Kuna jamaa nilimkopesha pesa aongezee akalipie matibabu ya mwanaye alikua na tatizo kwenye mishipa inayopeleka damu kwenye moyo, alinipigia simu sana akiniomba pesa akaniambia yuko tayari aweke rehani vyeti vyake na hati ya nyumba bado nilikua na kauzito kwa sababu mosi sijawahi mkopesha pesa hivyo sijui commitment yake ktk ulipaji pili pesa niliyonayo ni pesa ya biashara alivyoona simjibu siku moja asubuhi akaja na mtoto kambeba motto afya imezorota anapumua kwa shida huku jamaa akazungumza huku machozi yanamlenga akiomba nimsaidie basi niingiwa imani nilikua na sh.mil8.5 kwenye account yangu ya 1x bet nikazitoa zote nikampatia kwa ahadi kwamba azirudishe January hii, sasa January imefika jamaa nikimpigia ananijibu shit na kuniambia nikiona vipi niende mahakamani mahakama zipo kwa ajili ya watu, amenifanya nimekosa imani kabisa na wanadamu but kwa vile niliyemsaidia ni mtoto hana hatia basi nitamsamehe asiponilipa.