Tafadhali Serikali uzeni mahindi Kenya, sio unga

Tafadhali Serikali uzeni mahindi Kenya, sio unga

Chonde chonde jamani! Bei ya unga wa sembe itakuja kufika sh2000+ hapa tuje tutafute mchawi ni nani?

Biashara ya kuexport bidhaa nje inataka tujipange katika uzalishaji na kudhibiti kiwango cha matumizi ya ndani itosheleze bila ya kumuathiri mlaji kutokana na mripuko wa bei. Tanzania bado hatijajipanga uzalishaji wa ku export na tukilazimisha kutakuwa na mripuko wa bei na tushindwe kumiliki hata mlo mmoja kwa siku


Hata kidogo ndugu kwani hujasikia, "necessity is the mother of invention" ---- mahitaji yanapopanda ndipo watu watalima sana kukidhi soko, soko na mahitaji vinaenda sambamba, usiwe na khofu ya kupanda kwa bei ya mahindi.
 
Kukiwa na ukosefu wa mahindi na BWI ikawa juu v
Sio kwenye staple food kaka yangu, tutakuja kutafuta mchawi nani. Ulimaji wenyewe huu wa jembe la mkono 80%?
Kuneemeka kwa wakulima ndiyo tunakotaka.
vijana wote watatoka mjini wataenda vijijini kuchangamkia fursa ya kulima mahindi
 
kuna biashara kubwa ya kuuza pumba nchi jirani kwa ajili ya chakula cha mifugo unapouza mahindi unazuia fursa nyingine
 
Lete data kwamba tuna scarcity

Kaa usubiri data za mwenda mwendo wa jongoo basi wakati sisi tushafanya risk assessment na tushagundua tatizo litakalowakumba wananchi na kusababisha mripuko wa bei za bidhaa za vyakula
 
Mwaka huu tuna surplus ya tani 3 miloni ya mahindi. Hakuna haja ya kuweka vikwazo vya kuuza unga badala ya mahindi. Kenyatta amejitahidi kuwa Jirani mwema kwa kutupa kipaumbele kununua mazao yetu. Kwa masharti haya Kenya ataleta mahindi ya Mexico na sisi mahindi yatapungua bei toka 50,000 hadi 30, 000. Ni mkakati serikali haiwezi kukubali tuingie uchaguzi na inflation kubwa. Mbona 2016 esrikali iliruhusu bei ya mahindi ikafika 120,000 kwa gunia na watu walipolalamika akasema kama mnaona kilimo ni rahisi acheni ajira mkalime, Leo amgeuka? .Mkulima kwa kupangiwa pato LA jasho lake ni ukandamizaji . Waache demand and supply ifanye Kazi, hapo ndipo uzalishaji utaongezka . kama gunia likiuzwa 120,000 itachukuaiaka 3 vijana wengi wstahamia shambani na uzalishaji utapanda.. Protectionism kwenye business haijawahi kutoa matunda bora kuongeza uzalishaji. Tz ina uwezokuzalishahata tani 30 Milioni , ikiwa Vietnam anazlisha tani 20 mln ya mpunga na INA size hata nusu haitufikii. Tungeruhusu mahindi ya ziada kuuzwa nje mwaka huu tungepata hata dola 600 Milioni na ingestabilize shilingi yetu. Lakini kupanga ni kuchagua, tumchagua tule tuvimbiwe kilkibaki kiozee ghalani kama korosho. Hapo ndio jeuri ya madaraka inapotamalaki kwa kumpangia kila MTU ataishije.
 
Sio kwenye staple food kaka yangu, tutakuja kutafuta mchawi nani. Ulimaji wenyewe huu wa jembe la mkono 80%? Kuneemeka wakulima ndivo tunavotaka.
Kwaiyo unataka uneemeke wewe sisi tunaolima tuchakae
 
Yaani unataka tuuze malighafi nje??
Lengo hapa ni kuuza kwa bei nzuri ili wakulima waone kazi ya kilimo ina tija, na bei itatokana na mwitikio wa soko, sio vikwazo. Kilimo kitaimarika kutokana na nguvu ya soko la mazao yao
 
Kwaiyo unataka uneemeke wewe sisi tunaolima tuchakae
Sijasema wakulima muchakae, ninachosema ni kuwa kuwe na sera maalumu ya uzalishaji kwa ajili ya export.

