Swali kuhusu bosi mpya wa TPDC

Swali kuhusu bosi mpya wa TPDC

HNIC

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2011
Posts
1,898
Reaction score
2,199
Hivi huyu jamaa analipwa mshahara kiasi gani?

Na inawezekana vipi akawa anatumia milioni 70 za walipa kodi kila mwezi kwenda kutazama familia yake USA na kurudi?

Kwanini anatumia muda mrefu zaidi USA kuliko ofisini kwake?

Cha ajabu toka apewe hiyo kazi hakuna lolote la maana alilolifanya mradi wa mtambo wa LNG wa dola bilioni 25 na ushee huko Mtwara ushakwama kwa sababu watu wamekula pesa za viwanja na kesi za ajabu ajabu zimefunguliwa.

Mbaya zaidi huyu jamaa amebatizwa jina pale ofisini kwake wanamwita CAPTAIN AMERICA na wengine wanamwita MSAFIRI. Hivi haoni wenzake kama bosi mpya wa TCRA wanavyofanya kazi?

Halafu Magufuli ana tafuta wachawi wakati wapo wazi wazi.
 
Siku zote kokoro linaharibu samaki wadogo na mazalia yake
 
Tutaivamia na kuigufuli hii office karibuni na tumkute hayupo na yupo huko America!
Ticket yake itakuwa cancelled na hatorejea tena ofisini.
 
Kama kweli kaingia juzi juzi mbona mna haraka? Mmepati mtu ambaye anategemea mshahara mzuri sio rushwa sasa mafisadi wana haha
 
Mil 70 kwa mwezi kwa kusafiri? Mkataba wake 2a kazi unasemaje kuhusiana na hizo safari?
Nani aliyekula pesa za viwanja? Je walikuwa wanalipa wao au wizara husika?
 
Mkuu masuala ya la Wakurugenzi wa Kuu kufuja pesa kwenye safari za nje zisizo na tija kwa Taifa lipo kwenye baadhi ya Mashirika ya Umma nchini yakiwemo Crop Boards specifically Shirika la SUKARI - Dk.Magufuli lifatilie kwa karibu Shirika hilo - zao la SUKARI ni Political Commodity kuna madudu mengi pale.
 
Dr James mataragio nguli wa mafuta na gesi duniani tumemtoa wenyewe huko usa alipokuwa anafanya kazi
Hawa ndio akina balali, ndulu type
 
Tatizo wana JF mnapost mada isiyokuwa na chanzo cha habari (source). Huyo Boss mpya wa TPDC ni nani? Mimi namjua Yona Kilighane kama ameingia Mzungu tueleze mtoa mada.
 
Ni vizuri kuweka specific data za matumizi yake.. Mfano hiyo 70mil kwa safari moja ya US is a hell lot of money.
Weka vielelezo mkuu.
 
Na imani ulimaanisha billion 25 za kitanzania na sio dolla billion 25
 
Sioni kama kuna ukweli hapa...pesa kiasi hicho kinatumikaje kwa safari tu? Halafu kwa taratibu za kiserikali Mkurugenzi kama yule alisafiri lazima atoe taarifa kwa Katibu Mkuu wake na aeleze nia na madhumuni ya safari.... Kuhusu mradi wa LNG na mm naungana na huyu mwingine alieuliza kwani suala la ardhi ni la Tpdc pia? Sio kwamna kuna wizara husika? Na kama kuna watu wamekula pesa hizo si kuna auditing ya CAG inafanyika kwa taasisi za umma kila mwaka? Tusome hizi ripoti tujue ukweli
 
Huu ni unafiki namajungu kujaribu kuhaibu watendkazi wazuri, wewe ni sawa na mchawi huyu jamaa anajulianani kichwa asiyejivuna wala majungu. Watanzania tuachane na kupaka matope watu wasio na matatizo
 
Acheni unafiki, mtu hana hata mwaka kazini mlitaka afanyeje.

Yule bwana anafanya kazi kitaalam,ni msomi wa kiwango cha dunia,mambo ya kiswahili hawezi.

Ndugu unakula mezani pake nini maana huu Ujinga ulioandika nitashangaa ikiwa hushiriki japo makombo yake...Kwaakili yako kusafiri ndio kufanyakazi?....alaaniwe Mchina kule vitu vya electronic vya bei rahisi kila MTU anatumia kuandika bila kufikiria
 
Back
Top Bottom