Akiongea na waandishi wa habari leo John Mnyika amemshauri rais asianze kuitumia hiyo sheria hadi sheria hiyo ibadilishwe.
Kama hilo ndilo tamko kali tulilolisubilia, basi CDM imeshindwa katika medani za siasa za nchi hii. CCM imeshinda vita bila hata kutupa risasi moja.
Akiongea na waandishi wa habari leo John Mnyika amemshauri rais asianze kuitumia hiyo sheria hadi sheria hiyo ibadilishwe.
Mkuu Ben shauriana na viongozi wa CDM watafakari kwa umakini kinachotokea,haya matamko si makubaliano waliyosaini! Mpaka sasa sijielewi kabisa! tumeanguka vibaya ingawa vyombo vingi vya habari vimetusaidia kutosemea sana aina ya makubaliano tuliyosaini! Tumelikoroga sasa tulinywe.nakuhakikishia kuchomoka hapa hadi kueleweka inahitajika siasa ya kipekee sana.mpaka leo na hilo tamko la CDM ndio wanazidi kuchanganya watu.mimi mwenyewe nimemsia mheshimiwa Mbowe akihojiwa na BBC mara baada ya kikao hakusema wamekubaliana asisaini ule muswada! Naona kama mnasita kusema ukweli mkuu tumedharirika vibaya mno na vile viji paragraph viwili vya kihuni! Mkuu ile aibu ya mwaka!Hivi kama asingesaini na badala yake akasubiri kufanya marekebisho ni maslahi gani ya Taifa ambayo yangehatarishwa? Tuna imani gani na Rais(mwenye rekodi ya kutoaminika hata ndani ya chama chake wakiwamo washirika wake wa karibu) juu ya kutounda tume au kufanya ghiliba baada ya kusaini sheria hii?
Unaweza kufafanua zaidi kauli yako? Kwani wewe ulitaka watoe tamko lipi? Nakushauri usome vizuri nini kiliwapeleka CDM ikulu.
Hivi kama asingesaini na badala yake akasubiri kufanya marekebisho ni maslahi gani ya Taifa ambayo yangehatarishwa? Tuna imani gani na Rais(mwenye rekodi ya kutoaminika hata ndani ya chama chake wakiwamo washirika wake wa karibu) juu ya kutounda tume au kufanya ghiliba baada ya kusaini sheria hii?
hoja za chadema hazikuwa za kuzuia sheria hoja ilikuwa kupata maoni baada ya sheria kwa sababu hiyo maoni yao yatajumuishwa wakati wa mchakato wa kutoa maoni