Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Umoja wa Kisovieti (USSR au CCCP) taifa lililozaliwa mwaka 1914-1991,
Lilikuwa ni moja ya taifa lenye nguvu sana duniani lakini lenye mwisho mbaya sana ambao ni aibu kwa watu wake mpaka leo. Kiuchumi walikuwa wana nguvu sana, kiteknolojia walikuwa mbele, nguvu kubwa ya viwanda, kijeshi walikuwa mbele na mifumo yao ya kitamaduni iliyotokana na ukomunisti ilishawishi dunia kuanzia barani Marekani, Asia hadi Afrika na kubwa ziadi walikuwa na idadi kubwa sana ya watu ambapo takwimu zinasema kwamba walikuwa ni milioni 293.


Lakini baada ya kusambaratika nchi hii ilipoteza kila kitu ambacho ilikuwa nacho kuanzia Idadi ya watu, jeshi, viwanda na teknolojia maana kila nchi iliondoka na watu wake, majeshi yake na sehemu kama Ukraine ikapata viwanda vya bure kabisa, Poland na Georgia nao hawakuwa nyuma kabisa. Ikawa nchi dhaifu na masikini kweli....

Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ???

CC: chige , FisadiKuu
Russia licha ya kusambaratika lakini bado ana hazina kubwa ya Nyuklia duniani na bado ana Spheres of influence ambazo inajikuta mara kwa mara kimasirahi anazozana na nato....

Kuanguka kwa Ussr haikumaanisha ndio kaanza 0.....

chukulia mfano mzuri wa anguko la Britain as super power lakini bado ana sphere of influence kubwa tu......

Bahati mbaya kwa Russia ni bado ana migongano na Nato kimasirahi kuanzia Ukraine, Black Sea na pia Military alliance na China Pakistan nk
 
Russia licha ya kusambaratika lakini bado ana hazina kubwa ya Nyuklia duniani na bado ana Spheres of influence ambazo inajikuta mara kwa mara kimasirahi anazozana na nato....

Kuanguka kwa Ussr haikumaanisha ndio kaanza 0.....

chukulia mfano mzuri wa anguko la Britain as super power lakini bado ana sphere of influence kubwa tu......

Bahati mbaya kwa Russia ni bado ana migongano na Nato kimasirahi kuanzia Ukraine, Black Sea na pia Military alliance na China Pakistan nk
Good Observation,
Lakini Spheres of Influence za Urusi ya leo ni zipi hizo ?? Pia una uhakika kwamba Urusi na Pakistani wana ushirika wa kijeshi (Military Alliance)??
 
Good Observation,
Lakini Spheres of Influence za Urusi ya leo ni zipi hizo ?? Pia una uhakika kwamba Urusi na Pakistani wana ushirika wa kijeshi (Military Alliance)??
Kama umezisikiliza hotuba za Putin au waziri wa mambo ya nje wa Urusi....Sphere of influences za Urusi ni Nchi mwanachama wa Former USSr ambazo USA anajaribu zishawishi ziingie NATO au ziwe na sera kinyume na URUSI

Mfano Georgia Na Ukraine nk

Chinese Russia na Pakistan wana informer alliance ambayo in nature ni Anti American mfano inasemekana kuwa China kuna muda alikuwa anaisaidia Pakistan kuzi Shot down Drone za marekani zilizookuwa zina operate North Pakistan kuwa hunt Taliban.......na pia vyanzo vingine vinasema Taliban hupata sapoti pia kutoka kwa Russia.
 
Umoja wa Kisovieti (USSR au CCCP) taifa lililozaliwa mwaka 1914-1991,
Lilikuwa ni moja ya taifa lenye nguvu sana duniani lakini lenye mwisho mbaya sana ambao ni aibu kwa watu wake mpaka leo. Kiuchumi walikuwa wana nguvu sana, kiteknolojia walikuwa mbele, nguvu kubwa ya viwanda, kijeshi walikuwa mbele na mifumo yao ya kitamaduni iliyotokana na ukomunisti ilishawishi dunia kuanzia barani Marekani, Asia hadi Afrika na kubwa ziadi walikuwa na idadi kubwa sana ya watu ambapo takwimu zinasema kwamba walikuwa ni milioni 293.


Lakini baada ya kusambaratika nchi hii ilipoteza kila kitu ambacho ilikuwa nacho kuanzia Idadi ya watu, jeshi, viwanda na teknolojia maana kila nchi iliondoka na watu wake, majeshi yake na sehemu kama Ukraine ikapata viwanda vya bure kabisa, Poland na Georgia nao hawakuwa nyuma kabisa. Ikawa nchi dhaifu na masikini kweli....

Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ???

CC: chige , FisadiKuu
Nature mtaalamu.Nature ya hawa watu,inawabeba hta baada ya kusambaratika wana nature ya ubabe.
Cha pili ni mfumo.mfumo wa kikomunisti ni moja ya mifumo thabiti long term.ingawa short term haikuinesh faida.long term iliwajenga kidogkidogo.
 
Usumbufu unaoletwa na Urusi ni sawa na ule wa kunguni au chawa tu kwa binadamu. Sababu za usumbufu huo ni tatu:

1. Urusi tofauti na USSR imegeuka kuwa "rogue state" isiyo na lengo kuu la kimfumo (strategic objective) zaidi ya kuwepo tu (mere survival/existence). USSR ilikuwa na lengo la kuigeuza dunia nzima kuwa ya kikomunisti kwa misingi la Marx/Lenin. Hiyo ilishindikana, USSR ikasambaratika na kupoteza ushawishi huo duniani kote. Leo hii Urusi inaongozwa na kikundi maslahi kilichokumbatia madaraka na kugawana fursa za kibepari kwa kubebana (cronyism & patronage). Ukomunisti ulishatupiliwa mbali; sasa ni ma-oligarchs tu yanayojuana na Kremlin. Kikundi hiki kinajua kabisa kuwa maslahi yake yanategemea Marekani na Ulaya. Huko ndiko kwenye uhakika wa uchumi wake. Leo hii nenda Central London utakuta wamiliki wakubwa wa ardhi na mali ni kutoka Urusi/Ukraine. Wamewekeza kweli huko Marekani na Ulaya. Hivyo kila wakati wanahangaika kuhakikisha watu rafiki (sympathetic) (Trump & co.) wanakuwa madarakani.

2. Muhimu sana hawa wahuni (akina Putin) wamerithi rasilimali nzito za kiteknologia ikiwa ni pamoja na za nyuklia, ardhi, maliasili na mifumo ya elimu ya hali ya juu toka USSR. Na hapo wanajitahidi sana kutoa upendeleo kwa watu wao wenye kuweza kuziendeleza rasilimali hizo ili wazitumia kupambana na Marekani na Ulaya. Kule kuwepo kwa miundombinu ya uhakika ya nyuklia na sayansi za anga ni kinga/tishio (deterrence) tosha kwa yeyote atakayefikiria kupambana na Urusi. Tena wakiwa "rogue state" hawajali hata kutoa mhanga idadi kubwa ya watu wao kwa maslahi ya kikundi tawala kilichopo Kremlin. Tofauti na Marekani na Ulaya ambao watu wao wana thamani kubwa sana, wanaojali maisha bora kwa kila mtu na kuna mifumo thabiti ya kusimamia haki za binadamu. Marekani wakijua wanapambana na "wehu" si rahisi kuwavamia Warusi huko Crimea, Syria na kwingineko bila kujihakikishia kutozuka vita ya nyuklia!

3. Marekani na Ulaya ni jamii zilizo wazi (open societies). Mambo yao ni hadharani. Marais wao wakifanya faulo wanapashwa hadharani. Wanachunguzwa hadharani (Robert Mueller on Russian collusion). Wateule wa Rais wanapigwa interview hadharani. n.k. Kwa urusi, hiyo ni sawa na kuanika nguo zao za ndani hadharani. Rais wao (Putin) ni sawa na mungu! Athari zake ni kuwa watu hatari wanapata mianya kibao ya kuendesha uhalifu Marekani na Ulaya. Warusi wanatumia fursa hiyo kujaribu kuhujumu nchi za jumuia ya NATO. Marekani na Ulaya wanalijua hilo lakini hawako tayari kujifungia ndani kama Urusi. badala yake wanajiimarisha kitaaluma kukabiliana na chokochoko za Urusi na wahuni wengine. Na kwa kweli wamefanikiwa. Karibu harakati zote za Warusi wanazijua. Kuna wakati wanajifanya hawana uhakika ili kuwaingiza kwenye mitego.

Akina Putin wanajua vizuri sana kwamba hawaiwezi Marekani na washirika wake wa Ulaya. Kwanza, huko ndiko wanakohifadhia utajiri wao wa kifisadi. Ndiko wanakosomeshea watoto wao na ndiko ambapo kila Mrusi aliyefanikiwa anaotea kuwa na makazi na kumiliki mali kama ilivyo kwa watu wengine wa dunia ya tatu. Kitu nachoamini ni kuwa Urusi wangekuwa na viongozi wenye maono ya hali ya juu, kwa uwezo na rasilimali walizo nazo, wangekuwa tishio sana kwa washirika wa NATO. Bahati mbaya, wanaongozwa na watu wenye tamaa ya mali, madaraka na sifa (ujiko) bila falsafa kuu ya taifa. Watu ambao wanategemea kubebwa na miundombinu iliyowekwa na USSR ambayo sujui kama wataweza kuiimarisha ishindane na ya magharibi huko mbeleni.
Si kweli
 
dah mkuu nyote kwa umoja wenu mbarikiwe sana,tunawafuatili na kuwafurahia sana,asanteni sana kwa niaba ya wenye shukrani.
Asante sana Mkuu taamu,kwa baraka zako ,lakini kiukweli hii mijadala inapanua sana ufahamu wa mambo kwa sababu tun ashirikishana,na mimi pia najifunza toka kwa wengine ikiwa ni pamoja na wewe,hata hivyo mambo haya tunayapata kwa kusoma kutoka majarida na makala mbalimbali,kutazama na kusikiliza habari za dunia, kusikia kwa walioshuhudia ,kushuhudia sisi binafsi,na udadisi binafsi .Wewe ni mdau mkuu.
 
1. Lakini sasa mbona leo hii Kremlin inahangaika sana kujaribu kuziweka jirani nchi zile zilizojitoa kwenye muungano wakati KGB na Politburo ya CPSU ndiyo iliamua kuua muungano wao ???

2. Hao KGB walivyokuwa wanavunja muungano hawakutabiri kwamba kutakuwa na madhara makubwa sana kiulinzi huko mbeleni ???

NB: Basi kama KGB walifanya hivyo nadhani kuna hatihati siku watafanya tena wakichoka.....
Kuvunja muungano sio maana kuwa maadui,nadhani RF bado anawahitaji sana hawa Wasoviet wa zamani na wao bado wanamhitaji sana RF,kumbuka kuwa nchi nyingi sana za kisovieti ama zina raia wanaoongea kirusi ama raia wa urusi.
KGB ya sasa inawahitaji sana hawa wasovieti kwa sababu za kiuchumi na kuilinzi lakini muungano sio lazima.Ni kama vile USA anavyozihitaji nchi za South ama Latin Amerika.
 
Kuna uwezekano kuwa vita ya Afghanistan na vita baridi vilidhoofisha sana uchumi kiasi kwamba nchi yao ingeweza hata kuvamiwa ilibidi "wazee" wafanye "bluff" kabla mambo hayajaharibika zaidi.

Katika kufanya hivyo wakaona wavunje muungano na kumuweka mlevi (Yeltsin) ili kuudanganya ulimwengu kuwa wao sio watu wakuchukuliwa 'serious' huku teyari wakiwa na mtu wao (Putin) au wewe unasemaje kuhusu maneno haya ya Sun Tzu "All warfare is based on deception."
Perestroika na Glasnosk,mageuzi na kujitazama,waliamua kupunguza matumizi baada ya wao kama vile Marekani kuwa na makambi dunia nzima kwa ajili ya ulinzi.Hata hivyo vita ya Afghan na USSR ni kama vile USSR alikua anapigana na NATO na nchi za Kiislam indirect,kwa sababu US, na baadhi ya nchi za NATO pamoja na mataifa ya kiislam Pakistani ,Saud Arabia yalikua yanawapa MUJAHEDEEN silaha ,ushauri vifaa na fedha.Ndani ya Mujahidini ndo walikuwamo Mullah, Osama,Abdul rashid Dostum,Sheikh Masound n.k.Hawa ni baadhi ya wababe waliopambana na USSR kwa msaada wa Marekani na wapammbe wake.
 
huyu malcolm lumumba huyu dah, safi sana mkuu kama ulisoma ulisoma kweli kweli,karo ya aliyokusomesha ilienda kihalali.
Mkuu taamu,kiukweli huyu Malcolm ni kisima cha elimu humu JF,huyu kama tungempata na jembe mwingine anaitwa DOTWORLD jukwaa hili hunoga sana,pamoja na wadau wengine wapo humu wanafuatilia mjadala unavyotililika tu.
 
