Bella Ciao
JF-Expert Member
- May 28, 2019
- 1,804
- 4,469
Watu wengi wamesema mafuta ya taa, oil chafu nk... ila kwa kawaida kama unatakiwa umwagie kwa kuzunduka nyumba nzima na hauwezi mwaga kila mahali... Mafuta yana harufu kali.. Na oil ni uchafu..Naomba wajuvi mtuambie ni dawa gani itasaidia kuwapunguza kama siyo kuwafukuza kabisa hawa wadudu?inatisha sana maana nyumbani watoto bado wadogo na ijumaa ya week iliyoisha nilipigiwa simu mchana kwamba wamemuona huyu nyoka wa kijani aki-survey maeneo ya nje ya nyumba.
Nimeuliza watu nilio nao karibu wananiambia oil chafu inasaidia sasa sijui ni kweli!
Njia rahisi ni kuchoma tairi la gari kwa kuhakikisha moshi umesambaa eneo lote la nyumba... Unaweza kufanya hivi kila baada ya miezi miwili au mitatu kama eneo ulilopo kuna nyoka nyoka





