Swali la ufahamu: Hivi CCM hutoa taarifa ya mikutano ya hadhara au/na maandamano yao kwa Jeshi la Polisi?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Waungwana wa JF, husikeni na mada ya hapo juu.

Nikiri wazi kuwa katika kufuatilia kwangu siasa za Tanzania kupitia redio, magazeti, runinga na mitandao ya kijamii, sijawahi kuona au kusikia kuhusu barua iliyowasilishwa na CCM kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) waweze kuendesha maandamano ya amani au mikutano ya hadhara kwenye wilaya husika.

Imekuwa kawaida kusikia na kuona vyama vya upinzani vikiandika barua ya kutoa taarifa kwa OCD kwa ajili ya mambo hayohayo. Kuna wakati taarifa hiyo huridhiwa na upo wakati taarifa hiyo hairidhiwi kutokana na sababu za kiusalama almaarufu kama taarifa za kiintelijensia.

Je, CCM hukidhi matakwa ya kisheria na kikanuni katika kutoa taarifa Polisi? CCM wamewahi kutoridhiwa kufanya maandamano ya amani au mkutano wa hadhara?
 
Je, CCM hukidhi matakwa ya kisheria na kikanuni katika kutoa taarifa Polisi? CCM wamewahi kutoridhiwa kufanya maandamano ya amani au mkutano wa hadhara?
Ccm hawatoi taarifa mkuu.
Hii ni kwa sababu policcm ni taasisi mojawapo ya ccm ingawa hili ni kinyume na Katiba ya nchi.

Kuna mtu alisema: "..some people are more equal than others"
 
Waungwana wa JF, husikeni na mada ya hapo juu.

Nikiri wazi kuwa katika kufuatilia kwangu siasa za Tanzania kupitia redio, magazeti, runinga na mitandao ya kijamii, sijawahi kuona au kusikia kuhusu barua iliyowasilishwa na CCM kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) waweze kuendesha maandamano ya amani au mikutano ya hadhara kwenye wilaya husika.

Imekuwa kawaida kusikia na kuona vyama vya upinzani vikiandika barua ya kutoa taarifa kwa OCD kwa ajili ya mambo hayohayo. Kuna wakati taarifa hiyo huridhiwa na upo wakati taarifa hiyo hairidhiwi kutokana na sababu za kiusalama almaarufu kama taarifa za kiintelijensia.

Je, CCM hukidhi matakwa ya kisheria na kikanuni katika kutoa taarifa Polisi? CCM wamewahi kutoridhiwa kufanya maandamano ya amani au mkutano wa hadhara?
Ukishakuwa na chama kilichokaa muda mrefu madarakani tena kwa shuruti, ni nadra sana chama hicho kufuata Sheria kama ipasavyo, hasa zile Sheria zinazokibana. Na kwa bahati mbaya utakuta taasisi zote za kimamlaka ni sehemu ya mfumo mbovu wa chama hicho. Ccm inaweza kuwa inaomba kibali lakini sio kwa kubembeleza, bali ni kufuata kanuni tu, na hawahojiwi dhamuni la mikutano Yao.
 
Back
Top Bottom