TODAYS
JF-Expert Member
- Apr 30, 2014
- 13,773
- 21,272
Kumekuwa na matukio ya Watanzania wanaosafiri kwenda Hong Kong kuzuiliwa kuingia au kuhojiwa kwa muda mrefu na maafisa wa Idara ya Uhamiaji ya Hong Kong katika uwanja wa ndege wa Hong Kong.
Hali hiyo imejitokeza zaidi katika kipindi cha hivi karibuni tangu Hong Kong ifungue mipaka yake kuruhusu wageni kuingia baada ya miaka mitatu ya zuio la kuingia Hong Kong kwa ajili ya udhibiti wa maambukizi ya UVIKO19.
Hatua hizo za Mamlaka za Hong Kong zimetokana na matukio ya siku za nyuma ambapo watu wachache waliokuwa na passport ya Tanzania kufanya vitendo vya uvunjivu wa sheria.
Tarehe 30 Machi 2023 Ubalozi wa Tanzania nchini humo umewasiliana na Mamlaka za Hong Kong kueleza kutoridishishwa na hatua inayochukuliwa na Maofisa wa Uhamiaji wa Hong Kong kwa kila anayekuwa na passport ya Tanzania kuhojiwa kwa muda mrefu na wengine kurejeshwa walikotoka.
Mamlaka za Hong Kong zilijibu ofisi ya ubalozi wa Tanzania kwa kueleza kwamba Maafisa wao wataendelea kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kwa mujibu wa sheria za Hong Kong.
Na Wametoa rai kwa wasafiri wanaokwenda Hong Kong kuwa na nyaraka zote zinazohitajika, hususan sababu ya wewe kuingia Hong Kong.
Ubalozi wa Tanzania unatoa rai kwa Watanzania wenye safari ya kwenda Hong Kong wahakikishe kuwa na nyaraka zote muhimu kama zifuatazo:
1) Barua ya Mwaliko kutoka kwa Mwenyeji wa abiria anayekwenda Hong Kong- ambaye anaweza kuwa mtu binafsi au kampuni;
2) Tiketi ya ndege yenye kuonesha tarehe ya kuondoka Hong Kong;
3) Booking ya Hoteli inayoonesha jina la msafiri, tarehe ya kuingia na kutoka;
Na muhimu zaidi, kuepuka kuvunja sheria za Hong Hong kwa kubeba vitu/bidhaa ambazo ni kinyume na sheria.
Vitendo hivyo vitazidi kuchagua taswira ya nchi na kuwaathiri watanzania wengine wengi wanaofuata sheria ambao wangependa kwenda Hong Kong.
Aidha, Ubalozi unashauri watanzania ambao wanakwenda China (Mainland) watumie usafiri wa kwenda moja kwa moja katika miji ya China badala ya kupitia Hong Kong ili kuepuka usumbufu.
Hali hiyo imejitokeza zaidi katika kipindi cha hivi karibuni tangu Hong Kong ifungue mipaka yake kuruhusu wageni kuingia baada ya miaka mitatu ya zuio la kuingia Hong Kong kwa ajili ya udhibiti wa maambukizi ya UVIKO19.
Hatua hizo za Mamlaka za Hong Kong zimetokana na matukio ya siku za nyuma ambapo watu wachache waliokuwa na passport ya Tanzania kufanya vitendo vya uvunjivu wa sheria.
Tarehe 30 Machi 2023 Ubalozi wa Tanzania nchini humo umewasiliana na Mamlaka za Hong Kong kueleza kutoridishishwa na hatua inayochukuliwa na Maofisa wa Uhamiaji wa Hong Kong kwa kila anayekuwa na passport ya Tanzania kuhojiwa kwa muda mrefu na wengine kurejeshwa walikotoka.
Mamlaka za Hong Kong zilijibu ofisi ya ubalozi wa Tanzania kwa kueleza kwamba Maafisa wao wataendelea kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kwa mujibu wa sheria za Hong Kong.
Na Wametoa rai kwa wasafiri wanaokwenda Hong Kong kuwa na nyaraka zote zinazohitajika, hususan sababu ya wewe kuingia Hong Kong.
Ubalozi wa Tanzania unatoa rai kwa Watanzania wenye safari ya kwenda Hong Kong wahakikishe kuwa na nyaraka zote muhimu kama zifuatazo:
1) Barua ya Mwaliko kutoka kwa Mwenyeji wa abiria anayekwenda Hong Kong- ambaye anaweza kuwa mtu binafsi au kampuni;
2) Tiketi ya ndege yenye kuonesha tarehe ya kuondoka Hong Kong;
3) Booking ya Hoteli inayoonesha jina la msafiri, tarehe ya kuingia na kutoka;
Na muhimu zaidi, kuepuka kuvunja sheria za Hong Hong kwa kubeba vitu/bidhaa ambazo ni kinyume na sheria.
Vitendo hivyo vitazidi kuchagua taswira ya nchi na kuwaathiri watanzania wengine wengi wanaofuata sheria ambao wangependa kwenda Hong Kong.
Aidha, Ubalozi unashauri watanzania ambao wanakwenda China (Mainland) watumie usafiri wa kwenda moja kwa moja katika miji ya China badala ya kupitia Hong Kong ili kuepuka usumbufu.