Taarifa za njaa: Waandishi wa vituo vya televisheni muonyesheni Rais hali halisi ilivyo

Hizi taarifa za njaa hata kama ni kweli wewe zinakunufaisha nini. Kama una hio taarifa basi chukua hatua binafsi na sio kuichukulia kisiasa kama unavyofanya. Magufuli yupo mpaka 2025 ije mvua lile jua. Tatuta eneo kalime! Hao wafugaji wakiuza Ng'ombe watano tu wanauwezo wa kuchimba kisima na kuweka solar wanapata maji mwaka mzima kunywesha mifugo
Wewe kweli hamnazo sijuwi na wewe huu uozo uliouleta hapa unakusaidia nini kwa nini na wewe usikae kimya ukamsaidia mkeo kufumua nywele zake za chrismas!acha ushabiki wakijinga au bado hujakuwa lakini ukikuwa utaacha huu ujinga wako fyusii sana wewe!!
 
Wewe kweli hamnazo sijuwi na wewe huu uozo uliouleta hapa unakusaidia nini kwa nini na wewe usikae kimya ukamsaidia mkeo kufumua nywele zake za chrismas!acha ushabiki wakijinga au bado hujakuwa lakini ukikuwa utaacha huu ujinga wako fyusii sana wewe!!

Huyu jamaa atakuwa wa kishia,anasoma bitabu vya kina shigongo eti panda matikiti utakuwa tajiri,Ccm bhana,joka jeusi
 
Kwani siku hizi yeye haoni au hasikii siku hizi?!

Mfichaficha maradhi kilio kitamfichua! Hapo atakapoanza kuomba msaada wa chakula ataficha wapi uso wake!
Unafikiri yeye hajui yote hayo? Unafikiri hajui kuwa huwezi kuficha ujauzito mchanga kwamba utakua? Rais anajua anachokisema na anachokifanya tusubiri tuone anaomba huo msaada au wananchi wanakufa kwa njaa ndio mtamuhukumu.
 
Sitaseme mengi.

Baada ya Raisi kudai hakuna njaa,nawashauri tembeleeni maeneo mbalimbali na mchukue picha za hali ya mazao mashambani,mifugo wanaodaiwa kufa na mtembelee kwenye masoko.

Katika kupita kwenu, muhoji wakulima, wafugaji,wafanyabiashara wa mazao na wanaodaiwa kuathirika na njaa.

Vikwazo vinaweza kuwa ma-DC na ma-RC ila msisahau kuwa kila kazi ina changamoto zake.

Tulipofika tunahitaji documentary/documentaries


Hawahitaji kuwa hoji bali watupie video za mashamba na hali ya mahindi/mazao yaliyomo mashambani. Mwenye akili na macho huhitaji kusubiri kuambiwa.
 
Tanzania ina njaa tangu enzi za mababu, tajeni ni mwaka gani ulikuwa na neema zaidi, kama Arusha mifugo inakufa kwa ukame kila mwaka sasa sijui mwaka huu nini kipya????
Kwa hiyo unakubali kwamba njaa ipo ingawa umeandika ukiwa na lengo la kukubaliana na Magufuli kuwa hakuna njaa.
 
Je nikweli hakuna njaa labda tuanzie hapo mkuu maana mm niko tabora watu wanakula maembe ndio chakula je waziri mkuu alikuwa anamaanisha nn kuhusu njaa au waziri mkuu anatokea cdm
Mkuu, hawa jamaa wamevurugwa. Maendeleo ya Tanzania chini ya Rais Magufuli yanawachanganha sana aiseeee
 
Msipotoshe watu hata sisi vijijini mifugo wanakufa ni kweli lakini si mwaka huu tu hili jambo hujitokeza kila mwaka haswa ikifika kipindi cha mifugo kubadilisha majani yaani kutoka majani makavu ya kiangazi kwenda majani mabichi ya masika
Sasa isiwe habari kwamba eti ni kwasababu ya njaa huo ni unafiki msimdanganye rais
Taarifa mnazozitoa kwenye vyombo vya habari vina lengo la kupotosha ihalisia wa mambo ili matajili wanaowatuma wajinufaishe kibiashara kupitia misamaha ya kodi wezi wakubwa nyie
Kamati za maafa zipo mpaka ngazi ya kijiji wao wanawajibika kutoa taarifa kwa ngazi ya wilaya ili uchunguzi ufanyike kujua mahiyaji
Hatuwezi kutumia wandishi wa habari makanjanja kupotosha umma kwa maslahi ya wafanya biashashara
Je unga kilo moja kwasasa ni sh ngapi mkuu au debe la mahindi ni sh ngapi huko kwenu
 
Kwa kawaida majanga yanapotokea wapo wanaofurahia na wengine kuhuzunika. Wapinzani katika hili la njaa ya ukame mnalitumia kisiasa zaidi kwa malengo yenu binafsi

Umeyakusanya mawazo yako vizuri kweli? au umejisikia kulopoka tu,ongea vitu vyenye fact sio kukulupuka tu kwa sababu wewe ni CCM njaa haina chama,watakaokufa ni wananchi ambao ni walipa kodi wa Tanzania,kama unahisi wapinzani wanalitumia kisiasa thibitisha basi kuwa nchi ina chakula cha kutosha na hakuna ukame.
 
Back
Top Bottom