sixgates
JF-Expert Member
- Mar 19, 2011
- 3,979
- 1,662
Kwa watu wote, wanademokrasia na hata wale wahafidhina tufikie mahali tuweze kuzitenganisha propaganda na media spinning zinazoendelea kwa sasa kuhusu issue ya Zitto na chadema.
Natoa tahadhari kubwa sana hapa jamvini na nitasambaza hizi taarifa kwa vyombo vingine vya habari na social media nyingine.
Kuna baadhi ya watu wanaojiita "TEAM ZITTO" ambao pengine kwa nia njema ama kwa maksudi tu wanaharibu Taswira ya Mh Zitto Kabwe kwa kujaribu kutembea katika jina la Zitto kutoa Matamko, maneno na kuratibu mikutano isiyo rasmi kwa kusema wao ni TEAM ZITTO. Imebainika katika kufanya hivi sio tu inamchafua Zitto bali ina lengo la kumchonganisha Ndg Zitto na aidha viongozi wa chadema, kamati kuu ya chama, wapenzi,mashabiki wa chadema, marafiki na hata wananchi. Ajenda zinazoibuliwa na kikundi kinachojiita TEAM ZITTO ni tofauti na zile Zitto alizoziainisha mbele ya vyombo vya habari.
TUHUMA ZITTO ALIZOZIAINISHA KWA VYOMBO VYA HABARI
- Kutokushiriki kampeni za urais
- kutoshiriki operation za chama
- ukaguzi wa vyama
- posho za vikao
Zitto hajazungumzia lolote kuhusu Ukanda, Ukabila, ieleweke na iwe wazi tatizo aliloliainisha ni mapambano ya kukuza demokrasia ndani ya chama, mapambano dhidi ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina.
Kwa namna yoyote Zitto Kabwe asihusishwe na taarifa tofauti na hizi, asihusishwe na baadhi ya maandamano, asihusishwe na mikutano inayoratibiwa na wanaojiita TEAM ZITTO. Kama kuna taarifa zozote ambazo zinamuhusu zinukuliwe kutoka kwake moja kwa moja na sio mkusanyiko wa soga zisizo za msingi wowote.
Mwisho, kwa wale wote wapenda demokrasia watambue nyakati ngumu ni sehemu ya maisha ya binadamu, Zitto amekubali kufuata taratibu zote za chama kuhakikisha anahitimisha mtikisiko huu kwa hekma na kwa uvumilivu mkubwa.
Sixgates
DSM
Natoa tahadhari kubwa sana hapa jamvini na nitasambaza hizi taarifa kwa vyombo vingine vya habari na social media nyingine.
Kuna baadhi ya watu wanaojiita "TEAM ZITTO" ambao pengine kwa nia njema ama kwa maksudi tu wanaharibu Taswira ya Mh Zitto Kabwe kwa kujaribu kutembea katika jina la Zitto kutoa Matamko, maneno na kuratibu mikutano isiyo rasmi kwa kusema wao ni TEAM ZITTO. Imebainika katika kufanya hivi sio tu inamchafua Zitto bali ina lengo la kumchonganisha Ndg Zitto na aidha viongozi wa chadema, kamati kuu ya chama, wapenzi,mashabiki wa chadema, marafiki na hata wananchi. Ajenda zinazoibuliwa na kikundi kinachojiita TEAM ZITTO ni tofauti na zile Zitto alizoziainisha mbele ya vyombo vya habari.
TUHUMA ZITTO ALIZOZIAINISHA KWA VYOMBO VYA HABARI
- Kutokushiriki kampeni za urais
- kutoshiriki operation za chama
- ukaguzi wa vyama
- posho za vikao
Zitto hajazungumzia lolote kuhusu Ukanda, Ukabila, ieleweke na iwe wazi tatizo aliloliainisha ni mapambano ya kukuza demokrasia ndani ya chama, mapambano dhidi ya wapenda demokrasia dhidi ya wahafidhina.
Kwa namna yoyote Zitto Kabwe asihusishwe na taarifa tofauti na hizi, asihusishwe na baadhi ya maandamano, asihusishwe na mikutano inayoratibiwa na wanaojiita TEAM ZITTO. Kama kuna taarifa zozote ambazo zinamuhusu zinukuliwe kutoka kwake moja kwa moja na sio mkusanyiko wa soga zisizo za msingi wowote.
Mwisho, kwa wale wote wapenda demokrasia watambue nyakati ngumu ni sehemu ya maisha ya binadamu, Zitto amekubali kufuata taratibu zote za chama kuhakikisha anahitimisha mtikisiko huu kwa hekma na kwa uvumilivu mkubwa.
Sixgates
DSM