Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,672
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 24
“Patrick! Patrick! Patrick!” Nancy aliendelea kuita huku akiukimbiza msururu wa magari ulizidi kusogea mbele kuingia barabara ya Morogoro kutoka viwanja vya Jangwani, alilipita kila gari akiita jina la kaka yake lakini hakuitikiwa! Nancy alichanganyikiwa na kushindwa kuelewa ni wapi Patrick alikokuwa.
“Dada vipi mbona unahangaika?”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Namtafuta kaka yangu Patrick!”
“Patrick gani?”
“Aliyetangazwa jukwaani kama msaidizi wa Mwinjilisti Heinz! Nimepotezana naye siku nyingi na niliamini alishakufa!”
“Unamwongelea kijana aliyetambulishwa na Mwinjilisti?”
“Ndiyo!”
“Njoo nikuonyesha gari alilipanda!” Kijana huyo alimshika Nancy mkono na kuanza kumvuta kuelekea mbele ulikoelekea msafara wa magari.
Walipokaribia mwanzo wa msafara huo, kijana alijishika kichwani na kuonyesha masikitiko makubwa huku akimwangalia Nancy usoni.
“Nini?” Nancy aliuliza.
“Gari lenyewe ndiyo lile linaloingia barabarani!” Alisema kijana huyo baada ya kuliona gari aina ya Landcruiser Vx likiingia barabara ya Morogoro na kuongeza kasi.
“Una uhakika Patrick kapanda gari hilo kaka?”
“Ndiyo na si yeye tu bali hata mtumishi wa Mungu Heinz!”
“Kweli?”Nancy aliuliza tena.
“Ndiyo!”
“Asilimia mia moja?”
“Ahsante kaka kwa msaada wako Mungu akubariki sana!”
Alisema Nancy na kuondoka mbio akikimbia kwenda mbele, hakufuata barabara ya lami bali alikimbilia bondeni kwenye nyasi akijaribu kuliwahi gari ambalo Patrick alidaiwa kupanda. Mwisho wa bonde aliingia barabarani na kuyaona magari yote yamesimama na alipoangalia mbele yake aliona taa nyekundu zikiwaka!
“Hizi nafikiri ndio taa za kuzuia magari ambazo huwa nazisikia, lazima gari lililombeba Patrick litakuwa miongoni mwa gari haya !” Aliwaza Nancy na kuanza kupepesa macho yake kuangalia magari yote yaliyokuwa katika mstari yakisubiri taa ziruhusu.
Ghafla aliliona gari alililoonyeshwa likiwa kama hatua thelathini hivi kutoka mahali aliposimama! Furaha kubwa ilijaa moyoni mwake akawa na uhakika wa kumpata kaka yake Patrick.Watu waliokuwa ndani ya magari mengine walimwona kama mtu aliyechanganyikiwa, Nancy hakujali wala kuona aibu aliendelea kuliita jina la nduguye huku akikimbia kulielekea gari!
Alipokaribia gari hilo alizisoma namba zake na kuona ndio lenyewe, akawa na uhakika zaidi ya kumpata pacha wake! Akaongeza mbio zaidi lakini hatua kama tatu hivi kabla hajaligusa gari hilo taa nyekundu zilibadilika na kuwa kijani magari yote yakaanza kuondoka kwa kasi.
“Patrick! Patrick! Patrick! Mimi dada yako niko hapa!” Alipaza sauti Nancy lakini sauti yake yake haikusikika sababu gari hilo lilifungwa vioo vyote!
Nguvu zilimwishia Nancy miguuni na kwa sababu ya kukimbia sana alijisikia mvurugiko wa tumbo na kuanza kutapika! Hakutaka kupoteza muda aliendelea kukimbia huku akitapika kuufuata msururu wa magari uliokuwa ukienda kwa kasi kubwa.
“KUUUUUUUUUU!” Ulikuwa ni mlio wa magari yaliyogonana ghafla.
“Wee mshamba utaua watu!” Kelele zilisikika kutoka ndani ya magari yaliyokuwa jirani na eneo hilo, Nancy alikuwa amekatisha barabara ghafla akikimbia, kidogo tu agongwe vibaya kama dereva asingemkwepa! Lakini katika kufanya hivyo gari lake lilikutana uso kwa uso na daladala lililokuwa likitoka upande wa pili!
Kwa hofu ya kupigwa Nancy hakusimama alizidi kukimbia mbio kwenda mbele zaidi, dereva wa daladala alichomoka kwenye usukani na kuanza kumkimbiza, hasira kali ilimshika sababu ya kuharibiwa gari lake kwa uzembe wa Nancy, hatua chache tu mbele alimtia Nancy mkononi na kuanza kumzaba vibao usoni.
“Nisamehe kaka ....mimi ni mgeni hapa mjini!” Alisema Nancy huku machozi yakimtoka.
“Ukiwa mgeni ndiyo ukatishe barabara vibaya kiasi hicho, ungekufa wewe!”
“Ahsante kwa kuokoa maisha yangu kaka, nisamehe na Mungu atakulipia gari lako!”
Dereva alimmshushia Nancy ngumi mzito usoni, iliyomfanya avimbe juu ya jicho lake, alinguka chini na kusikia kizunguzungu lakini sababu alikuwa akilikimbiza gari lililombeba Patrick alijitahidi na kunyanyuka ardhini akiwa na maumivu yake na kuendelea mbele! Watu ndani ya magari walimcheka na kumzomea, roho yake iliuma lakini hakuwa na la kufanya.
Mbele kidogo alikuta magari yote yakiwa yamesimam kama ilivyokuwa nyuma na alipotupa macho yake mbele aliyaona mataa mengine yakiwaka kwa rangi nyekundu! Alijua gari lililombeba Patrick lilikuwa miongoni mwa magari hayo, Nancy aliongeza mbio jicho lake lilimuuma lakini hakujali, alipotupa macho mbele zaidi aliliona gari lililombeba l Patrick likiwa mbele ya magari yote, akaongeza mwendo zaidi lakini kabla hajalifikia taa za kijani ziliwaka na kuyaruhusu magari kuendelea na safari.
Aliendelea kuliita jina la Patrick wakati akikimbiza gari hilo, almanusura agongwe na lori lililobeba mchanga! Roho ya Nancy ilizidi kuuma akajikuta akilia machozi zaidi.
Hakukata tamaa alizidi kulifukuza gari hilo kwa nyuma, alikuwa amechoka kukimbia lakini aliendelea kwani alipania mno kukutana na kaka yake na pacha wake Patrick na alitaka kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kuwa anazuia safari yake ya kwenda nchi za nje na Mwinjilisti Heinz ! Alijua wazi Patrick alichukua uamuzi huo baada ya kuona hakuwa na ndugu tena Tanzania.
Mbele kidogo kwenye mataa ya Lumumba na barabara ya Morogoro Nancy aliyaona magari yakisimama, alikimbia zaidi lakini hakuyawahi kwani kabla hajayafikia taa ziliruhusu na magari yakaanza kuondoka kwa kasi, Nancy alichoka na kuamua kutembea taratibu hadi kwenye makutano ya barabara za Morogoro na bibi Titi ambako aliyaona magari hayo yakikata kushoto kwa mwendo wa kasi.
Hakuweza kukimbia zaidi ikabidi atembee taratibu, mbele aliingia barabara ya Bibi Titi Mohamed, giza lilishanzaa kuingia na taa ziliwaka kila mahali, kwa msaada wa taa alifanikiwa kusoma mabango ya ofisi mbalimbali kushoto kwake, aliona bango la ofisi za Tritel na mbele kidogo kwenye mataa ya Bibi Titi na barabara ya Azikiwe aliona bango jingine lililosomeka “Maktaba ya Taifa”!
“Sasa sijui magari hayo yaliekea upande gani? Sijui yalinyoosha au yalikata kulia?” Alijiuliza Nancy baada ya kuchanganikiwa juu ya upande yalikoelekea magari ya msafara wa mwinjilisti Heinz! Baada ya kufikiri kwa muda hatimaye aliamua kukata kulia kuingia barabara ya maktaba na kunyoosha moja kwa moja hadi Posta mpya lakini hakuona dalili yoyote ya kuliona tena gari lililombeba Patrick wala magari mengine ya msafara wa Mwinjilisti Heinz!
****************
Alipofika maeneo ya Posta alishangazwa na umati wa watu wengi wakisubiri magari ya kuwarudisha majumbani kwao, alizunguka hapo kwa muda bila kuelewa aelekee wapi au amuulize nani! Ghafla alipomwona msichana mmoja akipita jirani yake, msichana huyo alikuwa na biblia mkononi mwake, Nancy alijua huo ndio ulikuwa msaada pekee kwake wakati huo alimkimbilia na kumshika bega!
“Dada yangu samahani sana kwanza shikamoo!”
“Marahaba mdogo wangu, vipi mbona unalia?’
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Ninamtafuta kaka yangu!”
“Wewe ni mgeni hapa?”
“Ndiyo!”
“Unatoka wapi?”
“Mwanza!”
“Huyo kaka yako anafanya kazi wapi?”
“Hafanyi kazi ila yupo na Mwinjilisti Heinz aliyekuwa akihubiri kwenye viwanja vya!……….vya!……..vya! Vya Jangwani!”
“Aha! Yule kafikia hoteli ya Sheraton!”
“Ipo wapi hiyo dada?”
“Pitia hapa!” Alimwonyesha barabara iliyoshuka chini kupitia makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani na makao makuu ya posta nchini Tanzania!
“Sawa!”
“Pale mbele utakutana na barabara nyingine inayokatisha, hiyo ni mtaa wa Ohio! Hapo kata kushoto mbele utaona jumba refu mkono wa kulia si unajua kusoma?”
“Ndiyo!”
“Basi hapo utaona bango lililoandikwa Sheraton, kuna magari mengi sana utayakuta, ukifika ulizia tu watakuonyesha chumba cha huyo Mwinjilisti!”
“Ahsante sana dada yangu sina namna ya kukushukuru!” Alisema Nancy na kuanza kuondoka eneo hilo mbele kidogo aliona kibao kilichoandikwa ‘Ohio street’ alikata kushoto kama alivyoelekezwa na kusonga mbele, aliliona ghorofa refu zaidi mkono wake wa kulia na kukata kona kuingia hotelini hapo.
Alishangazwa na uzuri wa hoteli hiyo na kwa jinsi alivyovaa nguo chafu alihisi asingeruhusiwa kabisa kuingia ndani ya hoteli hiyo, alijipa moyo na kusonga mbele!
“Mimi sijali hata kidogo ili mradi tu nimwone Patrick!” Alijisemea Nancy akielekea geti la hoteli hiyo.
Tayari ilishatimua saa tatu ya usiku, Nancy alitembea bila kujiamini alipolifikia lango la kuingilia hotelini askari wa ulinzi alimsimamisha.
“wee changu unakwenda wapi?”
“Mh! Unasemaje kaka yangu?”
“Nakuuliza unakwenda wapi saa hizi?”
“Humu hotelini!”
“Hapana! Utawala wa hoteli umezuia kabisa nyinyi msiingie humu ndani wateja wenu wawakute hukohuko mtaani!” Alisema askari na kuanza kumsukuma Nancy kumtoa nje ya hoteli hiyo.
“Kaka sikuelewi?”
“Kama hunielewi basi shauri yako kafanyie umalaya wako nje!”
“Umalaya? Kwa umri huu mdogo niwe malaya, tafadhali nisikilize kaka yangu nikusimulie shida yangu!”
“Hakuna! Sitakii! Toka nje!” Alisema askari huyo akimsukuma Nancy kumtoa nje na kulifunga lango nyuma yake.
Nje Nancy aliendelea kulia akiligonga lango hilo, ilikuwa si rahisi kuamini kuwa kaka yake na pacha wake Patrick alikuwa ndani ya hoteli hiyo lakini alizuiliwa kumwona, alilia kwa uchungu na kuendelea kuligonga lango!
“Nifungulieni jamani! Nifungulieni, nimwone kaka yangu!”
“Kaka yako gani malaya wewe, toka hapa na nikitoka huko nje utanitambua!”
Nancy hakusikia onyo hilo la askari aliendelea kulia akibisha hodi mlangoni, mlinzi alitafsiri hiyo kama dharau na kuamua kutoka hadi nje ambako alimkuta Nancy na kumbeba juu juu hadi barabarani ambako alimbwaga chini na kurudi ndani ya hoteli.
Muda mfupi akiwa chini kundi la wasichana waliovaa nguo fupi na wengine wakiwa na chupi peke yake walimvamia, Nancy alitetemeka akifikiri labda wasichana wale walikuwa wachawi!
“Mdogo wetu vipi, umetoa huduma wamekudhulumu nini? Maana hapa kuna wazungu wadhulumati ile mbaya!”
Nancy alizidi kuwaangalia kwa mshangao hakuelewa kitu walichokua wakimweleza, aliendelea kulia machozi, kabla hajawaeleza kilichotokea walishtukia magari mawili aina ya Landrover yakiegesha pembeni yao, wasichana wengine wote walitimukia porini na kuwaacha Nancy na msichana mwingine mmoja ambao walijikuta mikononi mwa polisi, walifungwa pingu na kutupwa nyuma ya gari ambako walikutana na askari mwenye virungu, aliyekitumia vizuri kirungu chake juu ya vichwa vyao! Nancy alilia kupita kiasi.
“Nyie malaya tumeshawaeleza msikae mtaa huu wanapita viongozi hamsikii siyo?” Askari alisema huku akiendelea kuwagonga na virungu vichwani, kama wewe mtoto mdogo kabisa unafanya umalaya.
“Mimi siyo……!” Nancy alijaribu kujieleza lakini kabla sentensi yake haijafikia mwisho kirungu kilitua juu ya pua yake na damu zilianza kutoka puani.
“Kimya! Funga domo lako changu wee unafikiri mimi nataka mapenzi hapa?” Alifoka askari huyo.
Kwa upande wake Nancy aliamini kama angepewa nafasi ya kujieleza askari huyu angeweza kumwachia huru lakini nafasi hiyo haikuwepo.
Walipofikishwa kituoni walitupwa mahabusu bila hata kutoa maelezo, kila mtu aliwaita malaya wazururaji, majina hayo yalimuuma sana Nancy ukizingatia katika maisha yake hakuwahi hata mara moja kukutana na mwanaume kimapenzi.
“Ninaitwa Lwina! Sijui mwenzangu unaitwa nani?” Changudoa waliyekamatwa nae alimuuliza, Nancy hakujibu aliendelea kulia machozi ya uchungu mambo yalikuwa yakitokea katika maisha yake yalimsikitisha kupita kiasi, hata siku moja katika maisha yake hakuwahi kufikiria kuwa angeweza kuitwa malaya!
“Unaitwa nani?”msichana yule aliuliza tena.
“Mimi naitwa N….a..n…cy!” Alijibu huku akilia machozi.
“Jina lako zuri sana wewe huwa unasimama kiwanja gani? Sababu kiwanja cha Ohio ndio kwanza nimekuona leo? Huwa upo Kinondoni au Las Vegas nini?”
“Hapana!”
“Oysterbay?”
“Viwanja vya nini dada?”
************
Kidubo na mke wake mama Teddy walimtafuta Nancy kwenye mkutano bila mafanikio, walishaamua kuishi naye nyumbani kwao mpaka mama yake amalize kifungo cha miaka mitano, walijua Nancy alikuwa na matatizo na alihitaji msaada mkubwa na waliamini msaada huu ulikuwa mikononi mwao.
Watu wote kwenye mkutano walisambaa bila Nancy kuonekana, ndipo walipoamua kuzunguka huku na kule jijini wakimtafuta bila mafanikio mwisho walikata tamaa na kuamua kuondoka kurejea nyumbani kwao Segerea.
“Si ajabu amekutana na kaka yake na kuamua kuondoka naye!” Kidubo alimwambia mke wake.
“Inawezekana!” Mkewe aliitikia.
“Basi tena Mungu anajua!”
Walirejea nyumbani wakiwa na masikitiko makubwa mno kumpoteza Nancy Moyoni mwao walishampenda sana Nancy na walitaka kumsaidia!
****************
Mpaka usiku wa manane ndani ya hoteli ya Sheraton wakiwa wamelala chumba kimoja na Mwinjilisti Heinz, Patrick alikuwa bado hajapata usingizi akiyafikiria maisha yake! Hakuamini yote yaliyomtokea katika maisha yake, kukutana na mzungu na kukubali kumsaidia hakikuwa kitu alichowahi kukifikiria maishani mwake.
Pamoja na mawazo hayo yote bado aliendelea kuwafikiria mama na dada yake Nancy ambao aliamini walikuwa wafu! Hakuwa na taarifa yoyote kuwa usiku huo Nancy alishakuja hadi nje ya hoteli ya Sheraton akimtafuta! Mawazo juu ya mama na dada yake yalimfanya atokwe na machozi.
Ghafla alishtukia akimwona Mwinjilisti Heinz akinyanyuka kitandani kwake na kwenda kwenye moja ya masanduku yake na kulifungua akatoa kitu kama bomba la sindano na chupa ya dawa fulani! Alitupa macho yake kuangalia kwenye kitanda cha Patrick, Patrick aliamua kujifanya amelala ili ajue ni kitu gani kilichotaka kutokea, Mwinjilisti alisogea hadi karibu kabisa na kitanda cha Patrick na kumchunguza usoni.
“He is fully asleep!”(amelala fofofo)Mwinjilisti alisema peke yake na kuondoka.
Patrick alishuhudia kila kitu kutoka kwenye kona ya jicho lake la kushoto alimwona Mwinjilisti akihangaika kujifunga na mpira wa plastiki na kujipigapiga, alionekana kama mtu aliyekuwa akitafuta mishipa wa damu mikononi mwake. Alionekana kutofanikiwa ndipo alipochukua mpira huo na kuufunga sehemu za siri kwenye uume wake! Kwa macho yake yote mawili Patrick alishuhudia Mwinjilisti akichoma sindano ndani ya uume wake! Alilegea na kuanza kulala hapohapo sakafuni.
Patrick aliogopa na kunyanyuka kitandani kwake kumkimbilia Mwinjilisti, akidhani labda madawa aliyojichoma yalimzidi.
“Mtumishi! Mtumishi! Mtumishi wa Mungu Heinz!” Patrick aliita lakini Mwinjilisti hakuitikia aliendelea kukoroma na kudondosha udelele mdomoni kwake.
Patrick alimnyanyua na kumpandisha Mwinjilisti kitandani huku akitetemeka, alifikiria kupiga simu mapokezi ili waje wampe msaada!
Patrick ameshuhudia mambo ya Mwinjilisti Heinz ambayo ni siri kubwa na Mwinjilisti humuua mtu yeyote agunduaye siri hiyo!
Je nini kitampata Patrick?
Nancy yupo mahabusu akidhaniwa ni changudoa!
Je nini kinafuata?
“Patrick! Patrick! Patrick!” Nancy aliendelea kuita huku akiukimbiza msururu wa magari ulizidi kusogea mbele kuingia barabara ya Morogoro kutoka viwanja vya Jangwani, alilipita kila gari akiita jina la kaka yake lakini hakuitikiwa! Nancy alichanganyikiwa na kushindwa kuelewa ni wapi Patrick alikokuwa.
“Dada vipi mbona unahangaika?”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Namtafuta kaka yangu Patrick!”
“Patrick gani?”
“Aliyetangazwa jukwaani kama msaidizi wa Mwinjilisti Heinz! Nimepotezana naye siku nyingi na niliamini alishakufa!”
“Unamwongelea kijana aliyetambulishwa na Mwinjilisti?”
“Ndiyo!”
“Njoo nikuonyesha gari alilipanda!” Kijana huyo alimshika Nancy mkono na kuanza kumvuta kuelekea mbele ulikoelekea msafara wa magari.
Walipokaribia mwanzo wa msafara huo, kijana alijishika kichwani na kuonyesha masikitiko makubwa huku akimwangalia Nancy usoni.
“Nini?” Nancy aliuliza.
“Gari lenyewe ndiyo lile linaloingia barabarani!” Alisema kijana huyo baada ya kuliona gari aina ya Landcruiser Vx likiingia barabara ya Morogoro na kuongeza kasi.
“Una uhakika Patrick kapanda gari hilo kaka?”
“Ndiyo na si yeye tu bali hata mtumishi wa Mungu Heinz!”
“Kweli?”Nancy aliuliza tena.
“Ndiyo!”
“Asilimia mia moja?”
“Ahsante kaka kwa msaada wako Mungu akubariki sana!”
Alisema Nancy na kuondoka mbio akikimbia kwenda mbele, hakufuata barabara ya lami bali alikimbilia bondeni kwenye nyasi akijaribu kuliwahi gari ambalo Patrick alidaiwa kupanda. Mwisho wa bonde aliingia barabarani na kuyaona magari yote yamesimama na alipoangalia mbele yake aliona taa nyekundu zikiwaka!
“Hizi nafikiri ndio taa za kuzuia magari ambazo huwa nazisikia, lazima gari lililombeba Patrick litakuwa miongoni mwa gari haya !” Aliwaza Nancy na kuanza kupepesa macho yake kuangalia magari yote yaliyokuwa katika mstari yakisubiri taa ziruhusu.
Ghafla aliliona gari alililoonyeshwa likiwa kama hatua thelathini hivi kutoka mahali aliposimama! Furaha kubwa ilijaa moyoni mwake akawa na uhakika wa kumpata kaka yake Patrick.Watu waliokuwa ndani ya magari mengine walimwona kama mtu aliyechanganyikiwa, Nancy hakujali wala kuona aibu aliendelea kuliita jina la nduguye huku akikimbia kulielekea gari!
Alipokaribia gari hilo alizisoma namba zake na kuona ndio lenyewe, akawa na uhakika zaidi ya kumpata pacha wake! Akaongeza mbio zaidi lakini hatua kama tatu hivi kabla hajaligusa gari hilo taa nyekundu zilibadilika na kuwa kijani magari yote yakaanza kuondoka kwa kasi.
“Patrick! Patrick! Patrick! Mimi dada yako niko hapa!” Alipaza sauti Nancy lakini sauti yake yake haikusikika sababu gari hilo lilifungwa vioo vyote!
Nguvu zilimwishia Nancy miguuni na kwa sababu ya kukimbia sana alijisikia mvurugiko wa tumbo na kuanza kutapika! Hakutaka kupoteza muda aliendelea kukimbia huku akitapika kuufuata msururu wa magari uliokuwa ukienda kwa kasi kubwa.
“KUUUUUUUUUU!” Ulikuwa ni mlio wa magari yaliyogonana ghafla.
“Wee mshamba utaua watu!” Kelele zilisikika kutoka ndani ya magari yaliyokuwa jirani na eneo hilo, Nancy alikuwa amekatisha barabara ghafla akikimbia, kidogo tu agongwe vibaya kama dereva asingemkwepa! Lakini katika kufanya hivyo gari lake lilikutana uso kwa uso na daladala lililokuwa likitoka upande wa pili!
Kwa hofu ya kupigwa Nancy hakusimama alizidi kukimbia mbio kwenda mbele zaidi, dereva wa daladala alichomoka kwenye usukani na kuanza kumkimbiza, hasira kali ilimshika sababu ya kuharibiwa gari lake kwa uzembe wa Nancy, hatua chache tu mbele alimtia Nancy mkononi na kuanza kumzaba vibao usoni.
“Nisamehe kaka ....mimi ni mgeni hapa mjini!” Alisema Nancy huku machozi yakimtoka.
“Ukiwa mgeni ndiyo ukatishe barabara vibaya kiasi hicho, ungekufa wewe!”
“Ahsante kwa kuokoa maisha yangu kaka, nisamehe na Mungu atakulipia gari lako!”
Dereva alimmshushia Nancy ngumi mzito usoni, iliyomfanya avimbe juu ya jicho lake, alinguka chini na kusikia kizunguzungu lakini sababu alikuwa akilikimbiza gari lililombeba Patrick alijitahidi na kunyanyuka ardhini akiwa na maumivu yake na kuendelea mbele! Watu ndani ya magari walimcheka na kumzomea, roho yake iliuma lakini hakuwa na la kufanya.
Mbele kidogo alikuta magari yote yakiwa yamesimam kama ilivyokuwa nyuma na alipotupa macho yake mbele aliyaona mataa mengine yakiwaka kwa rangi nyekundu! Alijua gari lililombeba Patrick lilikuwa miongoni mwa magari hayo, Nancy aliongeza mbio jicho lake lilimuuma lakini hakujali, alipotupa macho mbele zaidi aliliona gari lililombeba l Patrick likiwa mbele ya magari yote, akaongeza mwendo zaidi lakini kabla hajalifikia taa za kijani ziliwaka na kuyaruhusu magari kuendelea na safari.
Aliendelea kuliita jina la Patrick wakati akikimbiza gari hilo, almanusura agongwe na lori lililobeba mchanga! Roho ya Nancy ilizidi kuuma akajikuta akilia machozi zaidi.
Hakukata tamaa alizidi kulifukuza gari hilo kwa nyuma, alikuwa amechoka kukimbia lakini aliendelea kwani alipania mno kukutana na kaka yake na pacha wake Patrick na alitaka kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kuwa anazuia safari yake ya kwenda nchi za nje na Mwinjilisti Heinz ! Alijua wazi Patrick alichukua uamuzi huo baada ya kuona hakuwa na ndugu tena Tanzania.
Mbele kidogo kwenye mataa ya Lumumba na barabara ya Morogoro Nancy aliyaona magari yakisimama, alikimbia zaidi lakini hakuyawahi kwani kabla hajayafikia taa ziliruhusu na magari yakaanza kuondoka kwa kasi, Nancy alichoka na kuamua kutembea taratibu hadi kwenye makutano ya barabara za Morogoro na bibi Titi ambako aliyaona magari hayo yakikata kushoto kwa mwendo wa kasi.
Hakuweza kukimbia zaidi ikabidi atembee taratibu, mbele aliingia barabara ya Bibi Titi Mohamed, giza lilishanzaa kuingia na taa ziliwaka kila mahali, kwa msaada wa taa alifanikiwa kusoma mabango ya ofisi mbalimbali kushoto kwake, aliona bango la ofisi za Tritel na mbele kidogo kwenye mataa ya Bibi Titi na barabara ya Azikiwe aliona bango jingine lililosomeka “Maktaba ya Taifa”!
“Sasa sijui magari hayo yaliekea upande gani? Sijui yalinyoosha au yalikata kulia?” Alijiuliza Nancy baada ya kuchanganikiwa juu ya upande yalikoelekea magari ya msafara wa mwinjilisti Heinz! Baada ya kufikiri kwa muda hatimaye aliamua kukata kulia kuingia barabara ya maktaba na kunyoosha moja kwa moja hadi Posta mpya lakini hakuona dalili yoyote ya kuliona tena gari lililombeba Patrick wala magari mengine ya msafara wa Mwinjilisti Heinz!
****************
Alipofika maeneo ya Posta alishangazwa na umati wa watu wengi wakisubiri magari ya kuwarudisha majumbani kwao, alizunguka hapo kwa muda bila kuelewa aelekee wapi au amuulize nani! Ghafla alipomwona msichana mmoja akipita jirani yake, msichana huyo alikuwa na biblia mkononi mwake, Nancy alijua huo ndio ulikuwa msaada pekee kwake wakati huo alimkimbilia na kumshika bega!
“Dada yangu samahani sana kwanza shikamoo!”
“Marahaba mdogo wangu, vipi mbona unalia?’
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Ninamtafuta kaka yangu!”
“Wewe ni mgeni hapa?”
“Ndiyo!”
“Unatoka wapi?”
“Mwanza!”
“Huyo kaka yako anafanya kazi wapi?”
“Hafanyi kazi ila yupo na Mwinjilisti Heinz aliyekuwa akihubiri kwenye viwanja vya!……….vya!……..vya! Vya Jangwani!”
“Aha! Yule kafikia hoteli ya Sheraton!”
“Ipo wapi hiyo dada?”
“Pitia hapa!” Alimwonyesha barabara iliyoshuka chini kupitia makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani na makao makuu ya posta nchini Tanzania!
“Sawa!”
“Pale mbele utakutana na barabara nyingine inayokatisha, hiyo ni mtaa wa Ohio! Hapo kata kushoto mbele utaona jumba refu mkono wa kulia si unajua kusoma?”
“Ndiyo!”
“Basi hapo utaona bango lililoandikwa Sheraton, kuna magari mengi sana utayakuta, ukifika ulizia tu watakuonyesha chumba cha huyo Mwinjilisti!”
“Ahsante sana dada yangu sina namna ya kukushukuru!” Alisema Nancy na kuanza kuondoka eneo hilo mbele kidogo aliona kibao kilichoandikwa ‘Ohio street’ alikata kushoto kama alivyoelekezwa na kusonga mbele, aliliona ghorofa refu zaidi mkono wake wa kulia na kukata kona kuingia hotelini hapo.
Alishangazwa na uzuri wa hoteli hiyo na kwa jinsi alivyovaa nguo chafu alihisi asingeruhusiwa kabisa kuingia ndani ya hoteli hiyo, alijipa moyo na kusonga mbele!
“Mimi sijali hata kidogo ili mradi tu nimwone Patrick!” Alijisemea Nancy akielekea geti la hoteli hiyo.
Tayari ilishatimua saa tatu ya usiku, Nancy alitembea bila kujiamini alipolifikia lango la kuingilia hotelini askari wa ulinzi alimsimamisha.
“wee changu unakwenda wapi?”
“Mh! Unasemaje kaka yangu?”
“Nakuuliza unakwenda wapi saa hizi?”
“Humu hotelini!”
“Hapana! Utawala wa hoteli umezuia kabisa nyinyi msiingie humu ndani wateja wenu wawakute hukohuko mtaani!” Alisema askari na kuanza kumsukuma Nancy kumtoa nje ya hoteli hiyo.
“Kaka sikuelewi?”
“Kama hunielewi basi shauri yako kafanyie umalaya wako nje!”
“Umalaya? Kwa umri huu mdogo niwe malaya, tafadhali nisikilize kaka yangu nikusimulie shida yangu!”
“Hakuna! Sitakii! Toka nje!” Alisema askari huyo akimsukuma Nancy kumtoa nje na kulifunga lango nyuma yake.
Nje Nancy aliendelea kulia akiligonga lango hilo, ilikuwa si rahisi kuamini kuwa kaka yake na pacha wake Patrick alikuwa ndani ya hoteli hiyo lakini alizuiliwa kumwona, alilia kwa uchungu na kuendelea kuligonga lango!
“Nifungulieni jamani! Nifungulieni, nimwone kaka yangu!”
“Kaka yako gani malaya wewe, toka hapa na nikitoka huko nje utanitambua!”
Nancy hakusikia onyo hilo la askari aliendelea kulia akibisha hodi mlangoni, mlinzi alitafsiri hiyo kama dharau na kuamua kutoka hadi nje ambako alimkuta Nancy na kumbeba juu juu hadi barabarani ambako alimbwaga chini na kurudi ndani ya hoteli.
Muda mfupi akiwa chini kundi la wasichana waliovaa nguo fupi na wengine wakiwa na chupi peke yake walimvamia, Nancy alitetemeka akifikiri labda wasichana wale walikuwa wachawi!
“Mdogo wetu vipi, umetoa huduma wamekudhulumu nini? Maana hapa kuna wazungu wadhulumati ile mbaya!”
Nancy alizidi kuwaangalia kwa mshangao hakuelewa kitu walichokua wakimweleza, aliendelea kulia machozi, kabla hajawaeleza kilichotokea walishtukia magari mawili aina ya Landrover yakiegesha pembeni yao, wasichana wengine wote walitimukia porini na kuwaacha Nancy na msichana mwingine mmoja ambao walijikuta mikononi mwa polisi, walifungwa pingu na kutupwa nyuma ya gari ambako walikutana na askari mwenye virungu, aliyekitumia vizuri kirungu chake juu ya vichwa vyao! Nancy alilia kupita kiasi.
“Nyie malaya tumeshawaeleza msikae mtaa huu wanapita viongozi hamsikii siyo?” Askari alisema huku akiendelea kuwagonga na virungu vichwani, kama wewe mtoto mdogo kabisa unafanya umalaya.
“Mimi siyo……!” Nancy alijaribu kujieleza lakini kabla sentensi yake haijafikia mwisho kirungu kilitua juu ya pua yake na damu zilianza kutoka puani.
“Kimya! Funga domo lako changu wee unafikiri mimi nataka mapenzi hapa?” Alifoka askari huyo.
Kwa upande wake Nancy aliamini kama angepewa nafasi ya kujieleza askari huyu angeweza kumwachia huru lakini nafasi hiyo haikuwepo.
Walipofikishwa kituoni walitupwa mahabusu bila hata kutoa maelezo, kila mtu aliwaita malaya wazururaji, majina hayo yalimuuma sana Nancy ukizingatia katika maisha yake hakuwahi hata mara moja kukutana na mwanaume kimapenzi.
“Ninaitwa Lwina! Sijui mwenzangu unaitwa nani?” Changudoa waliyekamatwa nae alimuuliza, Nancy hakujibu aliendelea kulia machozi ya uchungu mambo yalikuwa yakitokea katika maisha yake yalimsikitisha kupita kiasi, hata siku moja katika maisha yake hakuwahi kufikiria kuwa angeweza kuitwa malaya!
“Unaitwa nani?”msichana yule aliuliza tena.
“Mimi naitwa N….a..n…cy!” Alijibu huku akilia machozi.
“Jina lako zuri sana wewe huwa unasimama kiwanja gani? Sababu kiwanja cha Ohio ndio kwanza nimekuona leo? Huwa upo Kinondoni au Las Vegas nini?”
“Hapana!”
“Oysterbay?”
“Viwanja vya nini dada?”
************
Kidubo na mke wake mama Teddy walimtafuta Nancy kwenye mkutano bila mafanikio, walishaamua kuishi naye nyumbani kwao mpaka mama yake amalize kifungo cha miaka mitano, walijua Nancy alikuwa na matatizo na alihitaji msaada mkubwa na waliamini msaada huu ulikuwa mikononi mwao.
Watu wote kwenye mkutano walisambaa bila Nancy kuonekana, ndipo walipoamua kuzunguka huku na kule jijini wakimtafuta bila mafanikio mwisho walikata tamaa na kuamua kuondoka kurejea nyumbani kwao Segerea.
“Si ajabu amekutana na kaka yake na kuamua kuondoka naye!” Kidubo alimwambia mke wake.
“Inawezekana!” Mkewe aliitikia.
“Basi tena Mungu anajua!”
Walirejea nyumbani wakiwa na masikitiko makubwa mno kumpoteza Nancy Moyoni mwao walishampenda sana Nancy na walitaka kumsaidia!
****************
Mpaka usiku wa manane ndani ya hoteli ya Sheraton wakiwa wamelala chumba kimoja na Mwinjilisti Heinz, Patrick alikuwa bado hajapata usingizi akiyafikiria maisha yake! Hakuamini yote yaliyomtokea katika maisha yake, kukutana na mzungu na kukubali kumsaidia hakikuwa kitu alichowahi kukifikiria maishani mwake.
Pamoja na mawazo hayo yote bado aliendelea kuwafikiria mama na dada yake Nancy ambao aliamini walikuwa wafu! Hakuwa na taarifa yoyote kuwa usiku huo Nancy alishakuja hadi nje ya hoteli ya Sheraton akimtafuta! Mawazo juu ya mama na dada yake yalimfanya atokwe na machozi.
Ghafla alishtukia akimwona Mwinjilisti Heinz akinyanyuka kitandani kwake na kwenda kwenye moja ya masanduku yake na kulifungua akatoa kitu kama bomba la sindano na chupa ya dawa fulani! Alitupa macho yake kuangalia kwenye kitanda cha Patrick, Patrick aliamua kujifanya amelala ili ajue ni kitu gani kilichotaka kutokea, Mwinjilisti alisogea hadi karibu kabisa na kitanda cha Patrick na kumchunguza usoni.
“He is fully asleep!”(amelala fofofo)Mwinjilisti alisema peke yake na kuondoka.
Patrick alishuhudia kila kitu kutoka kwenye kona ya jicho lake la kushoto alimwona Mwinjilisti akihangaika kujifunga na mpira wa plastiki na kujipigapiga, alionekana kama mtu aliyekuwa akitafuta mishipa wa damu mikononi mwake. Alionekana kutofanikiwa ndipo alipochukua mpira huo na kuufunga sehemu za siri kwenye uume wake! Kwa macho yake yote mawili Patrick alishuhudia Mwinjilisti akichoma sindano ndani ya uume wake! Alilegea na kuanza kulala hapohapo sakafuni.
Patrick aliogopa na kunyanyuka kitandani kwake kumkimbilia Mwinjilisti, akidhani labda madawa aliyojichoma yalimzidi.
“Mtumishi! Mtumishi! Mtumishi wa Mungu Heinz!” Patrick aliita lakini Mwinjilisti hakuitikia aliendelea kukoroma na kudondosha udelele mdomoni kwake.
Patrick alimnyanyua na kumpandisha Mwinjilisti kitandani huku akitetemeka, alifikiria kupiga simu mapokezi ili waje wampe msaada!
Patrick ameshuhudia mambo ya Mwinjilisti Heinz ambayo ni siri kubwa na Mwinjilisti humuua mtu yeyote agunduaye siri hiyo!
Je nini kitampata Patrick?
Nancy yupo mahabusu akidhaniwa ni changudoa!
Je nini kinafuata?