Taifa Stars kuondolewa kwenye njia ya kwenda Qatar ni baraka toka kwa Mungu

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,313
12,613
Haya niambie!!! Taifa stars kwa ku fluke ikawa hiyooo hadi Qatar. Hebu tuseme ukweli ingekuwaje?

Taifa lengepata aibu inayoweza kuuangusha chini hata mlima wa Kilimanjaro. Timu hii ya akina Samatta na Kibu ingemwaibisha Waziri mkuu na kila mtu nchini.

Kilichoipata Zaire 1974 ambacho dunia inakumbuka hadi kesho ingekuwa cha mtoto.

MwenyeziMungu katunusuri na balaa zito.

Tunaomba serikali yetu sikivu ianze Sasa kutengeneza kikosi Cha kwenda USA na Mexico kuanzia Leo. Serikali iwekeze kwenye timu ya taifa kuanzia Sasa kwa kumwanga pesa kwenye soka la watoto na vijana.

TFF hakikisheni kuwa wachezaji wetu wote wanakuwa na maumbo makubwa wenye vipaji. Mikoa yenye wachezaji wenye maumbo makubwa inafahamika, nendeni huko mkachague watoto wenye vipaji na kuwaweka pamoja kuanzia utotoni.

Tusingojee kuwajaza pressure wachezaji kwa maneno na ahadi ya fedha siku ya mechi.
 
Wajinga nchi hii hawataisha kamwe.
We nani kakuongopea kua Tanzania tunafeli kwenye soccer kisa maumbo ya wachezaji wetu?
Hivi Korea kusini wanatuzidi maumbo?

Nb. Bora upate kidogo kuliko kukosa kabisa.
Ni bora alie ingia kombe la Dunia akafungwa hata goli 12 kwenye mechi moja, kuliko asie ingia kabisa.
 
Ukiitaja Tff katika mpira naona tushafeli ni kama kuitaja bakwata iwasaidie waislamu
 
Wajinga nchi hii hawataisha kamwe.
We nani kakuongopea kua Tanzania tunafeli kwenye soccer kisa maumbo ya wachezaji wetu?
Hivi Korea kusini wanatuzidi maumbo?

Nb. Bora upate kidogo kuliko kukosa kabisa.
Ni bora alie ingia kombe la Dunia akafungwa hata goli 12 kwenye mechi moja, kuliko asie ingia kabisa.
Aliyekwambia Korea wachezaji wote Wana maumbo madogo kakudanganya. Hata hivyo ni lini Korea imefika hata robo final kombe la Asia au world cup?
 
Wamekariri hawa.
Nitajie timu yenye vijitu vidogo kama Kaseja, shabalala, kibwana, gadiel, Samatta, nk iliyowahi kucheza finali za kombe la dunia.

Africa tunaongelea timu zenye wachezaji kama Drogba, samwel kufur, Eto, Asamoh, Obi, Kanu, okech, Yakin, na aina hiyo. Wachezaji wenye maumbo madogo sio wengi, kama wapo basi balaa lao sio dogo, highly talented kama Messi, ngolo, nk
 
Nitajie timu yenye vijitu vidogo kama Kaseja, shabalala, kibwana, gadiel, nk iliyowahi kucheza finali za kombe la dunia.
Japan

Korea kusini

China

Korea Kaskazini

Mpira sio umbo kubwa tu...
 
Aliyekwambia Korea wachezaji wote Wana maumbo madogo kakudanganya. Hata hivyo ni lini Korea imefika hata robo final kombe la Asia au world cup?
Sasa alie kuambia Tanzania wachezaji wote wanamiili midogo nani?
Kwani Lusajo na Mess nani mwenye jumbile dogo?

Alafu hoja hapa ni kushiriki world cup sio kuingia Robo fainali.

Kama kweli we ni mfuatiliaji wa soccer niambie mwaka gani ambao Korea kusini hakushiriki world cup?

Nitajie mchezaji wa Korea kusini mwenye jumbile kubwa kuwazidi Lusajo na Mwaikimba?

Mkuu huna hoja, unazingua bangi zetu wakushi.
 
Nitajie timu yenye vijitu vidogo kama Kaseja, shabalala, kibwana, gadiel, iliyowahi kucheza finali za kombe la dunia.

Hizo timu zinafanya vizurii kombe la dunia?
Muhimu zinashiriki tu....huko kufanya vizuri ni majaliwa tu.

