Naona Watanzania tumechoka na amani.
Upinzani walijenga hoja nzuri sana ya kuutokomeza UFISADI ambayo karibuni iing'oe CCM. Lakini walifanya kosa kubwa la kiufundi kwa kumleta Lowassa kama kinara wao.
Kuanzia pale upinzani wamejaribu sana kuisambaratisha serikali ya Magufuli kwa kutumia kila mbinu za kisiasa lakini wanaona wameshindwa kabisa. Hii ni dhahiri ukiangalia wananchi wa kawaida walivyorudi kuipenda CCM kwa kura wanazowapa.
HATARI
Sasa upinzani, wakiongozwa na CDM (na namshangaa Zitto nae pia yumo) wameamua kuwatumia wananchi (mithili ya UKUTA) kuleta vurugu nchi nzima kwa migomo na maandamano. Wanataka kutumia fujo hizi ili nchi isitawalike. Hiki kitu ni hatari sana.
Ni matumaini yangu kuwa Watanzania watayapuuza matakwa yao haya, kama walivyowapuuza kwa kuwakataa wagombea wao katika chaguzi hizi ndogo.
Hivi watu wana akili za kivipi? Mange yupo Marekani full-kiyoyozi anawashakiza muingie mitaani kupinga serikali na nyie kweli mnaitikia. Atakaelambwa virungu, maji ya washawasha, mabomu ya machozi, na risasi za moto ni nyie na watoto wenu.
Kwa kipi lakini?

Kwa sababu Mbowe na genge lake la wahuni wameishiwa na mbinu halali za kisiasa za kuchukua dola?

Au ni kwa sababu Mbowe na upinzani kwa ujumla wamekwishabaini kuwa, kwa mwendo huu ifikapo 2020 hawatapata wabunge wala madiwani na ndio itakuwa mwisho wa ruzuku?
Vijana msikubali kutumiwa na watu, hasa walioko nje ya nchi, kuvunjisha amani. Wenzenu wamekaa ndani na wanaangalia kinachoendelea mitaani kama sinema vile. Mwisho wa siku sio Mbowe, Zitto, au Mange atakaeumia au kufa. Ni wewe unaeshakizwa kama mbwa ukaumie ili waone machafuko.
Kuandamana ni hiari yako. Lakini kabla hujatoka nyumbani na kuingia mitaani jiulize, NINAPIGANIA KITU GANI HASA. Kama ukijiridhisha kuwa kuna maslahi yako ya kupigania basi endelea la sivyo ujue unatumiwa.