Tabora mji wa washamba kubayaaa

Tabora mji wa washamba kubayaaa

mjini haijabadilika mkuu, nimetoka huko mwaka 1994 nikiwa nimemaliza milambo secondary nikarudi 2018 hiim nikapita mitaa ya mwanza road, chemchem, isevya, kiloleni, nyumba nilizoacha miaka hiyo zipo vile vile, kwa kweli haijabadilika, ila nje ya mji kiduuuchu imebadilika, ila bado sana, sasa hujatembelea wilaya zake kama urambo, igunga, nzega, na sikonge, unaweza ukasema usirudi, ila napasifu kwa asali tu
Kama ungekuwa na Imani ya Mungu ningekuambia Muogope Mungu, tangu 1994 hakuna mabadiliko kweli, unamuongepea Nani sasa? Na kwa faida ipi? Au ulitaka mabadiliko yepi kwa mfano?
 
Tabora pakiwa pabaya basi hakuna mji mzuri katika nchi hii.
Mji ulipangwa vizuri kuliko mji wowote hapa nchini.
Hauna vichochoro kama Dar
Hauna vumbi kama Dodoma au Shinyanga.
Agreed......
 
Sasa Tabora utafananisha na mikoa kama Morogoro au Kilimanjaro.

Tabora is far better than Morogoro and Kilimanjaro combined.
 
Ogopa sana maeneo ambayo Sisiem INA kubalika Kwa asilimia kubwa,huwa ni masikini WA elimu,makazi,maendeleo ,afya,nk
Karibuni mjiunge kelele na dharau za nini wakati mnaishia Chama Cha Maono.
 
Nimeishi Tabora kwa zaidi ya miaka 20,nimesomea hukohuko(Tbr mjini)

Sifa za Tbr ni kama zifuatazo

Watu wake ni wakarimu hasa kwa chakula
Maendeleo yanakuwa kwa taratibu sana

Ushirikina upo sana na mtu anaweza kukufanyia kisa tu una maendeleo fulani

Vichaa ni wengi sana na hufanya mapenzi hadharani huku watu wakiwaangalia na kufurahia,wengi pia hutoka kigoma wakija kwa treni

Mtu anaweza kuwa na nyumba ya matope tena katikati ya mji ya urithi na ukitaka kuinunua atakuambia baba au babu alitoa wosia hii nyumba isiuzwe

Warembo wazuri wapo wengu ila nao wana tabia za ushirikina

Warembo wanapenda sana kuolewa hata ukimwambia kiutani lazima akawaambie kwao

Ndoa ni nyingi sana lakini hazidumu

Mabinti wengi huzalia nyumbani kabla ya ndoa

Majungu na fitina ndo kwao

Barabara za Lami ni nyingi sana katikati mwa mji zilifadhiliwa na World Bank

Wanaipenda sana CCM na hasa kina mama huwaambii kitu kwa CCM

Wabunge wao ni wa CCM tu na huwa hawakai miaka 10 ni 5 tu unatolewa,Aden Rage na wengine wa nyuma walikaa miaka 5 wakapigwa chini,hata huyu wa sasa hawezi kupewa miaka mitano mingine,kashachokwa mapema labda itumike nguvu toka juu
Nyymba za matope ni nyingi sana maeneo km Gongoni, kiloleni,chemchem,ng'ambo,mwanza road,mabatini,tambukareli...Ajabu ni kuwa nyumba hz za matope wanatoka watoto wakali sana

Usisahau shule kali kama Tabora boys,Tbr girls, kazima, Milambo na Isevya zimetoa watu wengi ambao ni viongozi,wacheza mpira n.k.

Waarabu na wasomali ni wengi pia

Vyakula ni vingi na bei ni rahisi,ukiwa na 3000 unakula milo mitatu.
 
Tabora pakiwa pabaya basi hakuna mji mzuri katika nchi hii.
Mji ulipangwa vizuri kuliko mji wowote hapa nchini.
Hauna vichochoro kama Dar
Hauna vumbi kama Dodoma au Shinyanga.
Sio kweli
 
Shin
Tabora pakiwa pabaya basi hakuna mji mzuri katika nchi hii.
Mji ulipangwa vizuri kuliko mji wowote hapa nchini.
Hauna vichochoro kama Dar
Hauna vumbi kama Dodoma au Shinyanga.
Shinyanga nao ulipangwa, maeneo mengi yalipimwa na sasa unapendeza matembe mengi yamebomolewa, alieondoka 1995 hapo atapotea tu.
 
Back
Top Bottom