Jaalia madaktari na wao wakaamua kwenda kufanya kazi Kenya, tutatibiwa na nani, au hutaki na wao waneemeke?
 
Wakulima wa mahindi wanapenda wapate soko la mazao yao. Ila iwapo kutakuwa na vikwazo vingi kama lazima mauzo ya nje yawe unga, ushuru na tozo mbali mbali, matokeo yake, biashara ya nje itashindikana, hivyo kukosa soko jumla, mnatuumiza sana.

Ni kwanini ulazimishe unga, kama wao wanapenda kande inakuwaje. Pia ifahamike, unga unaharibika mapema kuliko mahindi, Mahindi yataendelea kulimwa kwa wingi tu, iwapo yataendelea kupata soko la uhakika.

Kwa kweli sijui kwa nini hamjifunzi makosa ya kuingilia mazao kama kwanye korosho, hadi leo baadhi ya watu hawalipwa korosho, na hata waliosafirisha korosho kutoka vyama vya msingi hadi maghala ya mnada baadhi wamepata malipo theluthi ya madai yao.

Mimi nikiwa mkulima sipendi uingiliaji huo, na sijali habari ya misifa ya sgr, ndege, bwawa la umeme wala elimu bure, na nawaangalia tu akina Mpoto misifa kibao, sisi huku sijui kwanini na asimwambie atulipe ndio aendelee na sifa zake.
Pumba afaidike nazo nani.Tuna mifugo mingi kuliko kenya.
 
Good point. Kulazimisha wakenya wanunue unga badala ya mahindi, huo ni Ubeberu.
Pia hii inamnyonya mkulima. Mkulima akiuza mahindi kwenye soko la nje hupata pesa mingi kuliko akiuza mahindi kwenye viwanda ambavyo husaga unga na ku export.
Kitu ambacho umeshindwa Kuelewa ni kwamba,
Muuzaji wa Mahindi Kenya ni Serikali na sio Mtu Binafsi...

Kawaida ya Serikali huwa inauza bidhaa iliyoongezwa Thamani ili Faida Iwe ya Kutosha na wananchi walipwe hela ya kutosha...

Badala ya debe Moja kuuza 8,000/- sasa Unaweza kuta litauzwa Mpaka zaid ya 12,000/- na unga wa 25Kg utauzwa zaid ya 30,000/- Kenya

Kwa sasa Kenya Unga unauzwa 130KShs sawa na 2,900/- TZS

Tunataka kuuza Goods na sio raw materials...

Ikumbukwe kuwa chakula kikuu Kenya ni Ugali Kama ilivyo Tanzania na Uganda
 
Kitu ambacho umeshindwa Kuelewa ni kwamba,
Muuzaji wa Mahindi Kenya ni Serikali na sio Mtu Binafsi...

Kawaida ya Serikali huwa inauza bidhaa iliyoongezwa Thamani ili Faida Iwe ya Kutosha na wananchi walipwe hela ya kutosha...

Badala ya debe Moja kuuza 8,000/- sasa Unaweza kuta litauzwa Mpaka zaid ya 12,000/- na unga wa 25Kg utauzwa zaid ya 30,000/- Kenya

Kwa sasa Kenya Unga unauzwa 130KShs sawa na 2,900/- TZS

Tunataka kuuza Goods na sio raw materials...

Ikumbukwe kuwa chakula kikuu Kenya ni Ugali Kama ilivyo Tanzania na Uganda
Wakulima wa mahindi wanapenda wapate soko la mazao yao. Ila iwapo kutakuwa na vikwazo vingi kama lazima mauzo ya nje yawe unga, ushuru na tozo mbali mbali, matokeo yake, biashara ya nje itashindikana, hivyo kukosa soko jumla, mnatuumiza sana.

Ni kwanini ulazimishe unga, kama wao wanapenda kande inakuwaje. Pia ifahamike, unga unaharibika mapema kuliko mahindi, Mahindi yataendelea kulimwa kwa wingi tu, iwapo yataendelea kupata soko la uhakika.

