Msigazi Mkulu
JF-Expert Member
- Dec 22, 2013
- 4,110
- 3,269
Karibia mwezi mzima nipo jijini Mwanza, jambo ambalo halikunifurahisha ni hili la wanafunzi au makundi ya vijana kupiga kelele njia nzima, bora hata wangekuwa wanaimba ila wao ni kelele tu wooioiii,wooo,weeee, hadi mtu unajiuliza wamepatwa na nini hawa watu, ni ushamba wa kusafiri au nini maana wanaofanya hivi ni kutoka shule za kata.
Naomba mamlaka ishukue hatua kwa kuwaagiza wakuu wa shule kusimamia safari za wanafunzi wasiwe kero kwa watu wengine, lakini pia wakumbushwe kuwa shuleni ni sehemu ya kuwajengea ustaarabu na hapo wanaonekana wamefeli kwa hilo.
Naomba mamlaka ishukue hatua kwa kuwaagiza wakuu wa shule kusimamia safari za wanafunzi wasiwe kero kwa watu wengine, lakini pia wakumbushwe kuwa shuleni ni sehemu ya kuwajengea ustaarabu na hapo wanaonekana wamefeli kwa hilo.