Tabora mji wa washamba kubayaaa

Tabora mji wa washamba kubayaaa

Kumbukeni Tabora ina historia kubwa kwa uhuru wa nchi.Tabora ni watu walioelewa haraka maana ya vyama Vingi.Walimpa tabu kidogo Nyerere.Ninachowapendea Wanyamwezi sio wanafiki kwenye kusema ukweli wanakuchana live.Nawakumbuka James Mapalala,Kasanga Tumbo, Abdala Fundikira, Kasela Bantu

Wewe huwajui vizuri wanyamwezi...ni watu wa maneno maneno sanaa, fitina sanaa.
 
1/ ni watu wa dini sana wengi wao waislam 2/ mostly sio watu wa pombe 3/ wakarimu na sio wachoyo wa chakula 4/ wasafi 5/ wanawake wanajua mpz na kutunza mume 6/ wavumilivu kwenye mahusiano 7/ mwanamke akikuchoka kamaanisha 8/hawana tamaa ya mali9/ wanawake si wajepukaji 10/ wakulima wazuri and sooooo
 
Hili bandiko ni la mtu asiye na elimu, hekima na wala hajitambui.

Vinginevyo atakuwa ni kijana mdogo sana ambaye hata kamasi za utoto hazijakauka.

Sehemu wanayoishi binadamu hauwezi kupasema ni pabaya.

Pangelikuwa ni pabaya wangelihama na kutafuta mahali pengine pakuishi, dunia ni kubwa hii.

Hivi ulishafika maeneo ya mikoa ambayo ni semi desert, hakuna miti, hakuna kilimo chenye tija, maji ni shida, watu wanatumia vinyesi vya mifugo kama nishati ya kupikia, lakini watu wapo, wanapapenda na wanapaona ni pazuri.

Na wakisafiri kwamfano kuja Dar wanapamiss mno kwao na wanarudi hima kwa haraka maana ni pazuri na pamawafaa kwa maisha yao.

Kuzungumzia pahala wanapoendeshea maisha na kujipatia riziki binadamu wenziyo ni zaidi ya utoto.

Haya, toa ushauri wako basi ili wahame huko, waende pazuri unapopaona wewe ni panafaa?
Hili jamaa ndio maana walilipiga ndani.
 
mjini haijabadilika mkuu, nimetoka huko mwaka 1994 nikiwa nimemaliza milambo secondary nikarudi 2018 hiim nikapita mitaa ya mwanza road, chemchem, isevya, kiloleni, nyumba nilizoacha miaka hiyo zipo vile vile, kwa kweli haijabadilika, ila nje ya mji kiduuuchu imebadilika, ila bado sana, sasa hujatembelea wilaya zake kama urambo, igunga, nzega, na sikonge, unaweza ukasema usirudi, ila napasifu kwa asali tu
Sasa wewe mzee ulienda mitaa ya uswahilini je ulienda cheyo A, B, na C na je ulifika Mitaa ya Ipuli Bonana na freemasonry na je sansiro!
 
Back
Top Bottom