Taja madeni yako unayodaiwa

Taja madeni yako unayodaiwa

Kuna watu madeni yanawatia stress wanashindwa hata kula wakiyawaza wanaishia kufakufa tuwasaidie kwa kuwatajia madeni yetu ili wajione Hawapo peke yao.

Nikianza na Mimi mwenyewe.

1. Mkopo wa BOT(hazina)kila mwez 160000
2. Mkopo NMB kila mwezi 120000
3. Nyangao credit 90000 kila mwez bado miez miwili nimalize
4. Mama mwenye nyumba kodi 240000 miez mitatu
5. MGODI VODACOM 70000
6. Dukani kwa Rashid 30000
7. Nipige Tafu 21000
8. Fundi Fulani 50000
9. Maji na umeme 15000
10. Mfanyakazi mwenzangu alinikopesha 20000
11. Kwenye Mabar huwa sina madeni Makubwa ni kama 25000

Mimi nayowadai watu ni kama laki na kitu.
NB kama hudaiwi huna akili
 
ABSA makato kila mwezi 2,250,000/ (mkopo+ credit card+ life insurance)
Madeni mengine madogomadogo hayafiki 4m hadi Feb mwishoni nayamaliza
Kwanza ngoja niitafute chaka nikope 5m this week kuna ishu haipaswi kunipita ntajua namna ya kuilipa
 
Nilikuwa na madeni sana , mpaka iko siku nilienda kwa meneja wa benki kwenye tawi la wilaya anikopeshe elfu tano nipate hela ya nauli kurudi kituoni kwangu .

Yule mwamba alinipa elfu kumi yake huku anacheka na akasema nitaweka riba ya elfu mbili nililipa vizuri na sasa ni rafiki yangu .

Zingatia hapo nilipata mkopo wa mwanakijiji elfu ishirini ndiyo nikaenda kuinywa mjini na huko ikaisha nikakosa hata nauli

Basi kuna hela za urithi zilijaa nikaclear madeni yote , sasa niko free hata ukinistua kwenye bus nikiwa nimelala siogopi kama zamani.

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Zamani nilikua namuona anaedaiwa ni mpuuzi nimekuja kugundua kumbe ukidaiwa unakua active sana,nowdays nasikia raha sana kudaiwa muda mwingine silipi Ada za madogo makusudi ili wanisumbue naenda nawapiga kalenda nasepa siku nikijisikia nalipa
 
Zamani nilikua namuona anaedaiwa ni mpuuzi nimekuja kugundua kumbe ukidaiwa unakua active sana,nowdays nasikia raha sana kudaiwa muda mwingine silipi Ada za madogo makusudi ili wanisumbue naenda nawapiga kalenda nasepa siku nikijisikia nalipa
Loooooh,we msumbufu.
 
Nilikuwa na madeni sana , mpaka iko siku nilienda kwa meneja wa benki kwenye tawi la wilaya anikopeshe elfu tano nipate hela ya nauli kurudi kituoni kwangu .

Yule mwamba alinipa elfu kumi yake huku anacheka na akasema nitaweka riba ya elfu mbili nililipa vizuri na sasa ni rafiki yangu .

Zingatia hapo nilipata mkopo wa mwanakijiji elfu ishirini ndiyo nikaenda kuinywa mjini na huko ikaisha nikakosa hata nauli

Basi kuna hela za urithi zilijaa nikaclear madeni yote , sasa niko free hata ukinistua kwenye bus nikiwa nimelala siogopi kama zamani.

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom