Taarifa za njaa: Waandishi wa vituo vya televisheni muonyesheni Rais hali halisi ilivyo

Msaidieni huyu PhD holder naona kila kitu kwake ni siasa. Hii ni serious kwani anakataa ukweli wa wazi. Kama hamna njaa Kwa nini debe la mahindi linauzwa 20'000 na gunia la mahindi 100000 hadi 120000. Atuambie hii inasababishwa na nini. Je ngombe walioonyeshwa kwenye TV wamekufa Kwa kitu Gani?
 
Tanzania ina njaa tangu enzi za mababu, tajeni ni mwaka gani ulikuwa na neema zaidi, kama Arusha mifugo inakufa kwa ukame kila mwaka sasa sijui mwaka huu nini kipya????
Ngombe hawafi kila mwaka acha Ku support ujinga na tumia akili bora unyamaze. Mimi ni mkulima pia Kwa miaka 15 Sasa. Msimu wa kilimo 2016 nililima 12 acres za yellow beans lakini mvua haikutosha na sikupata hata gunia 2 za maharage. Haijawahi tokea hivyo miaka almost 10. Na wote tuliolima mi ndio nilivuna kwani wengine waliambukia majani ya ngombe. Am talking about Arusha. Funga mdomo kama hujui
 
teh teh teh teh. nishawazoea. hata hili litapita tutasahau watasubili tukio lingine ili wapate cha kusema.

kuna tofauti kubwa kati ya njaa na ukame.
usipopika haimaanishi kwamba hutokula
Ndg inaonekana umezoea kura kwa jirani ndio maana huoni shida kutokupika si jirani yupo?
 
Kwa
Msipotoshe watu hata sisi vijijini mifugo wanakufa ni kweli lakini si mwaka huu tu hili jambo hujitokeza kila mwaka haswa ikifika kipindi cha mifugo kubadilisha majani yaani kutoka majani makavu ya kiangazi kwenda majani mabichi ya masika
Sasa isiwe habari kwamba eti ni kwasababu ya njaa huo ni unafiki msimdanganye rais
Taarifa mnazozitoa kwenye vyombo vya habari vina lengo la kupotosha ihalisia wa mambo ili matajili wanaowatuma wajinufaishe kibiashara kupitia misamaha ya kodi wezi wakubwa nyie
Kamati za maafa zipo mpaka ngazi ya kijiji wao wanawajibika kutoa taarifa kwa ngazi ya wilaya ili uchunguzi ufanyike kujua mahiyaji
Hatuwezi kutumia wandishi wa habari makanjanja kupotosha umma kwa maslahi ya wafanya biashashara
Kwa hiyo hata wale wananchi waliomsimamisha mkuu wa mkoa na kulia njaa walitumwa na matajili?
 
Hizi taarifa za njaa hata kama ni kweli wewe zinakunufaisha nini. Kama una hio taarifa basi chukua hatua binafsi na sio kuichukulia kisiasa kama unavyofanya. Magufuli yupo mpaka 2025 ije mvua lile jua. Tatuta eneo kalime! Hao wafugaji wakiuza Ng'ombe watano tu wanauwezo wa kuchimba kisima na kuweka solar wanapata maji mwaka mzima kunywesha mifugo
usiseme hivo ndugu.

ile ndoto ya mheshimiwa Lema usiipuze!
 
Hizi taarifa za njaa hata kama ni kweli wewe zinakunufaisha nini. Kama una hio taarifa basi chukua hatua binafsi na sio kuichukulia kisiasa kama unavyofanya. Magufuli yupo mpaka 2025 ije mvua lile jua. Tatuta eneo kalime! Hao wafugaji wakiuza Ng'ombe watano tu wanauwezo wa kuchimba kisima na kuweka solar wanapata maji mwaka mzima kunywesha mifugo
Mkuu ng'mbe wakishakosa chakula hukonda na hawana bei. kwanza anayenunua anawalishia wapi? pia kulima ni kujipanga si sawa na kurusha jiwe!
 
Waandishi wa habari wategemee kuweka jela kwa amri za wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa ambao habari za maeneo yao yenye njaa yakitangazwa.
 
Msipotoshe watu hata sisi vijijini mifugo wanakufa ni kweli lakini si mwaka huu tu hili jambo hujitokeza kila mwaka haswa ikifika kipindi cha mifugo kubadilisha majani yaani kutoka majani makavu ya kiangazi kwenda majani mabichi ya masika
Sasa isiwe habari kwamba eti ni kwasababu ya njaa huo ni unafiki msimdanganye rais
Taarifa mnazozitoa kwenye vyombo vya habari vina lengo la kupotosha ihalisia wa mambo ili matajili wanaowatuma wajinufaishe kibiashara kupitia misamaha ya kodi wezi wakubwa nyie
Kamati za maafa zipo mpaka ngazi ya kijiji wao wanawajibika kutoa taarifa kwa ngazi ya wilaya ili uchunguzi ufanyike kujua mahiyaji
Hatuwezi kutumia wandishi wa habari makanjanja kupotosha umma kwa maslahi ya wafanya biashashara
wapi huko sisi wafugaji tuhamie huko ambako mpaka sasa mvua zinanyesha na nyasi zipo?
 
Hizi taarifa za njaa hata kama ni kweli wewe zinakunufaisha nini. Kama una hio taarifa basi chukua hatua binafsi na sio kuichukulia kisiasa kama unavyofanya. Magufuli yupo mpaka 2025 ije mvua lile jua. Tatuta eneo kalime! Hao wafugaji wakiuza Ng'ombe watano tu wanauwezo wa kuchimba kisima na kuweka solar wanapata maji mwaka mzima kunywesha mifugo

mpaka 2025 ? duh hii hatari
 
Sitaseme mengi.

Baada ya Raisi kudai hakuna njaa,nawashauri tembeleeni maeneo mbalimbali na mchukue picha za hali ya mazao mashambani,mifugo wanaodaiwa kufa na mtembelee kwenye masoko.

Katika kupita kwenu, muhoji wakulima, wafugaji,wafanyabiashara wa mazao na wanaodaiwa kuathirika na njaa.

Vikwazo vinaweza kuwa ma-DC na ma-RC ila msisahau kuwa kila kazi ina changamoto zake.

Tulipofika tunahitaji documentary/documentaries
Hivi njaa ya mwaka huu imesababishwa na nini? je ni kweli kwa sababu ya mvua hakuna au kwa ajiri ya wabunge wetu waliruhusu mazao kuuzwa nje? ninavyojua mm ni kuwa hata kama mvua ingenyesha kama kawaida leo hii mazao yangekuwa bado shambani sasa watu wanaposema kutokunyesha mvua ya kutosha kumeleta njaa sielewi sana, ila ukiniambia kuwa kutakuwa na njaa msimu huu nitakuelewa maana hakutakuwa na mavuno ya kutosha
 
Vyovyote itavyokuwa, si jambo la kushabikia....
Nikikumbuka mahindi ya 'Yanga' najikuta naumia sana njaa ni zaidi ya utumwa na mateso....



Dunia Uwanja wa Fujo
 
Sitaseme mengi.

Baada ya Raisi kudai hakuna njaa,nawashauri tembeleeni maeneo mbalimbali na mchukue picha za hali ya mazao mashambani,mifugo wanaodaiwa kufa na mtembelee kwenye masoko.

Katika kupita kwenu, muhoji wakulima, wafugaji,wafanyabiashara wa mazao na wanaodaiwa kuathirika na njaa.

Vikwazo vinaweza kuwa ma-DC na ma-RC ila msisahau kuwa kila kazi ina changamoto zake.