Hata hao wenye maumbo sio wote wanafanya vizuri isitoshe toka mwaka 2006 mpaka Sasa mataifa ya ulaya magharibi wametwaa hili kombe mfululizo sidhani sababu ya mafanikio yao ni maumbo tu
 
Nitajie timu yenye vijitu vidogo kama Kaseja, shabalala, kibwana, gadiel, Samatta, nk iliyowahi kucheza finali za kombe la dunia.

Africa tunaongelea timu zenye wachezaji kama Drogba, samwel kufur, Eto, Asamoh, Obi, Kanu, okech, Yakin, na aina hiyo. Wachezaji wenye maumbo madogo sio wengi, kama wapo basi balaa lao sio dogo, highly talented kama Messi, ngolo, nk
Argentina.
Anza na Diego Maradona.
Njoo kwa Diabara
Mtazame Khun Agüero
Sijui unamjua Juninho Canambucano?

Kiufupi maumbo sio fact kwa Tanzania kufanya vibaya kwenye soccer.

Fact hapa, sisi watanzania ni wavivu na mbaka leo tunaamini miujiza kuliko sayans

Wengi tunaamini tutafanikiwa kwa njia ya mkato badala ya mipango, ndio maana bongo hakuna mchezo wowote Duniani ambao tunafanya vizuri kimataifa.

Mfano mazuri angalia Olimpiki ilio fanyika mwaka huu huko Japan, jiulize kama taifa tulipeleka wanamichezo wangapi, na nini walicho kifanya?

Tanzania, sio Riadha
Sio soccer
Sio ngumi
Sio kuogelea
Kiufupi kuna sababu nyingi zinazo pelekea soka letu liwe la hovyo, moja wapo ndio hilo la uvivu.
 
Nitajie timu yenye vijitu vidogo kama Kaseja, shabalala, kibwana, gadiel, iliyowahi kucheza finali za kombe la dunia.

Hizo timu zinafanya vizurii kombe la dunia?
Kwani tunazungumzia kufanya vizuri ama kushiriki?
Kwani kuna inchi gani África iliyo wahi kufanya vizuri world cup?

Nb. Tangu nimeanza kuangalia michuano ya kombe la Dunia 1998 pale Ufaransa mpaka leo sijawahi kuiona timu ya Taifa ya England ikifanya vizuri kwenye kombe la Dunia.
 
Sasa alie kuambia Tanzania wachezaji wote wanamiili midogo nani?
Kwani Lusajo na Mess nani mwenye jumbile dogo?

Alafu hoja hapa ni kushiriki world cup sio kuingia Robo fainali.

Kama kweli we ni mfuatiliaji wa soccer niambie mwaka gani ambao Korea kusini hakushiriki world cup?

Nitajie mchezaji wa Korea kusini mwenye jumbile kubwa kuwazidi Lusajo na Mwaikimba?

Mkuu huna hoja, unazingua bangi zetu wakushi.
Hata wagonjwa Kuna mahututi wa ICU, wagonjwa wa wodini na wagonjwa wanaofuata matibu na kuondoka siku hiyohiyo (OPD). Korea inatoka kwenye Bara ambalo ni wagonjwa kwenye mchezo wa mpira wa miguu, hivyo Korea ni mgonjwa mwenye nafuu kwenye kundi. Anawashinda wagonjwa wenzake kama India, Pakistan, Afghanistan, Iraq, Saudia, China, nk. Lakini nakwambia kama nchi za Africa Kaskazini kama Egypt, Morocco, Tunisia, Algeria,nk zingehesabiwa kuwa ziko Asia pia hao Korea usingewaona world cup hata siku moja.

Lakini narudia tena kuwa hata Korea Kuna wenye miili mikubwa na warefu pia.
 
Hata wagonjwa Kuna mahututi wa ICU, wagonjwa wa wodini na wagonjwa wanaofuata matibu na kuondoka siku hiyohiyo (OPD). Korea inatoka kwenye Bara ambalo ni wagonjwa kwenye mchezo wa mpira wa miguu, hivyo Korea ni mgonjwa mwenye nafuu kwenye kundi. Anawashinda wagonjwa wenzake kama India, Pakistan, Afghanistan, Iraq, Saudia, China, nk. Lakini nakwambia kama nchi za Africa Kaskazini kama Egypt, Morocco, Tunisia, Algeria,nk zingehesabiwa kuwa ziko Asia pia hao Korea usingewaona world cup hata siku moja.

Lakini narudia tena kuwa hata Korea Kuna wenye miili mikubwa na warefu pia.
Mtaje mchezaji mmoja mwenye umbo kubwa kwenye kikosi cha Korea kusini.
 
Back
Top Bottom