Dunia hii hata Zanzibar tu ikiwa na silaha isiyozuilika na yoyote na inafika kokote itaingia G7. Nadhani nuclear power na uongozi imara wa Putin umeipa heshima na fursa ya kunawiri na maeneo mengi.
 
Mkuu umeandika vizuri sana.Ila mimi nin swali dogo tu hapo kwenye paragraph yako ya mwisho kuhusu uchumi na Demokrasia,ulipozilinganisha India na China.Tunafahamu kuwa nchi hizo mbili zipo tofauti sana,nchi zimeundwa katika mifumo tofauti zikiwa na jamii tofauti. Kwa mfano wako huo wa demokrasia/rushwa na maendeleo kwa nini usilinganishe nchi ambazo zina historia sawa ? Kwa mfano linganisha South Korea na North Korea. Zote roughly the same size,jamii ni ile ile,geographic location almost identical,mtawala alikuwa mmoja na uhuru ulipatikana wakati mmoja na mtawala wao alikuwa mmoja.Tofauti ni kwamba South kuna democrasia na uwazi (ndo maana wamemfunga Park Geun-hye) kwa rushwa.
South korea chini ya rais park(baba wa rais aliyejiuzulu) ilikuwa ni nchi ya kidikteta na ndiye aliyesababisha uchumi wa korea kusini kukua.
 
Mkuu taamu,kiukweli huyu Malcolm ni kisima cha elimu humu JF,huyu kama tungempata na jembe mwingine anaitwa DOTWORLD jukwaa hili hunoga sana,pamoja na wadau wengine wapo humu wanafuatilia mjadala unavyotililika tu.
ndio mkuu apewe haki yake akisikia na akiwa hai na mwenye nguvu,amebarikiwa na sio mchoyo.
 
Asante sana Mkuu taamu,kwa baraka zako ,lakini kiukweli hii mijadala inapanua sana ufahamu wa mambo kwa sababu tun ashirikishana,na mimi pia najifunza toka kwa wengine ikiwa ni pamoja na wewe,hata hivyo mambo haya tunayapata kwa kusoma kutoka majarida na makala mbalimbali,kutazama na kusikiliza habari za dunia, kusikia kwa walioshuhudia ,kushuhudia sisi binafsi,na udadisi binafsi .Wewe ni mdau mkuu.
like
 
Hichi ulichokizungumzia hapa kinaitwa The Heartland Theory au Nadharia ya moyo wa dunia.
Iliandikwa mara ya kwanza kabisa na mwanasayansi wa siasa kutoka Uingereza aitwaye Sir Halford MckKinder ambaye mwaka 1904 alisema kwamba kama taifa litafanikiwa kutawala eneo la Ulaya Mashariki na Asia (Eurasia) basi litatawala Ulaya yote na Asia. Aliyaandika haya kwenye chapisho lake liitwalo The Geographical Pivot of History na akasema kutokana na utajiri wa rasilimali wa eneo hilo taifa lolote litakalotawala Ufalme wa Urusi basi linaweza tawala dunia.


Ikumbukwe Urusi ndiyo nchi inayoongoza kwa wingi wa rasilimali zenye thamani ya dola za kimarekani trilioni 75. Marekani na ujanja wake wote ana rasilimali zenye thamani ya dola za kimarekani trilioni 4, hivyo Urusi kama ikisambaratika nchi nyingi za Ulaya zinaweza kunufaika sana na utajiri wake.

Wanahistoria wanaamini kwamba moja ya sababu kubwa za Adolf Hitler kuvamia Urusi mwaka 1941 kabla ya nchi nyingine zote ni kwasababu Wanazi waliamini kwenye The Heartland Theory kwamba kama watampiga Urusi mapema basi watatumia rasilimali zake zote kuipiga dunia yote na ndiyo maana mataifa ya Ulaya na Marekani ikabidi watume msaada wa kipesa kwa Urusi. Hata baada ya vita ya dunia kuisha, Vita Baridi ilichangiwa sana na hii nadharia ambayo Waingereza na Wamarekani iliwakaa sana kichwani.