Tulipofika tunahitaji documentary/documentaries

Hakuna sababu ya kufanya hivyo.
Mheshimiwa raisi ameshajibu yote.
Vituo vinavyotangaza njaa, vimenunuliwa na wafanyabiashara, njaa hakuna.
Wafugaji wanaolia mifugo inakufa kwa ajili ya ukame, wauze mifugo wapate fedha za kununulia mahitaji ya familia pamoja na chakula.
Wakulima wanaolia mavuno hakuna, walipashwa kujua mapema kwamba mwaka huu mvua hakuna hivyo wangelima mazao yanayostahimili ukame.
SERIKALI HAITATOA CHAKULA CHA MSAADA KWA MTU YEYOTE.

Ninaomba watanzania tutembee pamoja na raisi katika maono yake. Mabishano hayatatusaidia kuokoa watu wetu wanaokufa na njaa, na wala tusitegemee kuna hali yoyote inaweza kumshawishi Mheshimiwa raisi kubadili msimamo wa serikali kwa kuwa ninaamini, anachokitamka, kinakuwa kimefanyiwa uchunguzi na uchambuzi wa kina na ndiyo maana kinatangazwa kama msimamo wa serikali.

Pengine jambo ambalo ningelishauri lifanyike, Serikali sasa isaidie kutoa taarifa namna hawa Watanzanai waliozembea hadi wakapata njaa, watapata wapi chakula cha kununua. Serikali hapa ianze kuapkua chakula kutoka katika maghala yake na kuwafikishia karibu wananchi kwa utaratibu mzuri, ambapo WATANUNUA CHAKULA HICHO NA WASIDAI KUPEWA BURE KWA KUWA SERIKALI IMESEMA HAITOI CHAKULA CHA MSAADA.

Mheshimiwa raisi awawajibishe wakuu wa Wilaya katika wilaya ambazo zina njaa kwa kuwa walpashwa kujua na kuhimiza watu kulima mazao sahihi kulingana na hali ya hewa. Vinginevyo vyeo vya wakuu wa wilaya vifutwe kwa kuwa havina faida kwa taifa.
 
Mkuu umeshawahi kusikia la kuvunda halina utani?
Tuna tatizo nchini tena si dogo.

Sitaseme mengi.

Baada ya Raisi kudai hakuna njaa,nawashauri tembeleeni maeneo mbalimbali na mchukue picha za hali ya mazao mashambani,mifugo wanaodaiwa kufa na mtembelee kwenye masoko.

Katika kupita kwenu, muhoji wakulima, wafugaji,wafanyabiashara wa mazao na wanaodaiwa kuathirika na njaa.

Vikwazo vinaweza kuwa ma-DC na ma-RC ila msisahau kuwa kila kazi ina changamoto zake.

Tulipofika tunahitaji documentary/documentaries
 
Hivi njaa ya mwaka huu imesababishwa na nini? je ni kweli kwa sababu ya mvua hakuna au kwa ajiri ya wabunge wetu waliruhusu mazao kuuzwa nje? ninavyojua mm ni kuwa hata kama mvua ingenyesha kama kawaida leo hii mazao yangekuwa bado shambani sasa watu wanaposema kutokunyesha mvua ya kutosha kumeleta njaa sielewi sana, ila ukiniambia kuwa kutakuwa na njaa msimu huu nitakuelewa maana hakutakuwa na mavuno ya kutosha

Tanzanai ina misimu mbali mbali ya mavuno . Kuna sehemu wanaanza kvuna mapemba kabla ya Krismasi wakati sehemu zingine ndiyo wanapanda.

Uuzaji wa mazao ya chakula nje ya nchi unachangiwa na serikali kushindwa kuandaa masoko bora ya ndani yenye tija kwa mkulima. Aidha bei za mazao ya mkulima kutokuwiana na gharama za uzalishaji pamoja na mfumo wa ununuzi usioendana na muda wa mahitaji ya fedha kwa huyo mkulima. Bado Watanzania wanahitaji sera na uelekezi sahihi katika masuala yote.

