Tamba na Jicho 👁 la Ustawi wa Jamii Mtaa kwa Mtaa 🇹🇿

Tamba na Jicho 👁 la Ustawi wa Jamii Mtaa kwa Mtaa 🇹🇿

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
1,706
Reaction score
8,657
Wasalaam

Leo 24 Julai, 2025 asubuhi, nakiri kupokea taarifa kadhaa kutoka kwa Wananchi wa Kata ya Baraa, Mtaa wa Kibao cha Njano kwa Mrefu, Arusha.

Kwamba, mtu mmoja mzima analea binti wa umri kati ya miaka 8 hadi 10 hivi ambapo yaani ni anampa vipigo tu apendavyo yeye hivyo, mtoto amejaa makovu ya vipigo kila sehemu, ananyimwa chakula, anafungiwa mlango alale nje na mateso mengine aina hiyo hadi shuleni, maendeleo yanasua sua.

KILICHOFUATA: niliwasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha ambapo, maafisa ustawi wa jamii mara moja walielekea eneo la tukio na kumfikia mtoto. Hii ni kuonesha kuwa, ustawi wa jamii wako speed... wewe tu toa ushirikiano.

Watuhumiwa wataijibu sheria ya mtoto na vifungu vyake.

UJUMBE GANI KWA JAMII: tuache kutesa watoto, jicho la ustawi wa jamii linatamba alipo mwanajamii yeyote kwa ushirikiano na wananchi wenye mapenzi mema.

Hima, tuendelee kutamba na jicho la ustawi wa jamii 👁🇹 kuwadaka watu katili wa watoto popote/kokote 🇹🇿✍️

Pia, kumbuka kupiga 116 kituo cha taarifa za watoto. Vilevile, kuna namba za maafisa binafsi na za vituo vya huduma kwa wananchi hapa chini👇zikumbuke, mpe na mwingine.....
 

Attachments

  • IMG-20250724-WA0058.jpg
    IMG-20250724-WA0058.jpg
    249.3 KB · Views: 19
  • IMG-20250708-WA0027(5).jpg
    IMG-20250708-WA0027(5).jpg
    186.1 KB · Views: 17
  • IMG-20250708-WA0028(6).jpg
    IMG-20250708-WA0028(6).jpg
    151.2 KB · Views: 22
  • IMG-20250510-WA0045(23).jpg
    IMG-20250510-WA0045(23).jpg
    115.6 KB · Views: 19
Wasalaam

Leo 24 Julai, 2025 asubuhi, nakiri kupokea taarifa kadhaa kutoka kwa Wananchi wa Kata ya Baraa, Mtaa wa Kibao cha Njano kwa Mrefu, Arusha.

Kwamba, mtu mmoja mzima analea binti wa umri kati ya miaka 8 hadi 10 hivi ambapo yaani ni anampa vipigo tu apendavyo yeye hivyo, mtoto amejaa makovu ya vipigo kila sehemu, ananyimwa chakula, anafungiwa mlango alale nje na mateso mengine aina hiyo hadi shuleni, maendeleo yanasua sua.

KILICHOFUATA: nimewasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha ambapo, maafisa ustawi wa jamii wameelekea eneo la tukio mara moja.

UJUMBE GANI KWA JAMII: tuache kutesa watoto, jicho la ustawi wa jamii linatamba alipo mwanajamii yeyote kwa ushirikiano na wananchi wenye mapenzi mema.

Hima, tuendelee kutamba na jicho la ustawi wa jamii 👁🇹 kuwadaka watu katili wa watoto popote/kokote 🇹🇿✍️

Pia, kumbuka kupiga 116 kituo cha taarifa za watoto. Vilevile, kuna namba za maafisa binafsi na za vituo vya huduma kwa wananchi hapa chini👇zikumbuke, mpe na mwingine.....
Muheshimiwa hizi namba za bure zipo active kweli?
 
Sasa mhe. waziri mbona unatoa taarifa za huyo binti wa miaka 8 kabla ya mtuhumiwa kukamatwa. Je akiwa ni mwana JF akabahatika kuiona hii taarifa hapa, na kuamu kutoroka, hapo utakuwa umetengeneza au umeharibu?
 
Kwamba, mtu mmoja mzima analea binti wa umri kati ya miaka 8 hadi 10 hivi ambapo yaani ni anampa vipigo tu apendavyo yeye hivyo, mtoto amejaa makovu ya vipigo kila sehemu, ananyimwa chakula, anafungiwa mlango alale nje na mateso mengine aina hiyo hadi shuleni, maendeleo yanasua sua.
Wengine tunatafuta hizi nafasi za kukaa na watoto, wengine wanazipata halafu wanazichezea. Hongera sana mheshimiwa kwa hatua za haraka ulizochukua, naamini utatupa mrejesho wa kilichobainika eneo la tukio.
 
Back
Top Bottom