Tabia za Makondakta zinazonikera

Tabia za Makondakta zinazonikera

mapipando

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
2,922
Reaction score
3,563
1. Unalipa nauli lets say unatoa elfu moja, na nauli ni mia nne, konda anakuuliza wangapi? Kama ninao watu/ mtu wa kumlipia si ningesema mweneyewe!

2. Unatoa shilingi elfu kumi, konda anaanza kulalamika oo unatoa hela kubwa mara kimepanda kimeshuka na maneno machafu kibao. Mimi akiniuliza huna hela ndogo hapo mpaka utoe hii, namwambia ninayo nachukua elfu kumi yangu nampa mia, maana ndio hela ndogo niliyonayo, konda anaona anadharauliwa. Unanipangiaje pesa ya kutumia? Kama huna chenchi mimi inanihusu nini?

3. Unatoa nauli mathalani elfu 2, 5 au 10, konda hakupi chenchi anasubiria sijui usahau ili a-make super profit! Huwezi fanikiwa kwa kuiba vi elfu mbili mbili vya abiria.

Ongezea na wewe kero zako.
 
Unampa hela ya nauli anakuuliza,"una 100???"
Kama hauna unasubirishwa chenchi na usipodai hupati hiyo100
Wengine bila aibu et 100 tu unadai?
 
Binafsi huwa siko tayari kulipa zaidi ya nauli husika eti kwasababu tu konda hana chenchi.nitaidai haki yangu, ikiwezekana ile kwake no matter how other people will say.
 
konda kunidanganya eti kuna siti kumbe hakuna....

konda chenchi ni mia, anatoa safaru ya mia mbili anasema tutagawana na abiria mwenzangu....

konda gari imejaa bado anapoga kelele nje eti gari iko tupu....

nashukia manzese darajani ye kona ananilazimisha kushukia tiptop eti darajani hasimami....
 
Unampa hela ya nauli anakuuliza,"una 100???"
Kama hauna unasubirishwa chenchi na usipodai hupati hiyo100
Wengine bila aibu et 100 tu unadai?

Kama hana chenchi si dhambi akikuambia usubiri almradi akupatie au kama unayo mia mmpe ili akupatie mia mbili.
 
Kama hana chenchi si dhambi akikuambia usubiri almradi akupatie au kama unayo mia mmpe ili akupatie mia mbili.

j3 mpaka jpili konda hana100???
Ni wizi tu yeye kama mfanyabiashara anatakiwa kuwa na chenchi
 
1. Unalipa nauli lets say unatoa elfu moja, na nauli ni mia nne, konda anakuuliza wangapi? Kama ninao watu/ mtu wa kumlipia si ningesema mweneyewe!

2. Unatoa shilingi elfu kumi, konda anaanza kulalamika oo unatoa hela kubwa mara kimepanda kimeshuka na maneno machafu kibao. Mimi akiniuliza huna hela ndogo hapo mpaka utoe hii, namwambia ninayo nachukua elfu kumi yangu nampa mia, maana ndio hela ndogo niliyonayo, konda anaona anadharauliwa. Unanipangiaje pesa ya kutumia? Kama huna chenchi mimi inanihusu nini?

3. Unatoa nauli mathalani elfu 2, 5 au 10, konda hakupi chenchi anasubiria sijui usahau ili a-make super profit! Huwezi fanikiwa kwa kuiba vi elfu mbili mbili vya abiria.

Ongezea na wewe kero zako.

Ukisema makonda ni wachafu nitakuunga mkono. Lakini hili la chenchi linawahusu abiria na kondakta ambao lazima tuwasemee maana muda wa kuingia humu hawana. Ni asubuhi abia wanne wanatoa noti za sh. Kumi 10 sawa na sh 40, 000 wkt nauli ni sh 500?
 
I wish angetokea konda hapa naye akaeleza kero zake kuhusu abiria. Kuna abiria wanakera jamani mweh!
 
konda kunidanganya eti kuna siti kumbe hakuna....

konda chenchi ni mia, anatoa safaru ya mia mbili anasema tutagawana na abiria mwenzangu....

konda gari imejaa bado anapoga kelele nje eti gari iko tupu....

nashukia manzese darajani ye kona ananilazimisha kushukia tiptop eti darajani hasimami....
Kweli mkuu,unakuta gari limejaa abiria halafu konda anapiga kelele gari nyeupe, abiria wakimwambia gari imejaa anasema gari haijai inajaa ndoo ya maji.
 
Unampa hela ya nauli anakuuliza,"una 100???"
Kama hauna unasubirishwa chenchi na usipodai hupati hiyo100
Wengine bila aibu et 100 tu unadai?

ni haki kudai mia kwa sababu ni haki yako mua nayo ni ela bna imagine naul mia 4 alafu mia imepungua konda atakuelewaaaa
mimi nadai hata kama ni hamsini
ni haki yangu hela haichumwi
over
 
Kama hana chenchi si dhambi akikuambia usubiri almradi akupatie au kama unayo mia mmpe ili akupatie mia mbili.
Mkuu kama unawahi kibaruani utakaa umsubiri konda kweli? Kazi zenyewe za macapitalist,tena ukute mhindi ndio bosi wako utakuta kavimba mashavu kama anapuliza moto vile.Itabidi ile kwake bhana ili ajifunze kutembea na chenchi za kutosha.
 
Ukimwambie asiongeze abiria wengine ndani kuna joto "anakwambia ungepanda friji"
Anakudnganya kuna siti ukipanda unakuta hamna ukimuuliza anakujibu "ungekuja na stuli toka nyumbani"

SINA IMANI NA UKAWA
 
Ukisema makonda ni wachafu nitakuunga mkono. Lakini hili la chenchi linawahusu abiria na kondakta ambao lazima tuwasemee maana muda wa kuingia humu hawana. Ni asubuhi abia wanne wanatoa noti za sh. Kumi 10 sawa na sh 40, 000 wkt nauli ni sh 500?
Sasa kwa maana hiyo nikiwa na shilingi elfu kumi asubuhi nizurure kutafuta chenchi? au nisipande daladala?kukosa kwake chenchi mimi inanihusu nini? au ni dhambi kutoa elfu kumi asubuhi kwenye daladala?
Mtu makini katika kazi yake hujipanga vyema kukabiliana na changamoto na si kulalamika lalamika.
 
Back
Top Bottom