Nitatoa mfano, mkulima anahitaji fehda za ada ya mtoto, au ana mgonjwa anahitaji matibabu, ama anahitaji kuezeka nyumba kabla ya msimu mwingine wa mvua kwa mathalani. Soko lililopo ndani linalipa fedha ndogo kwa kuwa ni wakati wa mavuno mazao yako mengi, lakini pia halipwi taslimu anakopwa kwa muda usiojulikana, na wakati wa malipo ukifika, kuakuwa na mabadiliko ya bei kwa kile kinaitwa eti kampuni imekuta bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia inakouza imeshuka. Muda wa malipo haujulikani anaweza kulipwa musimu mwingine kabisa wa mavuno.

Mkulima huyu, atawezaje kulipa ada za mwanae aende shule kwa muda muafaka? Huyo mgonjwa atamfanyaje ili afya yake iendelee kusubiri malipo ya mazao yaliyokopwa ili akatibiwe? Wakati akisubiri fehda hizo ili aenzeke nyumba, familia yake inakuw ainaishi kwa naman gani? Kabla hatujawalaumu wakulima kuuza nje mazao, ni vyema tukajiweka mahala pao kwanza.

Lakini all in all, hawa watu wentu wanahitji kula na kuishi. Wapelekewe chakula na bei idhibitiwe ili waweze kununua chakula hata kama hakitatolewa bure kama serikali ilivyotamka. Mengien yatafuata lakini tuokoe uahi wao kwanza.
 
Southern Africa Food Crisis
Published on 23 Nov 2016
Southern Africa has experienced its worse drought in years as a result of El Nino. The drought has destroyed crops and harvests leaving 28 million people in need of emergency food assistance. Malawi is one of the hardest hit countries. Maize production is down 12.4% and prices have gone up 40% in some areas. The hunger crisis could grow worse in coming months as the hard-hit countries of Malawi, Mozambique, Madagascar and Zimbabwe are entering the lean months--6.5 million people(39% of the population) will not have enough food stocks to live on in Malawi alone. CARE CEO Michelle Nunn traveled with journalist Mike Cerre to report on how the drought is impacting the people of Malawi. Learn more by visiting http://www.care.org

Source: CARE
 
January 11, 2017
Nairobi, Kenya

Several regions to experience drought: Authority

Several regions in Kenya will experience drought, according to the National Drought Management Authority.

This has been attributed to depressed rainfall during the short rains season that occurs around December in most parts of the country as a result of which several regions that experienced drought last year could not recover.

A report by the authority titled “National Drought Early Warning Bulletin”, which contains data collected up to December 26, indicated that food shortage would continue to worsen in the coming months.

Source: DailyNation November 2016
This also follows reports from the weatherman that there is no prospect of rains in the country. particularly in arid and semi-arid areas until at least March or April.

The situation is especially dire in Garissa, Isiolo, Kilifi, Lamu, Mandera, Marsabit, Samburu, Tana River, Turkana and West Pokot counties, with the agency asking authorities to be on alert for worsening conditions.

On Wednesday, Devolution and Planning Cabinet Secretary Mwangi Kiunjuri told the Nation that the government was working day and night to address the situation.

He said ministries of Devolution, Health, Environment, Treasury, Agriculture, Education and Interior would meet and a collective statement would be issued on Thursday.

“We have set up a committee to address this issue and all those relevant ministries affected have agreed to work together. We also plan to invite governors from 23 counties which are affected to come dialogue with us on Monday on how to solve the issue,” said Mr Kiunjuri.
Source: Several regions to experience drought: Authority

Source: NTV Kenya January 4, 2017
N.B
Kenya, Malawi, Mozambique, Madagascar n.k wanakabiliwa na upungufu wa mvua na hivyo tishio la njaa. Tanzania imezungukwa kijiografia na nchi hizo je ni kweli hakuna tishio la njaa?
 
Waandishi wa Aljeera na BBC ndio wanaweza kuja kufanya kipindi na kuonyesha jinsi njaa ilivyo,Natamani pia DW wafanye hivyo!
 
Tuliosema lowasa ni fisadi ni sisi Mbowe, Lisu, Lema, Mnyika, Msigwa na ushahidi tunao.

Kama Lowasa anabisha atangulie mahakamani
 
Back
Top Bottom