Sanctus Mtsimbe
R I P
- Jul 14, 2008
- 1,820
- 1,031
Wazalendo;
Asalaam Aleykhum.
Napenda kutoa tahadahri kwa watumiaje wa barabara ya Mandela wakati wa Usiku.
Siku ya Ijumaa iliyopita nilikuwa naendesha gari along Mandela Road nikiwa natokea katika tafrija ya harusi Mbezi. Ilikuwa yapata saa nane za usiku/alfajiri. Tulikuwa Wanne katika gari.
Mara baada ya kupita Landmark Hotel (Nikielekea upande wa Buguruni)karibu na njia panda ya kwenda Mabibo Hostel; tuliwaona vijana kama kumi wakiwa wamefunga barabara kwa mawe makubwa na gogo. Kwa haraka, tulishauriana kuwa haikuwa salama na tukaanza kurudisha gari reverse na kusubiri. Baada ya muda vijana wale walitoa mawe yale na gogo, nikaendesha gari kwa speed sana mithili ya mtu anayetaka kuwagonga, wakatupisha.
Baada ya kupita salama, nilijaribu kupiga simu ya Emmergency 112 Kuomba msaada kwa Wanausalama wetu kuja kuwadhibiti wale waharifu, lakini automatic reply inilijulisha nisubiri dakika 17 kupata huduma ya kusikilizwa. Nilijaribu mara kadhaa lakini majibu yalikuwa yale yale.
Nilipojaribu Simu ya Kamanda Kova ilikuwa imezimwa.
Naomba sana Wazalendo mnaotumia barabara ile wakati wa usiku muwe makini sana.
Asalaam Aleykhum.
Napenda kutoa tahadahri kwa watumiaje wa barabara ya Mandela wakati wa Usiku.
Siku ya Ijumaa iliyopita nilikuwa naendesha gari along Mandela Road nikiwa natokea katika tafrija ya harusi Mbezi. Ilikuwa yapata saa nane za usiku/alfajiri. Tulikuwa Wanne katika gari.
Mara baada ya kupita Landmark Hotel (Nikielekea upande wa Buguruni)karibu na njia panda ya kwenda Mabibo Hostel; tuliwaona vijana kama kumi wakiwa wamefunga barabara kwa mawe makubwa na gogo. Kwa haraka, tulishauriana kuwa haikuwa salama na tukaanza kurudisha gari reverse na kusubiri. Baada ya muda vijana wale walitoa mawe yale na gogo, nikaendesha gari kwa speed sana mithili ya mtu anayetaka kuwagonga, wakatupisha.
Baada ya kupita salama, nilijaribu kupiga simu ya Emmergency 112 Kuomba msaada kwa Wanausalama wetu kuja kuwadhibiti wale waharifu, lakini automatic reply inilijulisha nisubiri dakika 17 kupata huduma ya kusikilizwa. Nilijaribu mara kadhaa lakini majibu yalikuwa yale yale.
Nilipojaribu Simu ya Kamanda Kova ilikuwa imezimwa.
Naomba sana Wazalendo mnaotumia barabara ile wakati wa usiku muwe makini sana.