Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 741
- 479
Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) imetua salama alfajiri ya Septemba 9, 2023 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ikitokea nchini Algeria kwenye mchezo wa wa kufuzu mashindano ya AFCON 2023 yatakayochezwa mapema mwakani 2024 nchini Ivory Coast.
Katika mchezo huo uliochezwa Septemba 7, 2023, Tanzania na Algeria zilitoka zilitoka sare ya bila kufungana (0-0), matokeo ambayo yanazifanya timu hizo kufuzu michuano hiyo, huku Tanzania ikifuzu kwa mara ya tatu katika historia ya mashindano hayo.
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kutua jijini Dar es salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu ambaye aliongoza msafara wa timu hiyo kwa niaba ya Serikali, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maono yake kwenye sekta ya michezo, hamasa pamoja na kuunga mkono timu hiyo.
Aidha, amewashukuru Watanzania wote kwa sala, dua na maombi yao na kuiunga mkono timu yao ya Taifa na kusisitiza kutakuwa na utaratibu mzuri kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) hatua itakayowezesha mashabiki waende kwa wingi nchini Ivory Coast mwakani 2024 kwenye michuano hiyo ili kuendelea kupeperusha vyema bendera ya taifa.
"Wizara yetu ambayo inaongozwa na Waziri Mhe. Dkt Damas Ndumbaro itaendelea kuyaishi maono ya Mheshimiwa Rais katika kuiendeleza wa timu ya Taifa na sasa ufadhili na uangalizi utaongezeka zaidi ili Ivory Coast tukafanye vizuri zaidi" amesema Katibu Mkuu Bw. Yakubu.
View attachment 2743865View attachment 2743866View attachment 2743868View attachment 2743867
Katika mchezo huo uliochezwa Septemba 7, 2023, Tanzania na Algeria zilitoka zilitoka sare ya bila kufungana (0-0), matokeo ambayo yanazifanya timu hizo kufuzu michuano hiyo, huku Tanzania ikifuzu kwa mara ya tatu katika historia ya mashindano hayo.
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kutua jijini Dar es salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu ambaye aliongoza msafara wa timu hiyo kwa niaba ya Serikali, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maono yake kwenye sekta ya michezo, hamasa pamoja na kuunga mkono timu hiyo.
Aidha, amewashukuru Watanzania wote kwa sala, dua na maombi yao na kuiunga mkono timu yao ya Taifa na kusisitiza kutakuwa na utaratibu mzuri kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) hatua itakayowezesha mashabiki waende kwa wingi nchini Ivory Coast mwakani 2024 kwenye michuano hiyo ili kuendelea kupeperusha vyema bendera ya taifa.
"Wizara yetu ambayo inaongozwa na Waziri Mhe. Dkt Damas Ndumbaro itaendelea kuyaishi maono ya Mheshimiwa Rais katika kuiendeleza wa timu ya Taifa na sasa ufadhili na uangalizi utaongezeka zaidi ili Ivory Coast tukafanye vizuri zaidi" amesema Katibu Mkuu Bw. Yakubu.
View attachment 2743865View attachment 2743866View attachment 2743868View attachment 2743867