kilwakivinje
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 6,000
- 9,091
Kwa haya uliyoyasema unahisi jamaa ni dhaifu???KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schroeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.
KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.
KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.
KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union
NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??