beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kitengo cha Kupambana na Rushwa ya Ngono, imesema imejipanga kuanza kutoa elimu mtaa kwa mtaa ili kuhakikisha inawafikia watu wa rika zote.
Mkurugenzi wa Idara hiyo, Janeth Mawinza, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipofungua kikao cha mgawanyo wa majukumu na wadau mbalimbali katika taasisi hiyo pindi watakapoanza kutoa elimu hiyo.
"Leo (jana) tumeitana hapa na ninyi wadau katika taasisi hii ya kupambana na rushwa ya ngono ili kupeana mikakati ya kuanza kutoa elimu hii mtaa kwa mtaa, tutaanzia Wilaya ya Ilala siku ya Ijumaa," alisema.
Mkurugenzi huyo alisema rushwa ya ngono ni hatari zaidi ya rushwa ya kawaida kwa kuwa madhara yake ni makubwa kwa mwili wa binadamu, ikiwa ni pamoja na kifo.
"Tumejitoa kukomboa hiki kizazi ambacho kinaonekana kuanza kupotea kwa sababu ya rushwa ya ngono, rushwa hii ni hatari na inaua, ukiachana na kuua, pia inamweka mtu katika hatari ya kupata magonjwa hatarishi kama kaswende, na gono sambamba na kumharibu mtendwa kisaikolojia.
"Kikubwa tunaomba ushirikiano wa kutosha pindi mtakapoona tunapita mtaani kutoa elimu, tuna mambo mengi ambayo tunatamani jamii ijue juu ya hii rushwa ya ngono hasa kwa hawa wanafunzi na watoto wa kike ambao ndiyo wahanga wenyewe," alisema.
Ofisa kutoka Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi Ilala, Christina Onyango, alisema wako bega kwa bega na taasisi hiyo kuzuia rushwa ya ngono.
"Sisi Jeshi la Polisi kitengo hiki cha kupambana na hii rushwa, tunalo dawati letu la kushughulika na watu wanaokumbwa na adha ya rushwa ya ngono sambamba na kuwashughulikia watu wanojihusisha kuomba rushwa ya ngono," alisema
IPP MEDIA
Mkurugenzi wa Idara hiyo, Janeth Mawinza, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipofungua kikao cha mgawanyo wa majukumu na wadau mbalimbali katika taasisi hiyo pindi watakapoanza kutoa elimu hiyo.
"Leo (jana) tumeitana hapa na ninyi wadau katika taasisi hii ya kupambana na rushwa ya ngono ili kupeana mikakati ya kuanza kutoa elimu hii mtaa kwa mtaa, tutaanzia Wilaya ya Ilala siku ya Ijumaa," alisema.
Mkurugenzi huyo alisema rushwa ya ngono ni hatari zaidi ya rushwa ya kawaida kwa kuwa madhara yake ni makubwa kwa mwili wa binadamu, ikiwa ni pamoja na kifo.
"Tumejitoa kukomboa hiki kizazi ambacho kinaonekana kuanza kupotea kwa sababu ya rushwa ya ngono, rushwa hii ni hatari na inaua, ukiachana na kuua, pia inamweka mtu katika hatari ya kupata magonjwa hatarishi kama kaswende, na gono sambamba na kumharibu mtendwa kisaikolojia.
"Kikubwa tunaomba ushirikiano wa kutosha pindi mtakapoona tunapita mtaani kutoa elimu, tuna mambo mengi ambayo tunatamani jamii ijue juu ya hii rushwa ya ngono hasa kwa hawa wanafunzi na watoto wa kike ambao ndiyo wahanga wenyewe," alisema.
Ofisa kutoka Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi Ilala, Christina Onyango, alisema wako bega kwa bega na taasisi hiyo kuzuia rushwa ya ngono.
"Sisi Jeshi la Polisi kitengo hiki cha kupambana na hii rushwa, tunalo dawati letu la kushughulika na watu wanaokumbwa na adha ya rushwa ya ngono sambamba na kuwashughulikia watu wanojihusisha kuomba rushwa ya ngono," alisema
IPP MEDIA