Papa Mopao
JF-Expert Member
- Oct 7, 2009
- 4,161
- 2,668
Kuna siku nilipokuwa darasani nakumbuka ilikuwa form two, kulikuwa na mwalimu mwanamke alikuwa anafundisha Chemistry, basi siku hiyo nilichoka sana kusikiliza, nilichofanya ni kuamua kuchora, nilichukua kikaratasi(plain paper) na pen nikaanza kumchora mwalimu copyright kabisa bila ya watu kujua mpoaka michoro ya pale ubaoni na ngua hadi mandhari ya darasa, kumbe jirani yangu alicheka sana baada ya kuona namchora mwalimu darasani, aisee tangu siku hiyo watu walijua kiwango changu cha uchoraji form two hiyo.
Form III sasa, kulikuwa na kampeni ya kuwachagua viongozi, basi kuna jamaa akaniomba nimchore ili abandike picha yake kwenye notes board, nilimchora fresh akiwa amesimama na miguu yake kabisa ya kupinda kwa nyuma mrefu baada ya kumaliza, nikawauliza watu niliyemchora ni nani, wengi walicheka sana baada ya kumtambua ni nani mpaka mwenyewe hakuamini, alibandika picha kwenye notes board na kuandika jina lake, siku ya siku jamaa akatangazwa mshindi maana iliwavutia wengi kuangalia hiyo picha kitu ambacho kilimsaidia jamaa kupata ushindi. Vituko vingi nilivyovifanya kupitia uchoraji, nitaviongezea vingine baadaye. Karibuni kama mna vituko mlivyokumbana navyo katika pitapita zenu!
Form III sasa, kulikuwa na kampeni ya kuwachagua viongozi, basi kuna jamaa akaniomba nimchore ili abandike picha yake kwenye notes board, nilimchora fresh akiwa amesimama na miguu yake kabisa ya kupinda kwa nyuma mrefu baada ya kumaliza, nikawauliza watu niliyemchora ni nani, wengi walicheka sana baada ya kumtambua ni nani mpaka mwenyewe hakuamini, alibandika picha kwenye notes board na kuandika jina lake, siku ya siku jamaa akatangazwa mshindi maana iliwavutia wengi kuangalia hiyo picha kitu ambacho kilimsaidia jamaa kupata ushindi. Vituko vingi nilivyovifanya kupitia uchoraji, nitaviongezea vingine baadaye. Karibuni kama mna vituko mlivyokumbana navyo katika pitapita zenu!