Ponjoro wa Kinondoni
JF-Expert Member
- Jan 5, 2024
- 3,536
- 9,611
Huyu kijana aliyekuwa anafanya kazi hapa kama operator wa forklift, aliacha ghafla kuja kazini wiki chache zilizopita. Nikafanya jitihada kumtafuta akawa hapokei simu.
Baada ya siku kadhaa akanipigia akaniambia anakaribia kuuza coin zake hivyo hafanyi kazi za kimaskini nitafute mtu mwingine.
Ukweli ni kuwa nilimpa muda wa kutafakari, baada ya ukimya kutawala ikabidi tutafute kijana mwingine.
Sasa leo kaja nyumbani na mjomba wake anaomba sana arudi kazini hata kwa kazi za kusaidia mafundi maana yakwake imeshachukuliwa.
Sasa naogopa kumwajiri tena huyu tajiri wa Pi - Network maana aliniambia yeye ni bilionea.
Niliwahi kuona uzi wa Pi hapa JF sijui matajiri wa hapa JF walifanikiwa au vipi? Nataka niwaunganishe na tajiri mwenzenu mpeane mbinu za kivita.
Baada ya siku kadhaa akanipigia akaniambia anakaribia kuuza coin zake hivyo hafanyi kazi za kimaskini nitafute mtu mwingine.
Ukweli ni kuwa nilimpa muda wa kutafakari, baada ya ukimya kutawala ikabidi tutafute kijana mwingine.
Sasa leo kaja nyumbani na mjomba wake anaomba sana arudi kazini hata kwa kazi za kusaidia mafundi maana yakwake imeshachukuliwa.
Sasa naogopa kumwajiri tena huyu tajiri wa Pi - Network maana aliniambia yeye ni bilionea.
Niliwahi kuona uzi wa Pi hapa JF sijui matajiri wa hapa JF walifanikiwa au vipi? Nataka niwaunganishe na tajiri mwenzenu mpeane mbinu za kivita.