Kwa kweli sijui kwa nini hamjifunzi makosa ya kuingilia mazao kama kwanye korosho, hadi leo baadhi ya watu hawalipwa korosho, na hata waliosafirisha korosho kutoka vyama vya msingi hadi maghala ya mnada baadhi wamepata malipo theluthi ya madai yao.

Mimi nikiwa mkulima sipendi uingiliaji huo, na sijali habari ya misifa ya sgr, ndege, bwawa la umeme wala elimu bure, na nawaangalia tu akina Mpoto misifa kibao, sisi huku sijui kwanini na asimwambie atulipe ndio aendelee na sifa zake.
 
UZA UNGA ,
HAKUNA KUUZA MAHINDI,UKIUZA MAHINDI UNASABABISHA MFUMUKO WA BEI YA UNGA NDANI YA NCHI KWANZA WALISEMA MAHINDI YETU MACHAFU.
 
Kitu ambacho umeshindwa Kuelewa ni kwamba,
Muuzaji wa Mahindi Kenya ni Serikali na sio Mtu Binafsi...

Kawaida ya Serikali huwa inauza bidhaa iliyoongezwa Thamani ili Faida Iwe ya Kutosha na wananchi walipwe hela ya kutosha...

Badala ya debe Moja kuuza 8,000/- sasa Unaweza kuta litauzwa Mpaka zaid ya 12,000/- na unga wa 25Kg utauzwa zaid ya 30,000/- Kenya

Kwa sasa Kenya Unga unauzwa 130KShs sawa na 2,900/- TZS

Tunataka kuuza Goods na sio raw materials...

Ikumbukwe kuwa chakula kikuu Kenya ni Ugali Kama ilivyo Tanzania na Uganda
Pia nawe unashindwa kuelewa hayo mahindi huwa yanalalia kila mwaka, na mwisho wake ununuliwa na wajanja kama chakula cha mifugo.
Uzeni mahindi acheni kiburi kutojali, mara ngapi Tanzania tumepokea mahindi toka nje. Ya Zimbabwe, kumbuka miaka ya 70 ugali wa yanga, tafuteni faida kwingine kinguvu sio kwenye chakula.
 
Kitu ambacho umeshindwa Kuelewa ni kwamba,
Kitu ambacho nilishindwa kuelewa ni kwamba, badala ya mkulima aliyeko Kiteto- Manyara kuuza mahindi yake Kenya yakavuka border ya Namanga, hayo mahindi itabidi yaletwe mpaka Dar kwenye viwanda vya kusagia unga, then yasafirishwe tena mpaka Namanga ili kuvuka border which will add to the costs. Na pia kuuza unga Kenya utaongeza demand ya unga kwa kuwa local market itakuwa ina compete na export market kitu ambacho kitachangia kuongezeka kwa bei ya unga kwa soko la ndani.
Kenya watapata unga kwa bei kubwa zaidi kutokana na hasa kuongezeka kwa transportation cost na pia wananchi wa Tz watapata unga kwa bei ya juu zaidi kutokana na kuongezeka kwa demand. So in the end itakuwa ni lose lose situation.
 
UZA UNGA ,
HAKUNA KUUZA MAHINDI,UKIUZA MAHINDI UNASABABISHA MFUMUKO WA BEI YA UNGA NDANI YA NCHI KWANZA WALISEMA MAHINDI YETU MACHAFU.
Hapa naona una kisasi kisicho isha, kauli hizo kwa wakati huo ni sahihi, na kauli yao ya leo kwa leo ni sahihi pia. Angalia biashara sio kauli.
 
Nakumbuka mwaka juzi kuna jamaa alinishawishi kulima mahindi yanalipa mzee nikaingia shambani poteza gharama kibao,kuja kuvuna naambiwa mahindi yameshuka baada ya kuzuiwa kutoka kuuzwa nje so gunia ilikuwa elf17 Yani na gharama nilizotumia nikipiga hesabu hata robo yake sifikishi kwa hela niloitumia, kwakifupi nilikata sana tamaa mpaka leo hii sijalima tena,lakini ningepata faida nilipanga kuongeza kutoka heka5 nillizoanza mpaka 10 na kuendelea na iwe ndo shufhuli yangu rasmi lakin nilichokutana nacho sina hamu.
 
Back
Top Bottom