Ivory Coast kuendelea kuisifu na kuiabudu Morocco ni upuuzi uliopitiliza

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,897
Katika mechi za mwisho hatua ya makundi katika mashindano ya AFCON 2023, Ivory Coast walikuwa wanahitaji Morocco ishinde mechi yake dhidi ya Zambia ili iweze kuinusuru Ivory Coast kuweza kuvuka hatua iliyofuata ya 16 bora. Na kweli, Morocco ilishinda 1-0 na Ivory Coast ikavuka kama best loser.

Toka wakati huo, watu wa Ivory Coast walianza kuishangilia Morocco katika mechi zake na baada ya Morocco kutolewa, wameendelea kuisifu na kuonyesha aina mbalimbali za mahaba kwa taifa hilo. Jana baada ya kuchukua ubingwa wa AFCON, waliishangilia sana Morocco baada ya bendera yake kuonyeshwa kwenye screen na kuna mchezaji wa Ivory Coast alizunguka uwanja mzima akipeperusha bendera ya Morocco.

Kwa nini nasema huu ni upuuzi uliopitiliza? Kuanzia mafanikio ya timu zao za taifa na ya wachezaji mmoja mmoja, Ivory Coast ni taifa kubwa katika ulimwengu wa soka, siyo tu hapa Afrika bali duniani kwa ujumla. Hawatakiwi kujidhalilisha kiasi hiki.

Pili, timu zote zinazojitambua zinataka zishindane na kushinda mechi zao zote hata kama ni za kirafiki au za kukamilisha ratiba. Morocco hawakuifunga Zambia kwa kuwa walikuwa wanataka kuwafanyia favor Ivory Coast bali walikuwa wanataka kushinda kwa sababu ni wajibu wao na kwa fahari ya taifa lao.

Iangalie Cape Verde ambao walienda mechi yao ya mwisho ya makundi dhidi ya Misri wakiwa tayari wameshafuzu ila walicheza kwa nguvu na jitihada utadhani wanapigania wasishuke daraja na wakalazimisha sare dhidi ya Misri iliyokuwa inaponea chupuchupu kutolewa. Hivyo ndiyo timu zote zinazojitambua zinavyotakiwa kucheza.

Embu waambieni Ivory Coast waache kujiaibisha. Matokeo ya mpira ndiyo yaliwavusha na siyo favor za Morocco.
 
Katika mechi za mwisho hatua ya makundi, Ivory Coast walikuwa wanahitaji Morocco ishinde mechi yake dhidi ya Zambia ili iweze kuinusuru Ivory Coast kuweza kuvuka hatua iliyofuata ya 16 bora. Na kweli, Morocco ilishinda 1-0 na Ivory Coast ikavuka kama best loser.
HAO WAMETUPIWA MAJINI MAANA DINI ILE KWA MAJINI BALAA
 
Aisee hukuelewa maana ya ile bendera umekurupuka,AFCON inayofuata inafanyika Morocco ndo maana ya bendera ya Morocco pale

Sent using Jamii Forums mobile app

Hakuelewa
Screen Shot 2024-02-12 at 4.29.37 PM.png
 
Mtoa mada huna akili, ile bendera iliriashiria kuwa next afcon itachezwa Morocco. Ila sio kosa lako najua kwa sababu wewe ni kolo.
Tuliza kijambio hiko, wewe mwenyewe una akili gani zinazokupa jeuri kusema wengine hawana akili? Ivory Coast walianza kuwashangilia Morocco toka round ya 16 bora
 
Nimetoa tu angalizo. Hizi nchi za watu weusi tuna historia ndefu za kuuza utu wetu kwa mambo ya kijinga sana.
Nilijua tu huu uzi umeuleta kwa misingi ya chuki ya Uafrika na Uarabu,acha ubaguzi hauwezi kukufikisha popote,prejudice is a chain,itakuhold maisha yako yote na hutaweza kumove on,

Kwa hivo Ivory coast wangekua na bendera ya taifa la watu weusi wewe ungeona ni sawa tu? Punguza chuki za kijinga kijana,

Mbona kuna watu wapo Kongo huko ila wanashabikia Argentina? Watu wapo Bongo ila wanashabikia England au taifa lolote la Europe au Amerika?

Kwanza Wewe unaonekana wala sio mtu wa mpira.
 
We boya nini
Kwenye mpira timu ambayo ikishinda inakupa nafasi ya kusonga mbele kwa nini usiishangilie, fuata kanuni hii, adui wa adui yako ni rafiki yako sawa we kolo.
Usichoelewa ni nini? Taifa kama Morocco haliwezi kukubali kufungwa kizembe kisa wanatimiza ratiba. Kila mechi kwao ni must win maana wameshajiwekea status ambayo lazima wailinde.

Na kwenye mpira hakuna huo uadui unaosema, ikitokea matokeo yangu yamekunufaisha au kukuumiza fresh tu, huo ndiyo mpira ulivyo.
 
Back
Top Bottom