Tabu Ley afariki

Tabu Ley afariki

images

114825625.jpg
 
RIP Chiriku Pascal..tutabaki tunakukumbuka kwa sauti yako nyororo na wana AFRISA INTERNATIONALE
 
Tabu Ley, Tutakukumbuka kwa vibao vyako kama vile: Twende Nairobi (wimbo ulioimbwa na Mbilia Bel), Bessama Muchacha, Maze n.k.

Kuna wimbo wake Sacramento naupenda sana. Kila ninapoupiga unanikumbusha ujana wangu nikiwa Mwalimu. Tulikuwa na kijoint fulani jioni tukienda kula nyama choma, kupata kinywaji na kusikiliza muziki Congolee. A prolific music writer indeed. Kusikia kafariki roho imeniuma sana jamani mwenzenu. Naona nitapiga sana huu wimbo iwe njia yangu ya kuomboleza Tabu Ley. Sacramento, Sango Lamu.... Lakini pia nazipenda nyimbo zake Mokolo nakokufa, Felly Mour, na zile nyimbo nyingine aliimba kipindi chake na Mbilia Bel. R

IP mwana wa Afrika. Tulikupenda sana...lakini Mungu kakupenda Zaidi.
 
Kila nafsi itaonja mauti...
Kwa masikitiko na huzuni Mwanaadamu huondoka kwa kusindikizwa na watatu:- 1.Ndugu,wapenzi wake.. 2.Mali na mamluki yake.. na 3.Matendo yake duniani..!! viwili vitarudi nyuma ( 1,2 ) na atazikwa na kubaki na kimoja namba 3 (Matendo yake)...!! Mema au Maovu.
 
Du! mkuu wa nyimbo za kiutu uzima kwaheri.

Sote tupo njia moja ya kurudi mavumbini, mwezi Mungu ailaze roho yako mahali pema,Amina.

Nakumbuka vibao vyako vya Amilo (Ponpon Kuleta) na ulikipiga kwa muda wa dakika 9 na Ma Fille dakika ulitumia dakika nane 8.

Nyimbo hizi mbili ulionyesha ni jinsi gani wewe ni mtunzi wa nyimbo za kiutu uzima, nyimbo zimetulia.

Tabu Ley ntakukumbuka daima kwa kumtunza bibie Mbilia Bell ambae aling'ara sana wakti ule na bendi yenu ya Afrisa International.

Jamani kama kuna mtu anaweza kuweka video kuonyesha vibao hivi viwli basi tafwadhali anisaidie.

Ahsante.
 
Mkuu hicho kibao kwa matamshi kilikuwa kinaitwa mburugukweni. Jinsi ya kuandika kwa kifaransa au kilingala sijui.

Tiba

Nilikuwa nikisikia redio one akikipiga marehemu Uncle J na Gamba. Nikipenda sana... nitaupataje huu wimbo?
 
Mkuu hicho kibao kwa matamshi kilikuwa kinaitwa mburugukweni. Jinsi ya kuandika kwa kifaransa au kilingala sijui.

Tiba

Huo wimbo alikuwa anaupiga sana Uncle J. Na sasa hivi Gamba Muyenjwa. Nitaupataje huu wimbo?
 
Back
Top Bottom