Tafadhali soma hapa.....

Tafadhali soma hapa.....

usiogope, usifaidhaike.. Mwenyezi Mungu atakulinda na operation itamalizika salama.

uwe na imani, yeye ni muweza wa kila jambo.
 
Kuwa na moyo wa uvumilivu na ujasiri..miili yetu sio mawe, ina uhai. Nakuombea kwa Mungu akutie nguvu na upone haraka kidonda cha OP
 
Mungu akupe ujasiri mpendwa usiruhusu mawazo mabaya, kila la kheri
 
Pole sana Mungu ni mwenye uweza utapona usiwe na wasi wasi
 
Habari za asubuhi wana MMU,
Muda mfupi ujao nitakuwa nikiingia chumba cha upasuaji,nasumbuliwa na uvimbe kwenye utumbo mpana.

Tafadhali naombeni maombi yenu wana MMU wote mwenyezi Mungu awe nami,maneno yenu ni faraja na uponyaji tosha kwangu.
Mungu awabariki.

Nakuombea Dua'a kwa Allah akupe Takhafifu na uponyi wa haraka...Bila kuhisi maumivu hata adhaa yyote.
Utakuwa mzima wa AFYA. amin
Furahiya neema ya uhai wako.
 
in the name of JESUS CHRIST SON OF GOD ALIVE i bring to you our pal Evelenk to you for better treatment AMEN.
 
Last edited by a moderator:
Mungu muweza wa yote atasimamia oprshni yako na kukuponesha haraka ktk jina la yesu kristo, Amina.
 
mtoa mada pole sana na Mungu atakuafu usijali sana manake imeandikwa katika isaya"alichubuliwa kwa makosa yetu alijeruhiwa kwa maovu yetu adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake na kwa kupigwa kwake sisi tumepona"

katika zab 16:8-11 inasema '' nimemweka bwana mbele yangu daima kwakua yuko kuumeni kwangu sitaondoshwa maana moyo wangu unafurahia nao utukufu wangu unashangilia nao mwili wangui utakaa kwa kutumaini maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, wala hutamtoa mtakatifu wako auone uharibifu.....................mbele za uso wako mna furaha tele na katika mkono wako wa kuume mna mema ya milele''
 
Uwe na moyo mkuu usiogope wala usifadhaike kwa kuwa Mimi nipo pamoja nawe nitakutia nguvu asema bwana wa majeshi.kama wewe ni mkristo ukitoka salama soma zaburi 40.1-5
 
Mungu wa Ibrahimu akupe nguvu na kupona haraka ,Amina.
Asanteni sana kwa dua na sala zenu na sasa ndo naingia chumba cha upasuaji,nimefarijika sana na kujiona niko kama na watu maelfu ,kwa kweli mmenipa moyo sana maana nilikuwa very stressed. Mungu awabariki sana na muendelee kuniombea.
 
Nawashukuru sana kwa Maombi yenu,operation ilienda vizur kabisa na nimeruhusiwa kutoka hospital sasa niko nyumbani nikijiuguza kidonda, Namshukuru Mungu kwa uzima alionipatia hakika ni mwema na kama mlivyoomba hakika alinipatia wepesi sana na ninaendelea vizuri sana.

MUNGU AWABARIKI SANA hakika mlinitia moyo sina lugha nzuri ya kuongea ila Mwenyezi Mungu awakumbuke katika kila mnalolihitaji.

Nokia83 utafiti Kongosho mdesi Blue G Magembeh miss chagga mwekundu Dannycage Leomimi Evelyn Salt Eiyer mpuko badiebey The Boss shahnaz Ennie NAMTUMBA Mbimbinho Straight corner magombe junior kijani11 Khantwe(samahan kwa kukuita kaka) Daddo google helper xiexie mtzmweusi LexAid Kichwa Ndio Mtu ng'wana ong'wa kulwa NI MTAZAMO TU neggirl Sizinga enhance miss neddy Ablessed Zamiluni Zamiluni thinky ndiga usiniguse gfsonwin na hips.com(mistari mliyonipatia ilinipa nguvu sana)
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru kwa mrejesho baada ya operesheni...upone sasa turudi kulijenga taifa.
 
Shukran sana kwa mrejesho everlenk Mwenyezi Mungu akuponye kidonda haraka uwe mzima na uendelee na kazi zako soon
 
Last edited by a moderator:
Mungu wa mbinguni akuinue, azikumbuke sadaka zako zote na kuzitakabali akuletee msaada kutoka patakatifu pake, akujibu siku ya tabu akupe haja ya moyo wako na kuyatimiza mahitaji yako yote,.
 
Back
Top Bottom