Tabia za wanawake wasomi na wenye hela

Tabia za wanawake wasomi na wenye hela

Status
Not open for further replies.
Hili si kweli labda useme baadhi yao, mimi nawafahamu wasomi tena wa hali ya juu lakini ni watu poa sana. Hawana majivuno wala maringo, ila wnazijua haki zao na hawakubali upumbavupumbavu wa aina yoyote ile.

Mkuu mi nadhani kuna haja ya mumuuliza mtoa mada anamaanisha nini anaposema "wasomi",maana kuna watu wana tafsiri wanazozijua wao kuhusiana na maneno mbalimbali!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kusoma na tabia ya mtu ni vitu tofauti. Kuna watu hawajasoma na waliosoma wana tabia ulizotaja.
Sema elimu inamsaidia mtu kujitambua, ndio hapo mtu atakuona unaringa, na hayo mengine.
Wengine mnapenda wanawake wa kuwapiga mizinga muwanyanyase, ukiona mwanamke anajimudu ukileta ujinga anakutupa kule unahisi anaringa na ujeuri, ni kujitambua tu.
Mpo wachache mliosoma lkn pia mmetulia kama hivi...angalia majibu ya wenzako hapo kachallange kadogo tu wanashidwa kuargue wanatukana na kumshusha mtoa mada.. Lkn pia naona kwa mademu wa kibongo..huwa nafikiria huko mahostel chuo huwa hawafundishani nanma ya kujenga hoja..? No wonder mtu akiwa ndani anapiga makelele tu akitumia nguvu ya kusoma na hela..
 
Nafikiri ni tabia ya mtu mmoja mmoja
 
Umejuaje mtoa mada anaelimu ndogo..huko mahostel hamfundishani nan mna ya kuargue mkipewa challange kidogo
Pole pia, maisha ya hostel nishayavuka enzi za mwalimu
hiyo ni inferiority complex over
 
Tabia haina dawa. Kuna mtu hajasoma lakini mziki wake ni balaa. Na kuna mwanaume kasoma lakini ndo hajiamini, full ugomvi. Kabla haujajisikia unadharauliwa, jiheshimu
 
Inferiority complex ni tatizo sana kwa wanaume wenye elimu ndogo pole....
mwanaume unatakiwa kujiamini!!!

Sawa kabisa....mimi napenda mwanaume anayejiamini nakutambua nafasi yake aliyopewa na Mungu....hata kama hajaelimika au hana pesa ataheshimika tu....hebu na muanze kujiamini ninyi watu
 
Sawa kabisa....mimi napenda mwanaume anayejiamini nakutambua nafasi yake aliyopewa na Mungu....hata kama hajaelimika au hana pesa ataheshimika tu....hebu na muanze kujiamini ninyi watu

Hawajui kama kujiamini ndo silaha kubwa....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom