njia moja au nyingine kulihujumu jeshi hilo kwa kutokukidhi maslahi ya wanajeshi au kikundi fulani jeshini hapo? Nawasilisha hoja.
 
je hoja yako ni nini? unamaansha kuwa hayo mabomu yalilipuliwa na baadhi ya wanajeshi walioasi?
maybe??
 
yote yanawezekana lakini nani wa kuchunguza , hata kama kuna hujuma Amiri Jeshi Mkuu Ndiye kamteua Mkuu wa Majeshi TZ unategemea uchunguzi gani kwenye jeshi, ingekuwa ni mambo ya kisiasa sana lakini huku paala nyeti, ndio maana hata mtu wa kawaida hawezi kufika, unaweza kufika Kijitonyama UWT lakini Jeshi ni noma huwa hamwamini mtu
 
yote yanawezekana lakini nani wa kuchunguza , hata kama kuna hujuma Amiri Jeshi Mkuu Ndiye kamteua Mkuu wa Majeshi TZ unategemea uchunguzi gani kwenye jeshi, ingekuwa ni mambo ya kisiasa sana lakini huku paala nyeti, ndio maana hata mtu wa kawaida hawezi kufika, unaweza kufika Kijitonyama UWT lakini Jeshi ni noma huwa hamwamini mtu

Kamanda asante kwa upeo ulionao natumaini habari ndio hiyo kwa hawa wanaGreat Thinkers kwa maswali walio uliza!
 
je hoja yako ni nini? unamaansha kuwa hayo mabomu yalilipuliwa na baadhi ya wanajeshi walioasi?
maybe??

Hoja yangu nikua vyote ambavyo tumeambiwa na wakuu hawa wa jeshi vinaweza kutokea, lakini hili langu pia lisiwe la kupuuzwa tufanye utafiti!
 
Jana wakati jeshi la Tanzania linatoa hoja tofauti pamoja na kujibu maswali ya waandishi wa habari kutokana na milipuko ya mabomu yaliyotokea kule G/Mboto na kuadhiri maisha ya Watanzania, nilimsikia mkaguzi mkuu wa JWTZ Brigedia-Jenerali Leonard Mndeme alitoa sababu tofauti ambazo zinaweza kuchangia kulipuka kwa mabomo yale, lakini pia hakujaribu kugusia pia kama kunaweza kukawa na uwezekano wa hali ya maisha duni kwa wanajeshi wa Tanzania ambayo sio kitu cha kuficha hata sisi wananchi tunaona hali ya polisi pamoja na wanajeshi ilivyo, je haipelekei kwa jeshi hilo kwanjia fulani wakajitokeza wanajeshi ambao kwa lugha ya kijeshi mnasema kutokua na nidhamu wakahusika kwa njia moja au nyingine kulihujumu jeshi hilo kwa kutokukidhi maslahi ya wanajeshi au kikundi fulani jeshini hapo? Nawasilisha hoja.

Mkuu kwa uelewa mdogo tu hii sababu si ya kuipuuzia, inabidi na yenyewe ichunguzwe pia.... inawezekana vipi wanaoishi hapo kambini asidhurike hata mmoja????:A S 13:
 
Back
Top Bottom