Tatizo la Urusi la anguko la Urusi ya Kisovieti lilikuwa siyo kusaidia mataifa mengine lakini mfumo wake mbovu na kukataa kubadilika kwa viongozi wa Kisovieti hasahasa wale kama Leonid Brezhnev. Tukisema kwamba tatizo ni kusaidia mataifa mengine tutakuwa tunasahau kitu cha muhimu sana kwamba hata Marekani naye alisaidia sana mataifa mengi sana duniani tena kwa nguvu nyingi sana kuliko hata Urusi.
Wakati Urusi alikuwa ana washirika wa Kijeshi wa Ulaya tu kupitia The Warsaw Pact, Marekani alikuwa na washirika wa kijeshi dunia nzima Kuanzia NATO, ANZUS, SEATO hadi CENTO. Mpaka leo Marekani ana mikataba ya ulinzi kama 60 hivi.


Misaada ya kiuchumi wote walitoa huku Marekani akianza na The Marshal Plan huku wasovieti wakija na The COMECON. Wote walisomesha watu huko Harvard, Yale, Moscow State University na University of St.Petersburg lakini Urusi aliachwa mbali sana. Kwanini ?? Mfumo mbovu wa kiuchumi au kuruhusu serikali kutawala uchumi kwa kila kitu (Command or Centralization of Economy). Uchumi wa Urusi haukuruhusu ushindani wa ndani ya nchi, wakati Marekani makampuni binafsi yalikuwa yanazalisha bidhaa na kupunguzia serikali mzigo. Uchina chini ya Deng Xiapoing waligundua hili mapema ndiyo wakaryuhusu mfumo wa masoko utawala nchi. Hivyo hapa sikubaliani na wewe kidogo mkuu wangu kwasababu kama kusaidia wote walisaidia mataifa ya nje kwa sana tu.



Hapa nakubaliana na wewe kwamba Urusi alikuwa na nguvu sana hadi kutanua lile eneo lake lote. Alifanya hivyo kwenye Vita Baridi ya kwanza aliyopigana na Muingereza tokea mwaka 1813 hadi 1907 ambayo iliitwa kama The Great Game au The Tournament of Shadows. Lakini naomba nikukosea kidogo hapo uliposema Marekani alikuwa hana nguvu: Nifahamuvyo mimi mpaka kufika mwaka 1916 Ujerumani alikuwa ameshashinda vita ya kwanza ya dunia na Muingereza alikuwa anajiandaa kusalimu amri, lakini aliyebadilisha mwelekeo ule wote ni Marekani chini ya Prof. Woodrow Wilson.

Mbali na hapo ikumbukwe kwamba Ujerumani alipanga kumvamia Marekani mwaka 1897 na Mfalme Kaiser Wilhelm alimtuma Ebenhard Von Mantey kupanga uvamizi kwa kutuma vikosi 100,000 lakini mpango huu ulikufa baada ya Marekani kuonesha nguvu zake kwa kumtwanga vibaya Mhispania kwenye vita ya mwaka 1898 (The Spanish American War)na kumnyang'anya CUBA na makoloni yake muhimu. Hapa utasemaje Marekani alikuwa hana nguvu ???

Unahisi Uingereza angeshinda Vita ya kwanza ya dunia dhidi ya Ujerumani bila Marekani kuingilia kati ?
Pia tusisahau kwamba Urusi ilisalimu amri mapema sana kutoka kwa Ujerumani wakati wa vita ya kwanza ya dunia hadi wakina Lenini wakasaini Mkataba wa hovyo kabisa wa Brest-Litovsk ambao ulikubali kumruhusu Ujerumani achukue sehemu za Urusi kama Poland, Estonia, Finland, Latvia, Ukraine na Lithuania. Bila Marekani kuingia kwenye vita uandhani haya maeneo yangerudi kirahisi ?


CC: Wick , muyovozi , MASAMILA , neo1
Nimeelimika sana hapa
 
Kama umezisikiliza hotuba za Putin au waziri wa mambo ya nje wa Urusi....Sphere of influences za Urusi ni Nchi mwanachama wa Former USSr ambazo USA anajaribu zishawishi ziingie NATO au ziwe na sera kinyume na URUSI
Mfano Georgia Na Ukraine nk
Sawa kabisa mkuu uko sawa,
Lakini unadhani ni sawa kabisa kwa hatma ya nchi ndogo kuamuliwa na mataifa makubwa ???

