We mama muogope Mungu
Sogea tu hapo Mkuranga,Kibiti,Ikwilili halafu uongee hizo kauli zako za dharau juu ya wasiolipwa pesa zao uone kama utabaki salama.
Watu hawajui hatima ya mashamba,sio palizi sio dawa vyote ni mtihani kwao na muda ndio huu umewadia.
Unapotetea jambo liweke katika muktadha wa dini na upime kama walichofanyiwa wakulima wa korosho ni haki au batili.
Ya mwaka huu atanunua nani? Ni sawa una watoto wawili,mmoja kafika umri wa kuanza shule halafu unamwambia kaa nyumbani eti utunze fedha za kumpeleka mdogo shule wakati hali ya mkubwa huijui.Ni ushauri mzuri hata hivyo korosho ya msimu ujao imeshapata mnunuzi na benki ya Mkombozi imeshatenga kiasi cha sh trilioni 1 kwa ajili ya zoezi hilo.
Ahsante kwa ushauri!
Hizo ndizo huitwa akiliccm.. wanajaribu kuzima moto kwa petroli[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Eti mnunuzi wa korosho za msimu ujao ,
Kwanini sio hizi korosho zinazoozea ghalani???
Mku kumbuka hiyo demand iliyopo kuna kuharibika pia.Kwanza kumbuka kuwa kwenye mazao yapo aina mbili kuu, mazao ya chakula na mazao ya biashara.
Korosho ni zao la biashara, biashara ya korosho soko lengwa ni la Kimataifa ili mpate fedha za kigeni.
Korosho iliyobanguliwa na kufungashwa vizuri ina soko kubwa sana duniani. Hilo halina shaka.
Ushindani wa kibiashara utakuwepo, fitna na majungu yatakuwepo lakini mwisho wa siku biashara itafanyika tu kwani demand ipo.
Kila mtu ana haki ya fursa zilizopo. Tazama vizuri post namba moja uone sababu zilizowataja Bakhrea na MO, tena kwa kukujuza tu kuna neno "kama".IFIKE HATUA KAMA KWELI WATU WANAONA TZ KUNA FURSA NZUURI YA KUTENGENEZA FEDHA BASI KILA MTU ATAJE MTU MMOJA KWENYE UKOO WAKE AU FAMILIA YAKE AU YEYE MWENYEWE ATUAMBIE AMEFANIKIWA KIASI GANI ILI NASI TUPATE MWANGA NA SIO KUTUTAJI AKINA MENGI, MO NA BAKHRESA
Hayo uyasemayo ndiyo sababu kuu ya mimi kuandika waachiwe wafanya biashara wakubwa wafanye biashara hizo na si serikali. Isome vizuri post namba moja.Mku kumbuka hiyo demand iliyopo kuna kuharibika pia.
Kuna kauli aliwahi kuitoa Babu yangu wa kitaifa na mwasisi wa chama changu Ccm Mwalimu Nyerere yakuwa Vikao vya kidunia vikifanyika huwa wanajadili hata Korosho ya Mzaramo huku Afrika kwa hiyo kujadili kwao ni kutupangia bei ya kuinunua hiyo korosho.
Kwa maana hiyo hizi kauli nyingi zilizotoka kwa watu wanaojiita Wazalendo za kuwakejeli hawa wanunuzi kuwaita Mabeberu tutegemee kuendelea kususiwa hili zao au kama ilivyokuwa Mbaazi ambayo nayo imekosa soko baada wanunuzi kulisusia.
Hizi kauli tunatakiwa kuwa nazo na kuzitoa kwa umakini mkubwa.
Sio kila kinachotoka kinywani kila Mtu atakikubali atakikubali baada kukifanyia uchambuzi tusitumie sana mihemko isiyosaidia mwisho inatupeleka kwenye mkwamo
Waumizwe zaidi ya korosho za kununuliwa kwa bei ndogo?Ya mwaka huu atanunua nani? Ni sawa una watoto wawili,mmoja kafika umri wa kuanza shule halafu unamwambia kaa nyumbani eti utunze fedha za kumpeleka mdogo shule wakati hali ya mkubwa huijui.
