Tahadhari: Lifts(Elevators) zinaweza kuua!

Tahadhari: Lifts(Elevators) zinaweza kuua!

Poleni sana Aise
Saa kama tatu hivi zilizopita nilikua Kariakoo kwenye jengo moja la ghorofa saba ambalo hutumika kama makazi ya watu na ofisi pia. Ofisi niliyokua naenda ipo ghorofa hiyo ya saba ambapo ilinilazimu nipande lift

Nilipobonyeza kitufe cha namba ya floor ninayoenda akawa amekuja dada ambaye kwa mavazi yake nikahisi alikua ametoka au anakwenda kwenye mazoezi (nadhani kwenye jengo lile ipo gym) hivyo ikanilazimu nibonyeze kitufe cha kumsubiria akapanda tukaondoka

Sekunde chache tu baada ya kuondoka tukiwa tunapita floor ya tatu taa zikazimika ndani ya ile lift, ikatoa mlio kama imegonga kitu halafu ikawa kama inarudi chini kisha ikasimama kabisaa! Yule dada akapiga yowe la ku panik. Nilipomwambia asiwe na wasiwasi tutatoka akanisogelea na kunikumbatia huku anaendelea kupiga kelele

Changamoto kubwa ni ile milango ya lift yenyewe ilivyokua mizito mpaka unahisi kabisa hata hizo kelele hazifiki popote. Nilinyoosha mkono na kubonyeza kitufe cha emergency bila kuondoa mkono(continuously) lakini hatukuweza kupata msaada kwa haraka

Hali ilikua ya taharuki kubwa maana kile kichumba cha lift ni kdogo, milango ni minene sana na joto lilikua linaongezeka. Tulikaa mle kama dakika saba au nane ambazo zilikua kama mwaka ndipo zikasikika sauti za watu kwa nje wakiwa wanashughulika kutufungulia mlango na muda walipofanikiwa kutufungulia yule dada niliyekua nae alikua amelala chini kwenye sakafu ya lift na akawa kama anaeelekea kupoteza fahamu!!!

Namshukuru Mungu tulitoka salama ingawa yule dada ilibidi apelekwe hospitali kwa hali aliyokua nayo maana hata mambo yake mengine ya kiuanamke (tafsida imezingatiwa) yalimuharibikia na ukizingatia mavazi aliyokua amevaa hakutarajia pengine mambo yamtokee wakati huo!

Wito wangu kwa watengeneza elevators, watengeneze lifts za milango transparent ili mtu aweze kuona nje angalau pressure inapungua kuliko hizi lift zenye milango utadhani gereza au kaburi aisee! Mtu unapokua unawaona watu nje unajua muda wowote unatoka. Amakweli kifo kwa binadamu ni sekunde tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ilishawahi nitokea kwenye jengo la muhimbili (MoI) tulikuwa kama 6 kwenye lift afu goma likazima kati tulikaa mle kama dk 10 hewa nzito kinoma watu full mikelele at the end wakaja kutufungulia tunasweat balaa jicho nyanya ...sitosahau asee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeniuliza kama ninawajua.Nimejibu kama wangekuwa na faida ya kuweka ugali mezani binti yangu Wakuru akala ningewajua.They have got nothing aside maandishi yao.
Kupitia maandishi ndipo tulipojifunza ustaarabu tulionao sasa. Haijalishi andiko linakuvutia wewe au la, ila elewa kila andiko liwe la kipuuzi au la hekima lina impact kwenye jamii yoyote. Wengine wanavutiwa na maandiko matakatifu na wanayafuata ila wanajishuhulisha na shuhuli za kuzalisha kipato, maandiko yana sehem yake na umuhimu wake. Wengine hayajui na wala hawana mpango wa kuyajua maandiko yako uyaonayo bora na yanakuletea kipato na rizki mezani na wanaishi vyema pengine hata kukushinda wewe.
Nimekuuliza wawafaham hao jamaa wawili nikimaanisha kupitia maandiko yao kwani umeonyesha kutomuunga mkono mmoja wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa ni fundi wa kizazi hiki. Uliishia wapi labda nikumegee ka utam kidogo. Msome pia kwenye Sniper, Wimbo wa gaidi, Mtuhumiwa, Utata wa 9/12 1&2. Kwa uchache,Ila kwa sasa yupo on fire na Mtafiti.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani hata sikumbuki vizuri best, niliishia pale mchumba wake anamsisitiza aende akatibiwe sina hakika kama niliendelea zaidi ya pale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom