Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,672
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 05
Mtu wa kwanza kabisa kufa alikuwa mwalimu wake, Lutambi. Anapoitwa na kuhojiwa, anakataa katakata. Haikuishia hapo, anajikuta akimuua mtu wa pili ambaye ni mwanafunzi handome aitwae Dioniz.
Hajui ni nini anachotakiwa kukifanya, akili yake imechanganyikiwa.
SONGA NAYO...
Kifo cha Dioniz kiliwasikitisha watu wengi sana, alikuwa kipenzi cha wanafunzi wengi shuleni kwao na si kwa wanafunzi peke yao bali hata walimu wake!
Lilikuwa ni pigo kwa kila mmoja wao na hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini Dioniz hakuwepo duniani! Wengi waliamini Dioniz alikuwa hai ila alikuwa ametoweka kwenda kusikojulikana na si ajabu Ulaya.
Wanafunzi wa Nsumba hawakuchoka kumtafuta, msako uliendelea usiku na mchana! Polisi nao walilazimika kuleta mbwa wa kunusa lakini hakuna mbwa hata mmoja aliyefanikiwa kuwapeleka kwenye shimo la maji machafu kulikokuwa na miili ya watu wawili.
Kwa siku saba Dioniz aliendelea kutafutwa bila mafanikio yoyote na hakuna mtu aliyehisi mahali alikokuwa wengi walijifariji kwa kusema Dioniz aliondoka shuleni kurejea nyumbani kwao kwa sababu katika kipindi hicho kulikuwa na tatizo ya ada ya shule kwa wanafunzi wengi! Lakini kwanini aondoke usiku? Wengi waliendelea kujiuliza bila majibu na walipofuatilia ofisini waligundua kuwa hakuwa na tatizo la ada ya shule.
***
Katika Shule ya Ngaza aliyosoma Anne hali ilikuwa mbaya pia, Emmaculata aliyekuwa mpenzi wa Dioniz kabla ya Anne kuyaingilia kati mapenzi yao alikuwa bado akimlilia Dioniz, aliamini kabisa Anne alifahamu vizuri mahali alikokuwa. Mara kwa mara alisisitiza upelelezi uzidi kufanyika na Anne abanwe ili aeleze.
Emmaculata hakuamini maneno kuwa Dioniz alipotea, wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kuuawa na maiti yake kufukiwa ardhini lakini alipolitoa wazo hilo kwa watu walimbeza na kumpuuzia! Alitamani amuulize Anne lakini alishindwa kufanya hivyo, aliamini asilimia mia moja Anne alikuwa mchawi na angeweza kumfanyia lolote hata kumuua kabisa.
****
Ilikuwa ni siku ya pili Anne akiwa mwenye mawazo mengi juu ya mauaji aliyokuwa ameyafanya! Muda mwingi alikuwa akilia na kumlaumu mama yake, hakupenda kuwa jinsi alivyokuwa alitaka awe na uhusiano na mvulana kama walivyokuwa wasichana wengine, lakini kila mvulana aliyekutaka naye alikufa! Jambo hilo lilimsikitisha sana.
Ni siku hiyo hiyo saa 11:30 jioni taarifa zilipelekwa ofisini kwa mwalimu mkuu msaidizi kuwa mwalimu Catherine hakuwepo kazini kwa siku mbili! Mkuu wa shule msaidizi alituma watu kuangalia kama alikuwepo nyumbani kwake.
“Hatujamkuta, tumekuta mlango wa nyumba yake umefungwa!”
Walimjibu mkuu wa shule msaidizi waliporejea.
“Hakuna mtu yeyote anayeishi naye?”
“Anaishi peke yake ila Mkuyuni kuna mchumba wake!”
“Basi nendeni hukohuko Mkuyuni kwa mchumba wake mkamwangalie si ajabu anaweza kuwa mgonjwa!”
Waliporudi baada ya masaa mawili jibu lilikuwa lilelile kuwa mwalimu Catherine hakuwepo Mkuyuni, mkuu wa shule alipojaribu kudadisi kama alimuaga mtu yeyote hakuna aliyekiri! Alipotafutwa mtu aliyekuwa naye mara ya mwisho jibu lake liliwapa utata!
“Ile siku ya mahafali mimi nilikuwa naye zamu lakini ilipotimu saa kumi na moja alfajiri aliondoka kurudi kwake, sikumwona tena nikafikiri labda amesafiri.
“Uliripoti mahali popote?”
“Ndiyo nilimwambia Wadeni!”
Watu walizidi kuchanganyikiwa walishindwa kuelewa ni nini kilikuwa kimetokea katika shule ya Ngaza, watu wawili kupotea kwa wakati mmoja halikuwa jambo la kawaida.
Habari za kupotea kwa mwalimu zilipoanza kuongelewa shuleni zilimtia Anne simanzi kubwa na kukiongeza kilio chake! Uongozi wa shule ulilazimika kutoa taarifa hiyo kwa polisi ambao mpaka wakati huo walikuwa bado wakiendelea na upelelezi wa kupotea kwa Dio.
****
“Itabidi huyu binti tuondoke naye ili atusaidie katika upelelezi wa suala hili tuna wasiwasi atakuwa anafahamu kitu fulani kuhusu kupotea kwa yule kijana!” mmoja wa maaskari alishauri baada ya Anne kuitwa ofisini kwa mahojiano zaidi.
Anne aliyasikia maneno hayo moja kwa moja hakutaka kabisa kupelekwa kituo cha polisi kama ilivyotokea mara ya kwanza mwalimu Lutambi alipokufa!
“Hiyo ni kazi yenu sisi hatuwezi kuwaingilia hata kidogo!’ Mwalimu Mkuu msaidizi alisema.
“Mfunge pingu upesi tuondoke naye sasa hivi, kituoni atasema tu alipo Dio!”
Bila kuchelewa mmoja wa maaskari aliyekuwepo ndani alinyanyuka na kumtia pingu mikononi Anne aliyekuwa akilia muda wote wa mahojiano na alizidi kusisitiza kuwa hakufahamu mahali alikokuwa Dioniz.
‘Utasema tu ukifika kituoni wewe si ndiye uliyekuwa nae mara ya mwisho!”
“Ndiyo lakini........!” Anne alishindwa kumalizia sentensi yake, kwikwi za kulia zilizidi kumkaba shingoni!
Anne alitolewa ofisini na kuanza kusukumwa na polisi akipelekwa kwenye gari la polisi lililokuwa limeegeshwa katikati ya uwanja wa mbele ya shule, wanafunzi waliokuwa mabwenini walimshuhudia Anne akisukumwa, kelele zaidi zilisikika kutoka ndani ya bweni liitwalo Machame! Bweni alilolala Emmaculata.
“Ni huyo huyo ndiye anafahamu alipo Dio! Mchukueni mchawi mkubwa huyo!”Alipiga kelele kwa nguvu Emmaculata.
Sauti ya Emmaculata ilipomfikia Anne pamoja na kwamba kweli alihusika na kupotea kwa Dio na mwalimu alijisikia vibaya sana moyoni mwake na kujikuta akimchukia Emma kwa mara nyingine.
Anne aliumia kujisikia muuaji, vifo cha Dioniz na mwalimu vilimuuma sana moyoni mwake, hakupenda Dioniz afe na zaidi ya yote mahali alipoficha maiti yake ndipo palipomsikitisha zaidi, Dio alikuwa kijana mzuri mno kutumbukizwa katika shimo la maji machafu tena ya chooni!
Ilikuwa si rahisi kwa mtu yeyote kufikiria kuwa miili wa Dio na mwalimu ilikuwa ndani ya shimo palepale shuleni! Anne alijua isingejulikana lakini bado aliamini kwake ilikuwa si rahisi kulisahau tukio hilo, siku zote za maisha yake angekuwa mtumwa wa siri hiyo jambo aliloliona ni mateso makubwa kwake lakini aliahidi kukaa nalo moyoni hadi kaburini!
Dakika tano baadaye gari liliegeshwa kituo cha polisi na Anne aliteremshwa na kupelekwa moja kwa moja hadi chumba cha upelelezi kilichokuwa na giza nene! Waipoingia, taa ziliwasha na Anne alisukumwa kwa nguvu na kuingia ndani ambako alikalishwa chini, hasira zilimkaba lakini alishindwa kumnyoshea askari kidole chake cha sumu akijua kufanya hivyo kungesababisha aaminike kuwa muuaji.
“Binti kama umefika hapa jiandae kueleza ukweli! Hapa si mchezo dada yangu, ukidanganya tu hutoki salama hebu pumzika kwanza ndio tuanze mahojiano yetu!” Alisema mmoja wa maaskari.
Anne alikaa chini kwa kama dakika ishirini hivi akiwa mwenye wasiwasi mkubwa, muda wote huo alishuhudia vifaa mbalimbali vikiingizwa chumbani yakiwemo mawe mawili makubwa! Aligundua yalikuwa maalum kwa ajili ya kumtesa ili aseme ukweli lakini aliuahidi moyo wake kutofanya hivyo!
“Dada wakati umefika sasa hebu nieleze wazi Dioniz yupo wapi?”
“Dioniz?”
“Ndiyo!”
“Tuliachana naye nje ya ukumbi siku ya mahafali!”
“Nje ya ukumbi? Unanitania siyo? Unaviona vifaa vyote hivi?”
“Ndiyo!”
‘Ni vifaa vya mateso kwa ajili yako usiposema ukweli tu nitavitumia!”
“Hata kama mtanitesa na kuniua kabisa sitakuwa na jibu jingine zaidi ya kusema sikumwona Dioniz, baada ya kuachana naye nilikuwa na mvulana mmoja aliyeitwa Benedict!”
“Una hakika?”
“Asilimia mia moja!”
“Unanidanganya mimi subiri sasa!”
Baada ya kusema hayo afande alichukua kinyundo kidogo na kuanza kumgonga nacho Anne kwenye visigino na magotini! Anne alilia kwa maumivu makali aliyoyapata!
“Jamani mtaniua bure mi sijui kitu chochote!”
“Utasema tu!”
Mateso yaliendelea hadi usiku lakini Anne hakuwahi kukubali kufahamu mahali alipokuwa Dio!
Mwili wake wote ulivimba kila sehemu, ndani ya nafsi yake alijua wazi kuwa kweli alihusika na vifo vya watu hao wawili lakini hakuwa tayari kutoboa siri hiyo kwani alijua huo ndio ungekuwa mwisho wa maisha yake kitu ambacho hakupenda kabisa kitokee! Alikuwa tayari kufa lakini si kutamka mahali mwili wa Dioniz ulipokuwa!
Ilipotimu saa nne ya usiku bila kusema kitu maafande walikusanya vifaa vyao vya mateso na kuondoka wakimwacha Anne amelala sakafuni, lawama zote za mateso yale Anne alimtupia mama yake.
****
Asubuhi siku iliyofuata majira ya saa tano idadi kubwa ya wanafunzi kutoka Shule za Ngaza na Nsumba walifurika kituo cha polisi cha kati mjini Mwanza, waliruhusiwa kwenda kituoni kumsalimia Anne, habari za kupotea kwa Dioniz na mlinzi wa shule ya Ngaza zilikuwa zimesambaa sana Mwanza mjini na katika vitongoji vyake kiasi kwamba watu wengi walitamani kumwona kwa macho Anne aliyetuhumiwa kuhusika na kupotea kwa Dioniz na pia kifo cha mwalimu Lutambi.
Kituoni haikuwa rahisi kwa wanafunzi kumwona Anne moja kwa moja mahabusu alikokuwa lakini walimwomba mkuu wa kituo awaruhusu kuongea na wanafunzi mwenzao walikubaliwa na mkuu wa kituo aliwaagiza maaskari wawili wamtoe Anne mahabusu ili asalimiane na wanafunzi wenzake.
Wanafunzi walitulia wakisubiri Anne atolewe mahabusu, dakika tatu baadaye walimwona mtu aliyevimba uso na viungo vya mwili akitoka katika chumba fulani kilichokuwa karibu na kaunta ya polisi, alipojaribu kutembea peke yake alishindwa na kuanguka chini.
Wanafunzi walipoangalia vizuri waligundua kuwa msichana yule alikuwa ni Anne! Wengi hasa ambao hawakuifahamu siri ya mauaji hayo walidondosha machozi.
Maaskari walimbeba hadi nje ambako alikalishwa kwenye msingi wa kituo! Aliponyanyua uso wake kuwaangalia wanafunzi wenzake Anne alilia machozi! Alitia huruma alikuwa amevimba mno usoni kutokana na kipigo wakati wa kuhojiwa.
“Pole Anne! lakini kweli unajua alipo huyo mwanafunzi wa Nsumba?”
“Hapana Angelina!”
“Mwalimu Catherine je?”
“Hata yeye sijamwona kabisa wananionea bure!”
Emmaculata aliyekuwa miongoni mwa wanafunzi waliokuwa kituoni na aliyasikia maneno hayo na kulazimika kusogea mbele ambako alianza kumzodoa!
“Unaonewa nini wakati huo ndio mchezo wako? Unajua kila kitu huna sababu ya kulia!”
Anne aligeuka kwa huruma na kumwangalia Emmaculata msichana waliyesoma naye darasa moja shuleni kwao na waliwahi kuwa marafiki kabla Dioniz hajajitokeza, hasira kali ilimshika Anne akajikuta akisahau kuwa kidole chake cha shahada kilikuwa ni sumu kali kuliko hata Thiodani!
“Wewe Emmaculata weweeeee!” Anne alimsonta Emmaculata kwa kidole chake huku akiwa amevimba kwa hasira.
Katika hali ambayo wanafunzi wengi hawakuitegemea Emmaculata alianguka chini kama mzoga na kuanza kufuka moshi mwili mzima! Wanafunzi wote walishangaa na wengine walianza kukimbia, Anne aligundua alikuwa amefanya kosa ambalo lingepelekea watu kuamini kuwa kweli alikuwa na nguvu za miujiza ya kichawi zenye uwezo wa kuondoa maisha!
“Hee! Kumbe kweli mchawi?” Ilisikia sauti ikitoka katika kundi la wanafunzi.
Anne alijilaumu kwa kitendo hicho na bila kuchelewa aliwaomba wanafunzi wamshikilie mkono na kumsogeza hadi mahali alipolala Emmaculata akitoka moshi na povu mdomoni kama mtu mwenye kifafa akitupa miguu huku na kule kama mtu aliyekuwa akitokwa na roho.
Anne alipomfikia alimsogezea Emmaculata mdomo karibu na sikio na bila mtu yeyote kuona alimpulizia kiasi kidogo cha pumzi sikioni.
****
Dioniz alikuwa ni mtoto wa tano na wa mwisho katika familia yao na ni yeye pekee aliyekuwa mtoto wa kiume na familia yake ilimtegemea yeye zaidi kuwa mrithi wa mali zote alizokuwa nazo baba yake, wazazi wake walimpa kila kitu alichokitaka na walihakikisha anapata elimu bora ili aweze kuziendesha vizuri shughuli za baba yake akiwa mtu mzima.
Taarifa za kupotea kwa Dioniz ziliwachanganya sana akili wazazi wake, presha ya mama yake ilipanda na kumwangusha chini akazirai, kwa siku saba mama huyo alikaa hospitali akisumbuliwa na ugonjwa mbaya wa kiharusi na alipooza upande mmoja wa mwili wake kwa sababu ya ugonjwa huo.
Walitumia kila uwezo waliokuwa nao kumtafuta Dioniz lakini hawakufanikiwa, walipiga simu kwa kila ndugu lakini hakuna aliyejitokeza na kusema Dioniz alikuwa kwake! Wazazi na ndugu wote walichanganyikiwa na waliposikia taarifa za Anne na hisia zilizokuwepo juu yake walitaka sana wamwone ili awaeleze kama kuna kitu chochote Dioniz alimweleza kabla ya kupotea.
Walipokwenda shule walimkuta Anne amekwishaondoka kwenda kwao Sengerema kwa mapumziko baada ya kutoka mahabusu, haikuwa gharama kubwa sana kwao kusafiri kwenda mpaka kisiwani Kome wilayani Sengerema ambako Anne na wazazi wake waliishi!
Majibu ya mama yake na Anne, Isabella yaliwasikitisha sana wazazi wa Dioniz, yeye alijua wazi kilichokuwa kikiendelea na alijua wasingeweza kufanya lolote.
“Mtoto wenu hajapotea isipokuwa kafa na maiti yake hamtaiona milele! Kwa sababu alimlazimisha mwanangu kufanya naye mapenzi na kuna mwalimu mmoja wa shule hiyohiyo aliwahi kumlazimisha nae akafa kifo kibaya! Sisi sio watu wa kuchezea” Alisema Isabella huku akifoka.
“Nini?” Aliuliza kwa ukali Regnald baba mzazi wa Dioniz.
“Umeshasikia! Na ninawaomba muondoke hapa nyumbani!”
“Mama acha kuwafukuza hao watu bado wanauchungu na mtoto wao!”
“Mimi hiyo sijui!”
“Binti ni kweli yanayosemwa na mama yako?”
“Hata mimi mwenyewe sijui kinachoendelea, huwa inanitokea tu ila mama anaelewa zaidi! Nilimpenda mno Dioniz nisingemuua ilikuwa bahati mbaya” Anne alijibu huku machozi yakimtoka.
Wazazi wa Dioniz waliondoka huku wakilia walipofika mjini Mwanza walichofanya ni kuitafuta familia ya marehemu mwalimu Lutambi na familia ya mwalimu Catherine ambao pia walikuwa na uchungu na kifo cha ndugu yao.
Siku hiyo hiyo usiku kilifanyika kikao na wote walikubaliana kutumia kila walichokuwa nacho kuhakikisha wanapambana na familia ya akina Anne!
“Tutatumia kila tulichonacho kuhakikisha kuwa tunalipiza kisasi, mimi nitakwenda Kigoma, wewe utakwenda Bagamoyo na wewe utakwenda Sumbawanga!” Mzee Regnald aligawa majukumu kwa watu wa familia zote.
Je nini kitaendelea?
Je watu hao wataweza kupambana na Anne na mama yake?
Je ni nini hatima ya kila kitu?
Mtu wa kwanza kabisa kufa alikuwa mwalimu wake, Lutambi. Anapoitwa na kuhojiwa, anakataa katakata. Haikuishia hapo, anajikuta akimuua mtu wa pili ambaye ni mwanafunzi handome aitwae Dioniz.
Hajui ni nini anachotakiwa kukifanya, akili yake imechanganyikiwa.
SONGA NAYO...
Kifo cha Dioniz kiliwasikitisha watu wengi sana, alikuwa kipenzi cha wanafunzi wengi shuleni kwao na si kwa wanafunzi peke yao bali hata walimu wake!
Lilikuwa ni pigo kwa kila mmoja wao na hakuna mtu aliyekuwa tayari kuamini Dioniz hakuwepo duniani! Wengi waliamini Dioniz alikuwa hai ila alikuwa ametoweka kwenda kusikojulikana na si ajabu Ulaya.
Wanafunzi wa Nsumba hawakuchoka kumtafuta, msako uliendelea usiku na mchana! Polisi nao walilazimika kuleta mbwa wa kunusa lakini hakuna mbwa hata mmoja aliyefanikiwa kuwapeleka kwenye shimo la maji machafu kulikokuwa na miili ya watu wawili.
Kwa siku saba Dioniz aliendelea kutafutwa bila mafanikio yoyote na hakuna mtu aliyehisi mahali alikokuwa wengi walijifariji kwa kusema Dioniz aliondoka shuleni kurejea nyumbani kwao kwa sababu katika kipindi hicho kulikuwa na tatizo ya ada ya shule kwa wanafunzi wengi! Lakini kwanini aondoke usiku? Wengi waliendelea kujiuliza bila majibu na walipofuatilia ofisini waligundua kuwa hakuwa na tatizo la ada ya shule.
***
Katika Shule ya Ngaza aliyosoma Anne hali ilikuwa mbaya pia, Emmaculata aliyekuwa mpenzi wa Dioniz kabla ya Anne kuyaingilia kati mapenzi yao alikuwa bado akimlilia Dioniz, aliamini kabisa Anne alifahamu vizuri mahali alikokuwa. Mara kwa mara alisisitiza upelelezi uzidi kufanyika na Anne abanwe ili aeleze.
Emmaculata hakuamini maneno kuwa Dioniz alipotea, wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kuuawa na maiti yake kufukiwa ardhini lakini alipolitoa wazo hilo kwa watu walimbeza na kumpuuzia! Alitamani amuulize Anne lakini alishindwa kufanya hivyo, aliamini asilimia mia moja Anne alikuwa mchawi na angeweza kumfanyia lolote hata kumuua kabisa.
****
Ilikuwa ni siku ya pili Anne akiwa mwenye mawazo mengi juu ya mauaji aliyokuwa ameyafanya! Muda mwingi alikuwa akilia na kumlaumu mama yake, hakupenda kuwa jinsi alivyokuwa alitaka awe na uhusiano na mvulana kama walivyokuwa wasichana wengine, lakini kila mvulana aliyekutaka naye alikufa! Jambo hilo lilimsikitisha sana.
Ni siku hiyo hiyo saa 11:30 jioni taarifa zilipelekwa ofisini kwa mwalimu mkuu msaidizi kuwa mwalimu Catherine hakuwepo kazini kwa siku mbili! Mkuu wa shule msaidizi alituma watu kuangalia kama alikuwepo nyumbani kwake.
“Hatujamkuta, tumekuta mlango wa nyumba yake umefungwa!”
Walimjibu mkuu wa shule msaidizi waliporejea.
“Hakuna mtu yeyote anayeishi naye?”
“Anaishi peke yake ila Mkuyuni kuna mchumba wake!”
“Basi nendeni hukohuko Mkuyuni kwa mchumba wake mkamwangalie si ajabu anaweza kuwa mgonjwa!”
Waliporudi baada ya masaa mawili jibu lilikuwa lilelile kuwa mwalimu Catherine hakuwepo Mkuyuni, mkuu wa shule alipojaribu kudadisi kama alimuaga mtu yeyote hakuna aliyekiri! Alipotafutwa mtu aliyekuwa naye mara ya mwisho jibu lake liliwapa utata!
“Ile siku ya mahafali mimi nilikuwa naye zamu lakini ilipotimu saa kumi na moja alfajiri aliondoka kurudi kwake, sikumwona tena nikafikiri labda amesafiri.
“Uliripoti mahali popote?”
“Ndiyo nilimwambia Wadeni!”
Watu walizidi kuchanganyikiwa walishindwa kuelewa ni nini kilikuwa kimetokea katika shule ya Ngaza, watu wawili kupotea kwa wakati mmoja halikuwa jambo la kawaida.
Habari za kupotea kwa mwalimu zilipoanza kuongelewa shuleni zilimtia Anne simanzi kubwa na kukiongeza kilio chake! Uongozi wa shule ulilazimika kutoa taarifa hiyo kwa polisi ambao mpaka wakati huo walikuwa bado wakiendelea na upelelezi wa kupotea kwa Dio.
****
“Itabidi huyu binti tuondoke naye ili atusaidie katika upelelezi wa suala hili tuna wasiwasi atakuwa anafahamu kitu fulani kuhusu kupotea kwa yule kijana!” mmoja wa maaskari alishauri baada ya Anne kuitwa ofisini kwa mahojiano zaidi.
Anne aliyasikia maneno hayo moja kwa moja hakutaka kabisa kupelekwa kituo cha polisi kama ilivyotokea mara ya kwanza mwalimu Lutambi alipokufa!
“Hiyo ni kazi yenu sisi hatuwezi kuwaingilia hata kidogo!’ Mwalimu Mkuu msaidizi alisema.
“Mfunge pingu upesi tuondoke naye sasa hivi, kituoni atasema tu alipo Dio!”
Bila kuchelewa mmoja wa maaskari aliyekuwepo ndani alinyanyuka na kumtia pingu mikononi Anne aliyekuwa akilia muda wote wa mahojiano na alizidi kusisitiza kuwa hakufahamu mahali alikokuwa Dioniz.
‘Utasema tu ukifika kituoni wewe si ndiye uliyekuwa nae mara ya mwisho!”
“Ndiyo lakini........!” Anne alishindwa kumalizia sentensi yake, kwikwi za kulia zilizidi kumkaba shingoni!
Anne alitolewa ofisini na kuanza kusukumwa na polisi akipelekwa kwenye gari la polisi lililokuwa limeegeshwa katikati ya uwanja wa mbele ya shule, wanafunzi waliokuwa mabwenini walimshuhudia Anne akisukumwa, kelele zaidi zilisikika kutoka ndani ya bweni liitwalo Machame! Bweni alilolala Emmaculata.
“Ni huyo huyo ndiye anafahamu alipo Dio! Mchukueni mchawi mkubwa huyo!”Alipiga kelele kwa nguvu Emmaculata.
Sauti ya Emmaculata ilipomfikia Anne pamoja na kwamba kweli alihusika na kupotea kwa Dio na mwalimu alijisikia vibaya sana moyoni mwake na kujikuta akimchukia Emma kwa mara nyingine.
Anne aliumia kujisikia muuaji, vifo cha Dioniz na mwalimu vilimuuma sana moyoni mwake, hakupenda Dioniz afe na zaidi ya yote mahali alipoficha maiti yake ndipo palipomsikitisha zaidi, Dio alikuwa kijana mzuri mno kutumbukizwa katika shimo la maji machafu tena ya chooni!
Ilikuwa si rahisi kwa mtu yeyote kufikiria kuwa miili wa Dio na mwalimu ilikuwa ndani ya shimo palepale shuleni! Anne alijua isingejulikana lakini bado aliamini kwake ilikuwa si rahisi kulisahau tukio hilo, siku zote za maisha yake angekuwa mtumwa wa siri hiyo jambo aliloliona ni mateso makubwa kwake lakini aliahidi kukaa nalo moyoni hadi kaburini!
Dakika tano baadaye gari liliegeshwa kituo cha polisi na Anne aliteremshwa na kupelekwa moja kwa moja hadi chumba cha upelelezi kilichokuwa na giza nene! Waipoingia, taa ziliwasha na Anne alisukumwa kwa nguvu na kuingia ndani ambako alikalishwa chini, hasira zilimkaba lakini alishindwa kumnyoshea askari kidole chake cha sumu akijua kufanya hivyo kungesababisha aaminike kuwa muuaji.
“Binti kama umefika hapa jiandae kueleza ukweli! Hapa si mchezo dada yangu, ukidanganya tu hutoki salama hebu pumzika kwanza ndio tuanze mahojiano yetu!” Alisema mmoja wa maaskari.
Anne alikaa chini kwa kama dakika ishirini hivi akiwa mwenye wasiwasi mkubwa, muda wote huo alishuhudia vifaa mbalimbali vikiingizwa chumbani yakiwemo mawe mawili makubwa! Aligundua yalikuwa maalum kwa ajili ya kumtesa ili aseme ukweli lakini aliuahidi moyo wake kutofanya hivyo!
“Dada wakati umefika sasa hebu nieleze wazi Dioniz yupo wapi?”
“Dioniz?”
“Ndiyo!”