Wakulima wa korosho waruhisiwe wauze korosho zao kwa bei elekezi. Wanaoumia ni wakulima.
Sawa bibi nimekuelewa.Waumizwe zaidi ya korosho za kununuliwa kwa bei ndogo?
Ni wakati muafaka ushauri wa bibi ufatwe.
Hao akina Bakhressa hawakopi wakafungie viwanda vya kusaka political millage, wanakopa na kufungua viwanda vinavyolipa. Mimi niliwahi kushauri kwakuwa sera ya viwanda ni ilani ya ccm, basi ccm waanze kuwa mfano, wao kuanzia rais na mawaziri wakope na kufungua viwanda kisha wazalishe, tukishaona mfano toka kwao tutavutika.
Maana wanaccm huwa tunawaona kwenye chaguzi kuanzia rais, wabunge na mawaziri wakitumia nguvu zao zote na kusaidiwa na vyombo vya dola kuhakikisha hawapotezi madaraka. Nguvu hizo hizo wazitumie kufungua viwanda tuone ubora wao maana viwanda vinalipa kuliko urais, uwaziri, ubunge nk. Sio ushauri akina Mo wakope kufungua viwanda, halafu nyie muue, mloge, mtoe rushwa kuhakikisha mnapata madaraka.
Well then, umeeleweka mkuu. Zao la korosho kama yalivyo mazao muhimu ya biashara linahitaji mjadala mpana hasa kipindi hiki ambapo serikali "imechafua" utaratibu.. mawazo ya wanazuoni kama wewe na ukiwa mdau wa korosho ni muhimu ili kusaidia nini kifanyike katika kuendeleza zao hilo na utafutaji wa masoko etc. Huenda analysis yako ingesaidia wakulima kadhaa huku mtwara..(who knows?)Tanzania tumezoweshwa mambo "complicated" ndiyo eti mazuri. Binafsi naamini the "simpler the best".
Siupendi ukiritimba hata kwenye mawazo au maandishi.
Serikali ya kuteka, serikali ya visasi, au unamaanisha serikali IPI?"Se non sta andando bene, chiama tua nonna." Hiyo ni methali maarufu ya Kitaliano ambayo nimepata tabu kidogo kutafuta ya Kiswahili inayofanana-nayo, sijafanikiwa kuipata. Kwa tafsiri isiyo rasmi inasema "ikiwa hakuna linalokwenda sawa, muone bibi".
Nafahamu Kitanzania ukisema "kumuona bibi" au "babu" wengi wengine huhusisha na kuwaona mabibi na mababu ili waongee na mizimu mambo yaende sawa. Wataliano kwa msemo wao huo hawamaanishi kama Watanzania, Wataliano wanamaanisha umuone bibi kwa hekima na busara zake. Labda niifananishe na methali yetu ya "uzee ni dawa".
Binafsi kama bibi, leo nimedhamiria kutoa tafakuri yangu kwenye zao la korosho na ufumbuzi wa "matatizo" ya zao hilo.
Kwanza napenda ku "declare interest" kuwa binafsi ni mdau wa korosho kwa kuwa na mikorosho, mingi tu, tiliyoirithi toka mashamba ya mabibi zetu ile mbegu ya asili ya kizamani mpaka tumejaribu kuiendeleza na kupanda ya kisasa na tunaliona tija nzuri tu.
Ushauri: Serikali ijitowe kimasomaso kuwakopesha bila riba wafanya biashara wakubwa wenye uzoefu wa viwanda kama vile akina Bakhresa na Mo kufunguwa viwanda vikubwa vya kisasa vya kubangua, kusindika na kufungasha korosho kwa kiwango cha Kimataifa na kuwasaidia kushindana na masoko ya Kimataifa.
Hiyo ni badala ya serikali kuingilia zao hilo.
Sababu kuu ni kuwa wafanya biashara hao tayari wana uzoefu mpana wa viwanda vya "food processing" na tayari wana mitaji katika nchi kadhaa za SADC na Afrika Mashariki.
Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy .
Juzi Mheshimiwa Rais amesema wanaoona hali ngumu ni wale waliozowea pesa zisizo halali.
