Tabora: Bodaboda yagonga Treni, Mwanafunzi afariki dunia

Tabora: Bodaboda yagonga Treni, Mwanafunzi afariki dunia

Bawabu wa pili

Senior Member
Joined
Nov 14, 2025
Posts
147
Reaction score
432
Binti aliyejulikana kwa jina la Tatu Mgeta (23), mwanafunzi wa Chuo cha Tabora Polytechnic College, amefariki dunia huku dereva wa bodaboda akijeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea wakati walipokuwa wamepakizana kuelekea chuoni,kugongana na treni ya abiria iliyokuwa ikitokea mkoani Tabora kuelekea mkoani Katavi.

Tukio hilo limetokea katika maungio ya reli yaliyopo Kata ya Isevya, Manispaa ya Tabora, Januari 20, 2025.



Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Maganga Peter na Abdallah Ismail, ajali hiyo ilitokana na bodaboda kushindwa kuzingatia sheria za barabarani, ikiwemo ishara ya bendera ya muongoza treni pamoja na honi iliyotolewa kwenye makutano hayo.

Mashuhuda hao pia wameiomba Serikali kuweka kingo na alama za tahadhari katika maungio hayo ya reli, ili kuwasaidia watumiaji wa barabara kutambua uwepo wa treni.

Wamesema changamoto hiyo inatokana na baadhi ya watumiaji wa barabara kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu alama za barabarani, pamoja na baadhi ya wengine kuzipuuzia.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Afisa Utawala wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tabora, Afisa Mnadhimu Omary Simba, amesema majeruhi mmoja ameelekwa hospitali kwa matibabu huku akibainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa dereva wa bodaboda kwa kutokuzingatia sheria za barabarani.
 
Kuna boda jana kaburuzwa na Semi Singida mjini, yeye katoka barabara ya pembeni anaingia highway hataki kusubiri,Semi ikaburuza chini ya uvungu tairi ya mbele ya pikipiki ikanang'oka na yeye katobolewa vibaya sehemu ya Usoni sijui kama alipona.
 
Kwann mtu akifika pale hatoki
Hehehehe navo penda sifa sasa umekuja, Kuna mtu anaitwa David Bernoulli miaka ya 1700s aligundua kwamba fluids,Gas, air na object zikiwa kwenye speed kubwa pressure kwenye hyo fluid,Gas ,air na hyo object inapungua kulingana na speed yenyew,....sasa twende kwenye issue yako kwann watu wanaganda😎😎😁,huyo mtu akiwa jirani na treni pale pressure ya hewa kati ya treni na huyo mtu inapungua sana kulingana na speed ya train sasa ile hewa ambayo Iko nyuma ya yule mtu nyenyewe inakuwa kubwa kuliko ile ambayo Iko kati ya train na mtu,so hyo pressure ndo inamsukuma huyo mtu kuelekea kwenye train,kumbuka pressure huwa inatoka kwenye high kwenda kwenye low😎😎,..

Nakuongeza ukijenga jiko halafu ukaweka lile bomba la kutolea moshi juu,hata ukiliweka mbali na sehemu ya moto,moshi lazima utafata lile bomba lilipo ndipo utoke nje😁😁😁,yote hyo ni ktu kimoja kinaendeshwa na Bernoulli principles.....

So
High flow=low pressure
Low flow=high pressure

Ukitaka formula nayo naweza nikakumiminia ndugu mwanafunzi😁😁
 
Back
Top Bottom