Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana Oktoba 16, 2014 katika siku ya kwanza ya kikao chake cha siku mbili kinachoendelea mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete imejadili na kupitisha Sera ya CCM ya kujitegemea kimapato na kiuchumi.
Sera hiyo inalenga kuwa muongozo wa kuifanya CCM ianze kuzitumia rasilimali zake kuzalisha ili iweze kujitegemea kiuchumi. Kama inavyofahamika CCM ina rasilimali nyingi wakiwemo wanachama wake, viwanja na majengo ambavyo kwa pamoja vkitumika vizuri vitasaidia kukifanya chama kuondokana na utegemezi wa ruzuku na badala yake kujitegemea.
Aidha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imefanya uteuzi wa wagombea kwa nafasi za Uenyekiti wa CCM katika wilaya mbili pamoja na wagombea Ujumbe wa NEC katika wilaya tatu zilizokuwa na nafasi wazi.
WALIOTEULIWA KUGOMBEA UENYEKITI WA WILAYA NI;-
Wilaya ya Njombe:-Ndugu Edward Pius Mgaya Ndugu Vallence Mtenzi Kabelege Ndugu Betram Simon Ngimbudzi
Wilaya ya Misenyi:-Ndugu Sosthenes Rweyemamu Kabandwa Ndugu Said Ibrahim Seruh Ndugu Erica Kiiza Stephen
WALIOTEULIWA KUGOMBEA UJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA NI:-
Wilaya ya Tandahimba:-Ndugu Lutavi Abdula Suleman Ndugu Malela Mohamed Chibwana Ndugu Nanyundu Ally Salum
Wilaya ya Mkuranga:-Ndugu Ally Mohamed Msikamo Ndugu Maulid Hamis Zowange Ndugu Wakati Nassoro Mtulia Ndugu Zawadi Ally Kilapo
Wilaya ya Njombe:-Ndugu Christian Marcus Fwalo Ndugu George Benedict Mngongo Ndugu Oscar Michael Msigwa Ndugu Justin Nusulupia
Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye, KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA, ITIKADI NA UENEZI 17/10/2014