Soma para ya kwanza ya post namba moja. Kama hujaielewa soma para ya tatu kama hujaielewa soma upya post yote namba moja kisha endelea na posts za majibu, utaelewa tu.Ukishaiomba serikali ikopeshe bila riba ili kijengwe kiwanda ina maana tayari kuna chaos! Hilo umeliomba mwenyewe! Huoni tayari kuna shida mahali?
Korosho ndiyo zimekuteka?Serikali ya kuteka, serikali ya visasi, au unamaanisha serikali IPI?
Hebu 2020 tufanye mabadiliko, alafu ndo uje ushari vinginevyo wazungu wanasema "you beat around/ about the bush"
Hata sasa wenye hela wapo. Hujawaona juzi wakiongea kero zao?Turudi tu kwenye issue ya korosho, wakulima hawaoni hali ni ngumu? Je, walizoea pesa zisizo halali?
Rais alipoongea na wafanyabiashara hakusikia kero na vilio vya wafanyabiashara? Hizo kero ndizo chanzo cha hali ngumu na pia mzunguko wa uchumi ni mdogo kwa mtu mmoja mmoja hivyo maisha kuwa magumu. Kumekuwa na kodi nyingi mno zisizo na utaratibu kiasi ambacho mtu aliyekopa hela za SACCOS au bank badala ya kusogea mbele kiuchumi, anarudi nyuma pengine uli mortgage nyumba au samani za ndani unajikuta unavipoteza ukiona.
Ni miaka minne sasa imepita utawala wa awamu ya 5, sikatai hela kuwepo enzi za JK lkn sidhani kama wote waliokuwa na hela walikuwa mafisadi.
Wakulima wanachotaka ni kuuza korosho zao hawajali nani anaezinunua. Iwe binaadam au shetani wao wanahitaji pesa tu.Well then, umeeleweka mkuu. Zao la korosho kama yalivyo mazao muhimu ya biashara linahitaji mjadala mpana hasa kipindi hiki ambapo serikali "imechafua" utaratibu.. mawazo ya wanazuoni kama wewe na ukiwa mdau wa korosho ni muhimu ili kusaidia nini kifanyike katika kuendeleza zao hilo na utafutaji wa masoko etc. Huenda analysis yako ingesaidia wakulima kadhaa huku mtwara..(who knows?)
Hiyo "mkinishauri" umeongezea wewe.Nakumbuka kwenye uzinduzi wa fly over ya ubungo unayetaka ashauriwe Alisema haya “ mnahangaika kwenye Mitandao ya kijamii mnaposti hili mara lile kunipangia la kufanya, Mimi huwa sipangiwi na ukinipangia ni kama unaingilia uhuru wangu, hakuna aliyenichukulia fomu ili nigombee nilichukua mwenyewe. Mkinipangia/mkinishauri ndio mnaharibu kabisa” Bibi FaizaFoxy huyajui haya au CCM huwa mnafikiria kwa kutumia nini. Kulishauri jitu linalojifanya linajua kuliko watanzania wote ni UBOYA. Umechemka bibi.
Punguza kelele. Mbona unatupigia kelele na maandishi ya ilani?KUNA WATU WAPUUZI SANA YAANI UKIZUNGUMZIA WATU HAWAFANIKIWI HAPA TZ KUTOKANA NA MAZINGIRA MABOVU NA SERA ZA ZISIZORAFIKI WATU KUTUSUA UTASIKIA MTU ANAKUTAJIA MENGI, BAKHRESA, MO LAKINI HATAJI HATA MTU MMOJA WA UKOO WAKE AU KABILA LAKE AU JIRANI YAKE ALEFANIKIWA, SWALI JE INAMAANA UKOO MZIMA HAWAHANGAIKI KUTAFUTA MAPENE? JE UKOO MZIMA NI MBUMBUMBU WA MAISHA JIBU JEPESI NI KWAMBA WATU WANHANGAIKA KADRI WAWEZAVYO TATIZO HAKUNA MAZINGIRA RAFIKI YA WATU KUTUSUA UKIFIKIA LEVEL FLANI VIKWAZO LUKUKI