TAKUKURU: Alex Msama bado anatafutwa

TAKUKURU: Alex Msama bado anatafutwa

Stuxnet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
18,846
Reaction score
29,341
Screenshot_20260515_231916_Lite.jpg


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kinondoni imesema inaendelea na msako wa Alex Msama ili ajibu mashtaka yanayomkabili

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam ijumaa, Mei 15, 2026, Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni, Elizabeth Mokiwa, amesema tangu watangaze kumtafuta bado hawajafanikiwa kumpata licha ya kutangaza donge nono kwa atakayefanikisha zoezi hilo.

Itakumbukwa, Januari 22, 2026 TAKUKURU ilitangaza kumtafuta ndugu Msama akikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi, yakiwemo kuongoza genge la uhalifu, kughushi nyaraka, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji fedha.

Soma Pia: TAKUKURU: Tunamtafuta Alex Msama ana mashtaka ya uhujumu uchumi na kuongoza genge la uhalifu. Atakayempata kuna zawadi nono

"Jitihada za kumtafutia Alex msama bado zinaendelea na kuna dau kwa atakayefanikisha kumpata" amesema Elizabeth akijibu swali la mwandishi wa habari juu ya hatima ya suala hilo.
 
Mtafutaji na mtafutwaji wanafanana kama mapacha sheikh, Best of lucky wampate ikiwa wamejiridhisha kuwa ni Mhalifu.
 
Muda wa drama za TAKUKURUCCM na kada mwenzao, kwamba jifiche nje ya nchi halafu tuseme tunakutafuta ili watu wajue ni kweli.

Haishangazi kujua ni sinema za majambazi ya CCM yanachezea watanganyika.

Hao TAKUKURUCCM wangekua sio tawi la CCM tungeanza kuona kazi yao kwenye ripoti ya CAG wangekamata yale majizi kwanza ndio waje kwa hawa akina Msama.

images (93).jpeg
 
Muda wa drama za TAKUKURUCCM na kada mwenzao, kwamba jifiche nje ya nchi halafu tuseme tunakutafuta ili watu wajue kweli.

Haishangazi kujua ni sinema za majambazi ya CCM yanachezea watanganyika.

Hao TAKUKURUCCM wangekua sio tawi la CCM tungeanza kuona kazi yao kwenye ripoti ya CAG wangekamata yale majizi kwanza ndio waje kwa hawa akina Msama.
Ni kweli
 
Muda wa drama za TAKUKURUCCM na kada mwenzao, kwamba jifiche nje ya nchi halafu tuseme tunakutafuta ili watu wajue ni kweli.

Haishangazi kujua ni sinema za majambazi ya CCM yanachezea watanganyika.

Hao TAKUKURUCCM wangekua sio tawi la CCM tungeanza kuona kazi yao kwenye ripoti ya CAG wangekamata yale majizi kwanza ndio waje kwa hawa akina Msama.
Mbeba maono anatafutwaje na Takukuru tena, kala nini?
 
Si waende kwake sinza 😄

Msama kamzingua nani huko juu,mbona mmemkalia
Kooni 😄
Ila naye msama mzushi mzushi sana 😄

Ova
Msama Mpigaji sana wa Viwanja kwenye Prime Areas..........Nakumbuka alikuwa na eneo Beach Front Mbweni JKT lilikuwa karibu na Mussa Mtimizi(Mtoto wa Waziri Tatu Mtimizi -Enzi za JK) nalo alilipata kwa UTAPELI.
 
Mtafutaji na mtafutwaji wanafanana kama mapacha sheikh, Best of lucky wampate ikiwa wamejiridhisha kuwa ni Mhalifu.
Sasa angekuwa siyo mhalifu si angeobekana openly? Amechemka kujificha
 
Back
Top Bottom