Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake kukosekana kwa huduma ya umeme kulikosababishwa na upungufu wa kina cha maji kwenye vyanzo vyetu vya Kihansi na Pangani pamoja na hitilafu iliyotokea kwenye vituo vya Kinyerezi I na Songas leo, Jumanne, Septemba 13, 2022.
Hitilafu hii imesababisha baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar Es Salaam, Morogoro, Singida, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Njombe, Ruvuma, Songwe, Iringa, Shinyanga, Tabora, Dodoma, Geita, Mara, Manyara, na Simiyu kukosa huduma ya umeme.
Jitihada za kiufundi zinaendelea kufanyika ili kuhakikisha hitilafu iliyojitokeza inatatuliwa haraka iwezekanavyo. Aidha, tutatoa taarifa mara huduma ya umeme itakaporejea.
Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.
IMETOLEWA NA KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA, TANESCO MAKAO MAKUU.
SIMU: +255 748 550 000
Hitilafu hii imesababisha baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar Es Salaam, Morogoro, Singida, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Njombe, Ruvuma, Songwe, Iringa, Shinyanga, Tabora, Dodoma, Geita, Mara, Manyara, na Simiyu kukosa huduma ya umeme.
Jitihada za kiufundi zinaendelea kufanyika ili kuhakikisha hitilafu iliyojitokeza inatatuliwa haraka iwezekanavyo. Aidha, tutatoa taarifa mara huduma ya umeme itakaporejea.
Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.
IMETOLEWA NA KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA, TANESCO MAKAO MAKUU.
SIMU: +255 748 550 000