- Mkuu hela za EPA legally zilikuwa ni za mkopo sio kwamba zilikuwa ni hela za wizi, however ni hela zilizochukuliwa na kundi la Mtandao, toka hii ishu ianze tumeona wahusika wote wakitajwa na kufikishwa kwenye mkono wa sheria, sasa leo the question ni kwamba Where was Malecela huko nyuma mpaka aje aingie leo? Halafu Mtandao walikuwa wanapigana na Malecela sasa ilikuwaje tena wakampa hela hizo hizo wanazompiga nazo? It does not make any sense at all!
William @ NYC, USA.
Hapo kwenye maneno, "legally zilikuwa ni za mkopo" una maana kuwa CCM walikopa fedha kihalali kutoka vyombo vya fedha kwa taratibu za mikopo?kama ni kweli hizo taratibu na masharti ya mkopo yalikuwaje? wakati wa urejeshaji ilikuwaje mpaka watu watajwe kama mafisadi ndiyo wakaanza kurejesha fedha? hata hivyo kwanini waliokuwa wakirejesha siyo (CCM) waliokopa bali watu wengine (mafisadi)?kundi la mtandao (ambalo siyo CCM) ulilotaja lilitoka wapi? una maana fedha ziliibwa mikononi mwa CCM na wanamtandao?
Ninachoona unakubaliana na ukweli kuwa CCM walichukua fedha lakini hapo hapo unataka kusema kuwa Malecela hakuhusika. Kwa vipi Malecela hakuhusika wakati yeye alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM?
Kwa hiyo Malecela naona wamtetea Malecela bila kuwa na hoja zinazotosheleza kujibu maswali ya msingi juu ya wizi wa EPA.