Chinese Russia na Pakistan wana informer alliance ambayo in nature ni Anti American mfano inasemekana kuwa China kuna muda alikuwa anaisaidia Pakistan kuzi Shot down Drone za marekani zilizookuwa zina operate North Pakistan kuwa hunt Taliban.......na pia vyanzo vingine vinasema Taliban hupata sapoti pia kutoka kwa Russia.
Nadhani Urusi na Pakistan wanashirikiana tu, lakini hawana umoja wa kujihami kijeshi. Nazungumza hivi kwasababu ya mahusiano makubwa ya Kihistoria baina ya India (Adui mkubwa wa Pakinstan) na Urusi. Nakumbuka vita ya mwaka mwaka 1971 baina ya India na Pakistan USSR alikuwa upande wa India huku Uchina akiwa upande wa Pakistan. Pia miaka 1970's Pakistan aliwasaidia sana Wamarekani na Mujahedeen kuua maelfu ya Warusi nchini Afghanistan. Hawa ni washirika tu lakini hawana umoja: Mwaka 2001 Iran ndiyo ilimsaidia Marekani kuvamia Afghanistan na kuwatoa Taliban lakini mwaka 2003 wakawa maadui.

NB: Huu ni ushirika wa kimaslahi tu na utapita....
 
Nchi yetu ya Tanzania ifanye nini ili iweze kuwa na kinu japo kimoja cha nyuklia?
Maendeleo huletwa na viongozi sababu wao ndio wenye maamuzi je unaona akina bashite jiwe wana weza kukuvusha mto wenye mamba wenye njaa kama ndio basi tuna weza kama hapana ujuwe ndio hivyo tena! sikio la kufa halisikie dawa Afrika tumesha tekwa tunaendeshwa kwa remote control!
kama dawa za kututibu tunatengenezewa na watu wenye matamanio na rasilimali zetu mkuu chanjo wana tupa wao toka tukiwa wadogo tusubiri kufa tu mkuu sisi ni simba wanao fugwa !
Huko Syria wamezima channel za YouTube za serekali sinazo onyesha mambo yanayo endelea huko Dunia ni kiza ila mchana upo!
 
Umoja wa Kisovieti (USSR au CCCP) taifa lililozaliwa mwaka 1914-1991,
Lilikuwa ni moja ya taifa lenye nguvu sana duniani lakini lenye mwisho mbaya sana ambao ni aibu kwa watu wake mpaka leo. Kiuchumi walikuwa wana nguvu sana, kiteknolojia walikuwa mbele, nguvu kubwa ya viwanda, kijeshi walikuwa mbele na mifumo yao ya kitamaduni iliyotokana na ukomunisti ilishawishi dunia kuanzia barani Marekani, Asia hadi Afrika na kubwa ziadi walikuwa na idadi kubwa sana ya watu ambapo takwimu zinasema kwamba walikuwa ni milioni 293.


Lakini baada ya kusambaratika nchi hii ilipoteza kila kitu ambacho ilikuwa nacho kuanzia Idadi ya watu, jeshi, viwanda na teknolojia maana kila nchi iliondoka na watu wake, majeshi yake na sehemu kama Ukraine ikapata viwanda vya bure kabisa, Poland na Georgia nao hawakuwa nyuma kabisa. Ikawa nchi dhaifu na masikini kweli....

Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ???

CC: chige , FisadiKuu

La msingi unalotakiwa kuelewa ni kwamba hiyo iliyoitwa USSR au CCCP ilikuwa na tafsiri moja tu kuwa ni URUSI. Umoja kama unaoufikiri wewe haukuwepo.

Mfano mwepesi wa kueleweka ni hivi: URUSI katika umoja huo ilikuwa ni kichwa cha Treni, nchi nyingine washirika zilikuwa ni mabehewa tu yaliyovutwa na kichwa.

Kichwa kilipojikata mabehewa yakasimama na kukodi injini za mapajero kuvivuta. Kwa hiyo kichwa cha Treni ndicho kinachotazamana na NATO. Hapo unategemea nini?

Jingine la muhimu kwako kuelewa ni kwamba vile vyama vya kibaguzi vinavyokuwa Ulaya vinapinga vikali mpango wa kuiona URUSI kama adui. Wanahitaji washirikiane na Urusi kwa vile ni weupe wenzao. Kwa hivi sasa Amini usiamini Wabaguzi wa Urusi wanashangilia siku ya kuzaliwa kwa Adolf Hitler.
 
Back
Top Bottom