“Tuliachana naye nje ya ukumbi siku ya mahafali!”
“Nje ya ukumbi? Unanitania siyo? Unaviona vifaa vyote hivi?”
“Ndiyo!”
‘Ni vifaa vya mateso kwa ajili yako usiposema ukweli tu nitavitumia!”
“Hata kama mtanitesa na kuniua kabisa sitakuwa na jibu jingine zaidi ya kusema sikumwona Dioniz, baada ya kuachana naye nilikuwa na mvulana mmoja aliyeitwa Benedict!”
“Una hakika?”
“Asilimia mia moja!”
“Unanidanganya mimi subiri sasa!”
Baada ya kusema hayo afande alichukua kinyundo kidogo na kuanza kumgonga nacho Anne kwenye visigino na magotini! Anne alilia kwa maumivu makali aliyoyapata!
“Jamani mtaniua bure mi sijui kitu chochote!”
“Utasema tu!”
Mateso yaliendelea hadi usiku lakini Anne hakuwahi kukubali kufahamu mahali alipokuwa Dio!
Mwili wake wote ulivimba kila sehemu, ndani ya nafsi yake alijua wazi kuwa kweli alihusika na vifo vya watu hao wawili lakini hakuwa tayari kutoboa siri hiyo kwani alijua huo ndio ungekuwa mwisho wa maisha yake kitu ambacho hakupenda kabisa kitokee! Alikuwa tayari kufa lakini si kutamka mahali mwili wa Dioniz ulipokuwa!
Ilipotimu saa nne ya usiku bila kusema kitu maafande walikusanya vifaa vyao vya mateso na kuondoka wakimwacha Anne amelala sakafuni, lawama zote za mateso yale Anne alimtupia mama yake.
****
Asubuhi siku iliyofuata majira ya saa tano idadi kubwa ya wanafunzi kutoka Shule za Ngaza na Nsumba walifurika kituo cha polisi cha kati mjini Mwanza, waliruhusiwa kwenda kituoni kumsalimia Anne, habari za kupotea kwa Dioniz na mlinzi wa shule ya Ngaza zilikuwa zimesambaa sana Mwanza mjini na katika vitongoji vyake kiasi kwamba watu wengi walitamani kumwona kwa macho Anne aliyetuhumiwa kuhusika na kupotea kwa Dioniz na pia kifo cha mwalimu Lutambi.
Kituoni haikuwa rahisi kwa wanafunzi kumwona Anne moja kwa moja mahabusu alikokuwa lakini walimwomba mkuu wa kituo awaruhusu kuongea na wanafunzi mwenzao walikubaliwa na mkuu wa kituo aliwaagiza maaskari wawili wamtoe Anne mahabusu ili asalimiane na wanafunzi wenzake.
Wanafunzi walitulia wakisubiri Anne atolewe mahabusu, dakika tatu baadaye walimwona mtu aliyevimba uso na viungo vya mwili akitoka katika chumba fulani kilichokuwa karibu na kaunta ya polisi, alipojaribu kutembea peke yake alishindwa na kuanguka chini.
Wanafunzi walipoangalia vizuri waligundua kuwa msichana yule alikuwa ni Anne! Wengi hasa ambao hawakuifahamu siri ya mauaji hayo walidondosha machozi.
Maaskari walimbeba hadi nje ambako alikalishwa kwenye msingi wa kituo! Aliponyanyua uso wake kuwaangalia wanafunzi wenzake Anne alilia machozi! Alitia huruma alikuwa amevimba mno usoni kutokana na kipigo wakati wa kuhojiwa.
“Pole Anne! lakini kweli unajua alipo huyo mwanafunzi wa Nsumba?”
“Hapana Angelina!”
“Mwalimu Catherine je?”
“Hata yeye sijamwona kabisa wananionea bure!”
Emmaculata aliyekuwa miongoni mwa wanafunzi waliokuwa kituoni na aliyasikia maneno hayo na kulazimika kusogea mbele ambako alianza kumzodoa!
“Unaonewa nini wakati huo ndio mchezo wako? Unajua kila kitu huna sababu ya kulia!”
Anne aligeuka kwa huruma na kumwangalia Emmaculata msichana waliyesoma naye darasa moja shuleni kwao na waliwahi kuwa marafiki kabla Dioniz hajajitokeza, hasira kali ilimshika Anne akajikuta akisahau kuwa kidole chake cha shahada kilikuwa ni sumu kali kuliko hata Thiodani!
“Wewe Emmaculata weweeeee!” Anne alimsonta Emmaculata kwa kidole chake huku akiwa amevimba kwa hasira.
Katika hali ambayo wanafunzi wengi hawakuitegemea Emmaculata alianguka chini kama mzoga na kuanza kufuka moshi mwili mzima! Wanafunzi wote walishangaa na wengine walianza kukimbia, Anne aligundua alikuwa amefanya kosa ambalo lingepelekea watu kuamini kuwa kweli alikuwa na nguvu za miujiza ya kichawi zenye uwezo wa kuondoa maisha!
“Hee! Kumbe kweli mchawi?” Ilisikia sauti ikitoka katika kundi la wanafunzi.
Anne alijilaumu kwa kitendo hicho na bila kuchelewa aliwaomba wanafunzi wamshikilie mkono na kumsogeza hadi mahali alipolala Emmaculata akitoka moshi na povu mdomoni kama mtu mwenye kifafa akitupa miguu huku na kule kama mtu aliyekuwa akitokwa na roho.
Anne alipomfikia alimsogezea Emmaculata mdomo karibu na sikio na bila mtu yeyote kuona alimpulizia kiasi kidogo cha pumzi sikioni.
****
Dioniz alikuwa ni mtoto wa tano na wa mwisho katika familia yao na ni yeye pekee aliyekuwa mtoto wa kiume na familia yake ilimtegemea yeye zaidi kuwa mrithi wa mali zote alizokuwa nazo baba yake, wazazi wake walimpa kila kitu alichokitaka na walihakikisha anapata elimu bora ili aweze kuziendesha vizuri shughuli za baba yake akiwa mtu mzima.
Taarifa za kupotea kwa Dioniz ziliwachanganya sana akili wazazi wake, presha ya mama yake ilipanda na kumwangusha chini akazirai, kwa siku saba mama huyo alikaa hospitali akisumbuliwa na ugonjwa mbaya wa kiharusi na alipooza upande mmoja wa mwili wake kwa sababu ya ugonjwa huo.
Walitumia kila uwezo waliokuwa nao kumtafuta Dioniz lakini hawakufanikiwa, walipiga simu kwa kila ndugu lakini hakuna aliyejitokeza na kusema Dioniz alikuwa kwake! Wazazi na ndugu wote walichanganyikiwa na waliposikia taarifa za Anne na hisia zilizokuwepo juu yake walitaka sana wamwone ili awaeleze kama kuna kitu chochote Dioniz alimweleza kabla ya kupotea.
Walipokwenda shule walimkuta Anne amekwishaondoka kwenda kwao Sengerema kwa mapumziko baada ya kutoka mahabusu, haikuwa gharama kubwa sana kwao kusafiri kwenda mpaka kisiwani Kome wilayani Sengerema ambako Anne na wazazi wake waliishi!
Majibu ya mama yake na Anne, Isabella yaliwasikitisha sana wazazi wa Dioniz, yeye alijua wazi kilichokuwa kikiendelea na alijua wasingeweza kufanya lolote.
“Mtoto wenu hajapotea isipokuwa kafa na maiti yake hamtaiona milele! Kwa sababu alimlazimisha mwanangu kufanya naye mapenzi na kuna mwalimu mmoja wa shule hiyohiyo aliwahi kumlazimisha nae akafa kifo kibaya! Sisi sio watu wa kuchezea” Alisema Isabella huku akifoka.
“Nini?” Aliuliza kwa ukali Regnald baba mzazi wa Dioniz.
“Umeshasikia! Na ninawaomba muondoke hapa nyumbani!”
“Mama acha kuwafukuza hao watu bado wanauchungu na mtoto wao!”
“Mimi hiyo sijui!”
“Binti ni kweli yanayosemwa na mama yako?”
“Hata mimi mwenyewe sijui kinachoendelea, huwa inanitokea tu ila mama anaelewa zaidi! Nilimpenda mno Dioniz nisingemuua ilikuwa bahati mbaya” Anne alijibu huku machozi yakimtoka.
Wazazi wa Dioniz waliondoka huku wakilia walipofika mjini Mwanza walichofanya ni kuitafuta familia ya marehemu mwalimu Lutambi na familia ya mwalimu Catherine ambao pia walikuwa na uchungu na kifo cha ndugu yao.
Siku hiyo hiyo usiku kilifanyika kikao na wote walikubaliana kutumia kila walichokuwa nacho kuhakikisha wanapambana na familia ya akina Anne!
“Tutatumia kila tulichonacho kuhakikisha kuwa tunalipiza kisasi, mimi nitakwenda Kigoma, wewe utakwenda Bagamoyo na wewe utakwenda Sumbawanga!” Mzee Regnald aligawa majukumu kwa watu wa familia zote.
Je nini kitaendelea?
Je watu hao wataweza kupambana na Anne na mama yake?
Je ni nini hatima ya kila kitu?